MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

June 14, 2025 Add Comment

Na John Mapepele

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini kuwaongeza wananchi katika maeneo yao kufanya "jogging" na mazoezi ili kuimarisha afya.

KAMISHNA WA UMEME NA NISHATI JADIDIFU AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA UMEME JIJINI DAR ES SALAAM

June 14, 2025 Add Comment


▪️Aridhishwa na hatua ya utekelezaji wa miradi


▪️Awataka wakandarasi kuzingatia viwango na TANESCO kuongeza usimamizi ili kuepuka ongezeko la gharama


▪️Aisisitiza dhamira ya Serikali ya kuhakikisha Watanzania wanapata umeme wa uhakika


Na. Agnes Njaala, Dar es Salaam


Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga, tarehe 12 Juni 2025, amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme ya Gridi Imara inayoendelea katika Jiji la Dar es Salaam, na kutoa maelekezo muhimu kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo.


Miradi hiyo inalenga kuimarisha upatikanaji wa umeme kwa kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha huduma bora na ya uhakika kwa wananchi.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Kamishna amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, licha ya changamoto mbalimbali za kimazingira, na kusisitiza umuhimu wa kuendelea na jitihada za kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.


“Nimeridhishwa na hatua zilizofikiwa, lakini nimeagiza wakandarasi waharakishe kazi, vifaa vipatikane kwa wakati, na viwango vya kazi vizingatiwe ili miradi hii itoe matokeo yaliyokusudiwa kwa wananchi,” amesisitiza Mhandisi Luoga.


Akifafanua amebainisha kuwa miradi hiyo ya kimkakati, inayotekelezwa na TANESCO kwa ufadhili wa Serikali, inalenga kuboresha huduma ya umeme kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini. Aidha, ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuidhinisha rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo muhimu.


Katika maagizo yake, ameitaka TANESCO kuongeza usimamizi kwa wakandarasi katika kuhakikisha upatikanaji wa vifaa kwa wakati, na kusimamia ubora wa kazi ili kuepuka ongezeko la gharama zitokanazo na ucheleweshaji.

Kwa upande wake, Mhandisi Abdallah Chikoyo, Meneja wa Miradi ya Kuzalisha Umeme TANESCO aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji , ameahidi kuongeza juhudi katika usimamizi wa miradi na kuweka mipango kazi inayotekelezeka kwa wakati.


“Tumejipanga kuongeza nguvu katika usimamizi wa miradi hii, na kuimarisha ushirikiano na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa ufanisi, tukitimiza wajibu wetu katika kuboresha huduma ya umeme nchini,” amesema Mhandisi Chikoyo.


Ziara hiyo ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa Serikali katika kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambapo Kamishna Luoga alitembelea vituo vya umeme vya Ubungo I, Mabibo, Kinyerezi na Gongo la Mboto. Katika vituo hivyo, kazi ya ufungaji wa mashine umba zenye uwezo mkubwa  (transformers) inaendelea kwa kasi ya kuridhisha, ikiwa ni hatua ya kuimarisha miundombinu ya usambazaji wa umeme jijini Dar es Salaam.

MWENGE WA UHURU 2025 KUPITIA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 3 WILAYA YA TANGA

June 14, 2025 Add Comment










Na Paskal Mbunga,TANGA

MWENGE wa Uhuru unatarajiwa kuwasili katika wilaya ya Tanga Jumatatu June 16 mwaka huu na upitia katika miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya Sh.Bilioni 3,058,289,671.99.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa za ujio wa Mwenge huo,Mkuu wa wilaya ya Tanga Dadi Kolimba alisema wataupokea ukitokea wilayani Mkinga katika uwanja wa shule ya Msingi Mabambani Mtaa wa Mpirani Kata ya Chongoleani.

Aliitaja miradi ambayo itapitiwa na Mwenge ni ujenzi wa madarasa 4 ya Ghorofa ,matundu 13 ya vyoo na ofisi shule ya Msingi Mbuyuni yenye thamani ya Milioni 388,769,596.80 na Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ya awali ya mfano shule ya msingi Mwakidila yenye thamani ya Milioni 70,100,000.00.

Mkuu huyo alisema pia miradi mingine ni ujenzi wa ofisi ya mtendaji kata ya Tongoni uliogharimu kiasi cha sh.Milioni 85,000,000.00,ujenzi wa barabara ya Sahare awamu ya kwanza na ya pili yenye urefu wa mita 600 kwa kiwango cha lami uliogharimu Sh.Milioni 489,606,700.00.

“Lakini pia Mwenge utapita katika ujenzi wa Jengo la X-Ray kituo cha Afya Makorora wenye thamani ya Sh.Milioni 84,721,640.00 pamoja na mradi wa ufungaji wa dira za maji za malipo ya kabla awamu ya kwanza wenye thamani ya Sh. 1,872,091,735.00 “Alisema.

Hata hivyo alisema kwamba mradi mwengine ambao utapitiwa na mwenge ni mradi wa kikundi cha vijana cha kutengeneza gypsum wenye thamani ya Sh.Milioni 68,000,000.00

Alisema mbali na miradi hiyo saba mwenge wa uhuru utakagua shughuli za maandalizi ya uchaguzi,kongamano la vijana pamoja na maswala mtambuka.

Mwisho.

KAMPENI YA PIKA SMART INAYOHAMASISA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAZINDULIWA

June 13, 2025 Add Comment


*📌 Kamishna Luoga asisitiza matumizi ya umeme katika Nishati Safi ya Kupikia*


Kamishina wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga amezindua kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ya umeme inayokwenda na kaulimbiu ya PIKA SMART.


Mha. Luoga amezindua kampeni hiyo leo Juni 13, 2025 jijini Dar es Salaam akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi  Mramba. 


Kampeni hiyo imeandaliwa na Shirika la Modern Energy Cooking Services (MECS) chini ya ufadhili wa UKAID kwa kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya Nishati.


Mhandisi Luoga amesema kampeni hiyo imezinduliwa ikiwa ni mojawapo ya jitihada za Serikali kuhakikisha inawahamasisha wananchi kutumia nishati safi ya kupikia ili kufikia lengo la asilimia 80 ya watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034. 

Luoga amewatoa hofu wananchi kuhusu kutumia nishati safi ya kupikia ya umeme akitanabaisha kuwa ni salama na gharama nafuu na kuongeza kuwa Tanzania Ina Umeme mwingi na wa kutosheleza mahitaji.

"Kama tunavyofahamu bwawa la kufua umeme kwa maji la Julius Nyerere limekamilika na hivyo kupelekea umeme uliopo nchini hadi sasa kufikia takribani megawati 4,031,  umeme huu umeshafika  katika Vijiji vyote 12, 318 vya Tanzania  hivyo kuna kila sababu kwa wananchi kutumia nishati safi ya umeme kupikia." amesema Mha. Luoga



Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Mkurugenzi wa Mipango na uwekezaji TANESCO, Mhandisi Henryfried Byabato amesema Shirika hilo limekuwa likihamasisha wananchi kutumia nishati safi ya kupikia ya umeme kutokana na uwepo wa kutosha wa nishati hiyo nchini.

Ameongeza kuwa, teknolojia  zimeboreshwa hivyo majiko ya umeme yanatumia nishati kidogo na kwa ufanisi mkubwa.

Kampeni hii ya kuhamasisha matumizi ya pika smart imekuja wakati muafaka ambapo Wizara ya Nishati imezindua mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wenye lengo la kutoa mwongozo kwa wadau kuendeleza kampeni ya uhamasishaji matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye ni kinara wa nishati safi ya kupikia kuhakikisha watanzania wanahama kutoka kwenye matumizi ya nishati isiyo safi kwenda kwenye nishati safi



RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI REA KUHARAKISHA UTEKEZAJI MIRADI YA UMEME JUA VISIWANI

June 13, 2025 Add Comment


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi wa usambazaji wa mifumo midogo ya umeme jua katika maeneo ya visiwani kuhakikisha wanatumia muda vizuri na kukamilisha kazi kwa wakati, ili kuwaondolea wananchi wa maeneo hayo adha ya ukosefu wa nishati ya uhakika.


Akizungumza leo Juni 13, 2025 ofisini kwake jijini Mwanza, Mhe. Mtanda amewataka pia wataalamu kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikisha kuwa wakandarasi wanalipwa kwa wakati, jambo litakalowasaidia kuendelea na kazi bila kuchelewa.

“Ni muhimu kutumia muda vizuri na kukamilisha miradi hii kwa wakati. Serikali inatambua juhudi za kila mkandarasi anayefanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi, na hao ndio wanaopewa kazi nyingine zaidi. Chema chajiuza, kibaya chajitembeza,” amesema RC Mtanda.


Mkuu huyo wa mkoa pia amewasisitizia wakandarasi umuhimu wa kujitambulisha kwa mamlaka za mikoa, wilaya, tarafa na vijiji ili jamii ziwe na uelewa wa mradi huo, kushirikishwa kikamilifu na kutoa maoni, taarifa au mapendekezo yatakayosaidia kufanikisha utekelezaji wake.

“Kwa kufanya hivyo, mtapata ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi. Na pale changamoto zinapojitokeza, ni rahisi kupata msaada au taarifa muhimu kutoka kwao,” aliongeza.


Kwa upande wake, Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Ernest Makale, amesema mradi huo wa umeme wa jua unatekelezwa katika visiwa 78 vilivyopo wilaya tano za Mkoa wa Mwanza ambazo ni Sengerema, Buchosa, Ukerewe, Magu na Ilemela.

Mhandisi Makale Pia amebainisha  kuwa zaidi ya shilingi bilioni 4 tayari zimetengwa kwa ajili ya mradi huo, ambao unalenga kufikisha huduma ya umeme katika nyumba takribani 8,410 kwa bei ya ruzuku ya mpaka asilimia 75.


Lengo kuu la mradi huo ni kuhakikisha kuwa wakazi wa maeneo ya visiwani wanapata huduma ya nishati ya umeme ya uhakika, jambo litakaloboresha maisha yao na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo husika.


Mwisho.