Mradi wa kituo cha Kupoozea umeme Sahare ni juhudi za Serikali Kuu.

May 19, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
IMEELEZWA kuwa mradi wa kituo cha kupozea umeme kilichopo Sahare (33/11Kv,15MVA)ni muendeleo wa Juhudi za serikali kuu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hapa nchini kuendeleza usambazaji wa umeme wa uhakika katika maeneo yote hapa nchini.

Kauli hiyo imetolewa  na Mkurugenzi wa Millenium Challenge Tanzania,Mhandisi,Ipack Chanji wakati akitoa taarifa ya mradi wa kituo hicho kidogo cha kusambazia umeme Sahare kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa 2013 ambapo amesema mradi huo ulianza Juanri mwaka 2011 na unatarajiwa kukamilika Julai 2013.

Chanji amesema mradi huo ni utatumia kiasi cha (dola 1,541,408.95) ambazo ni sawa na shilingi za kitanzania 2,508,643,066.12(Bilioni mbili milioni mia tano na nane,laki sita arobaini na tatu elfu sitini na sita na senti kumi na mbili) zilizopatikana kupitia akaunti ya changamoto za millennia ikiwa ni msaad wa watu wa marekani.

Amesema faida za mradi huo ni kuongeza nguvu ya umeme hasa kwa maeneo ya viwandani kitendo ambacho kitavutia wawekezaji ndani na nje pamoja na kupatikana  umeme wa uhakika kwa mahitaji ya nyumbani na maofisini na hivyo kuongeza tija kwenye uzalishaji mali hasa za viwandani ikiwemo kukua kwa pato la Taifa.

Mwenge huo umezindua miradi 7 yenye thamani ya bilioni 8 katika wilaya ya Tanga ambayo ni maabara katika shule ya sekondari st.christina,barabara ya viwandani,chama cha ushirika wafugaji maziwa kichangani,umeme,

  Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »