Jana huko Mjini Khartoum, Sudan ndio ilifanyika Droo ya Timu 13 kupangwa Makundi matatu na Droo hiyo ilisimamiwa na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kagame Cup, Raoul Gisanura, wa kutoka Rwanda.
KUNDI A:
Merrickh El Fasher (Sudan), Simba (TZ), Al Mann (Somalia), APR (Rwanda).
KUNDI B:
Hilal Kadougli (Sudan), Ahli Shandi (Sudan), Al Nasr (S.Sudan), Tusker (Kenya), Super Falcon (Zanzibar).
KUNDI C:
Yanga (Tanzania), Express FC (Uganda), Vital O (Burundi), AS Port (Djibouti)
Mashindano haya yatachezwa kwa Wiki mbili katika Miji ya Kaskazini ya Sudan, Al Fasher na Kadugli, South Kordufan State, na Yanga, ambao ni Mabingwa Watetezi, wanawania kutwaa Ubingwa huu kwa mara ya 3 mfululizo.
Zanzibar wanawakilishwa na Super Falcon ambao walitwaa Ubingwa wa Zanzibar Msimu wa 2011/12 lakini hivi sasa, huko Visiwani, wameshashushwa Daraja.
Zanzibar wanawakilishwa na Super Falcon ambao walitwaa Ubingwa wa Zanzibar Msimu wa 2011/12 lakini hivi sasa, huko Visiwani, wameshashushwa Daraja.
Super Falcon wataanza kucheza Juni 18 na Tusker ys Kenya huko Kadugli, South Kordufan State, Sudan.
Mashindano haya yanadhaminiwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, na zawadi ni Dola 60,000.
EmoticonEmoticon