MGAMBO SHOOTING,COASTAL UNION HAKUNA MBABE.

November 02, 2013


Na Oscar Assenga, Tanga.
TIMU za soka Mgambo Shooting na Coastal Union zote za mkoani Tanga leo zimeshindwa kutambiana baada ya kulazimisha suluhu pacha ya kutokufungana katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa dimba la soka Mkwakwani.

Katika mchezo ambao ulikuwa wa kawaida ulishuhudiwa mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza timu hizo zikitoka sare ya kutokufungana mchezo ambao ulikuwa mkali.

Raundi ya lala salama katika mchezo huo ilianza kwa kasi ambapo kila timu iliweza kulisakama lango la mwenzie kwa kushambuliana kwa zamu ambapo kwenye dakika ya 60 Mgambo Shooting walifanya mabadiliko kwa kumtoa Martin Mlolera na kumuingiza Full Maganga huku Coastal Union wakimuingiza Yayo Lutimbba na kumtoa Seleman Kassim Selembe.

Hali kadhalika Coastal Union kwenye dakika ya 71 walimtoa Haruna Moshi Boban na kumuingiza Daniel Lyanga ambapo kutokana na mabadiliko hayo,Coastal Union waliweza kuimarisha nguvu ambapo dakika 72 Yayo Lutimba alimanusura aipatia bao timu hiyo baada ya kupiga shuti kali lililogonga mwamba na kurudi uwanjani.

Kikosi cha Coastal Union leo kiliwakilishwa na mlinda mlango,Shabani Kado,Hamad Hamisi,Othumani Tamimu,Mbwana hamisi,Juma Nyoso,Jerry Santo,Uhuru Seleman,Crispine Odulla,Daniel Lyanga,Keneth Masumbuko.

Kwa upande wa Mgambo Shooting,Mlinda Mlango,Godson Mmasa,Salum Mlima Bashiru Chanache,Novart Lufunga,Bakari Mtama,Salum Kipanga,Malimi Busungu,Mohamed Samata,Omary Juma,Martin Mlolera na Peter Mwalyanzi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »