January 04, 2014

MADIWANI BUMBULI WAPEWA SOMO.

       (Katibu wa January Makamba(Hoza Mandia ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Milingano)
 
Na Raisa Said, Bumbuli
Imewekwa Januari 4.
MADIWANI  wa Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto wametakiwa kusimamia ipasavyo maazimio na mikakati wanayopitisha katika vikao vyao  ili kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo.

Ushauri huo umetolewa na Mbunge wa Jimbo la Uchaguzi la Bumbuli, January Makamba akizungumza katika mahojiano na waandishi wa Habari hivi karibuni kufuatia kikao maalumu cha wajumbe wa Kamati ya Madiwani wa CCM kilichoitishwa kwa niaba yake na Katibu wake Hoza Mandia.
Mbunge huyo amesisitiza kuwa madiwani wanapaswa kusimamia maazimio waaliyoyapitisha katika kikao hicho ili kuiharakisha maendeleo kwa wananchi wa eneo hilo ambalo limebahatika kuwa Halmashauri kamili.

Katika maazimio hayo madiwani walimshauri Mbunge ajipangie utaratibu wa kuwasIliana kwa simu na madiwani angalau kila baada ya wiki au kadri atakavyoona inafaa zaidi ili kupata taarifa na kujua changamoto gani zilizopo katika jimbo hilo.

Pia waliazimia kuwa kero zote za wananchi zinazohusui miradi ya maendeleo ziwasiklishwe kwa kupitia vikao husijka na madwani wahusike kumuona mkurugenzi ili kupata majibu ya ufumbuzi wa kero hizo

Kikao hicho pia kiliazimia kuwa kila diwani awe amekamilisha na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwenye vikao husika  ndani ya mwezi mmoja na nakala ya taarifa hiyo iliyopitishwa iwasilishwe kwa katibu wa CCM wilaya na kwa mbunge.

Mbunge huyo alisisitiza kuwa hayo yote yaliyoazimiwa yasimamiwe kwa faida ya wananchi na Chama cha mapinduzi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »