WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ZANZIBAR AZINDUA MAONYESHO YA MADINI LINDI

June 12, 2025 Add Comment

 

Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.

Na Fredy Mgunda, Ruangwa, Lindi.


Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Kaduara alisema thamani ya dhahabu imeendelea kupanda katika soko la dunia kutokana na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine, ambako dhahabu inayozalishwa na Urusi imewekewa vikwazo kuingia katika masoko ya kimataifa.


"Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya 1996, pamoja na Sera ya Maendeleo ya Viwanda ya 1996–2020 na ile ya Viwanda Vidogo ya mwaka 2003, zipo kwenye mchakato wa kupitia upya kwa lengo la kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo ya kimkakati," alisema Kaduara.


Waziri huyo alibainisha kuwa miradi ya madini ni miongoni mwa miradi ya kimkakati nchini, ambayo inaendelea kufanyiwa tathmini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sera mpya itakayowezesha Watanzania kunufaika zaidi na sekta hiyo.


Lindi Yajitokeza Kama Kitovu cha Madini Nchini

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack, alisema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali kubwa za madini ambazo tayari zimeanza kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.


“Maonyesho haya yanafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Yanachochea uchumi wa eneo hili na kuongeza thamani ya madini tunayochimba,” alisema RC Telack.


Aliongeza kuwa maonyesho ya awamu ya kwanza mwaka 2023 yalivutia wageni kutoka mataifa 14 na zaidi ya watu 6,000 walihudhuria, jambo lililoongeza hadhi ya Lindi kama eneo la kimkakati kwa shughuli za madini nchini.


“Kwa sasa tunaona ongezeko la wawekezaji, uboreshaji wa miundombinu na fursa za ajira, hali inayodhihirisha kuwa Lindi ni sehemu muhimu katika ajenda ya maendeleo ya taifa,” aliongeza.


Ongezeko la Wachimbaji na Teknolojia ya Uchimbaji

Kwa mujibu wa Mratibu wa Maonyesho hayo, Bw. Mwinjuma Mkungu, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi mkoani Lindi, idadi ya wachimbaji imeongezeka kutoka 2,265 hadi 2,948 baada ya maonyesho ya kwanza, huku mitambo ya kisasa ya uchimbaji ikiongezeka pia.


“Tumeona ongezeko kubwa la wawekezaji na mapato ya serikali yameongezeka kwa asilimia 10.1 baada ya maonyesho ya awali. Hii inaonyesha mchango wa moja kwa moja wa maonyesho haya kwa uchumi wa taifa,” alisema Mkungu.


Alfred Chilumba, mchimbaji mdogo, alishuhudia mabadiliko makubwa baada ya kupata elimu kupitia maonyesho ya awali.


“Tulikuwa hatujui kama tunaweza kutumia mitambo ya kisasa. Maonyesho haya yametufungua macho,” alisema.


Anna Milanzi, mama lishe anayehudumu kwenye maonyesho hayo, alisema ametumia fursa ya ongezeko la wageni kuongeza kipato chake.


“Kwa siku za kawaida napika kilo 5 za unga, lakini leo nimepika kilo 15. Biashara imenoga,” alisema kwa furaha.


Maonyesho Yadumu kwa Siku Kadhaa

Maonyesho hayo ya siku kadhaa yanahusisha maonesho ya bidhaa za madini, teknolojia mpya za uchimbaji, warsha za kitaalamu, na majadiliano baina ya serikali, wawekezaji na wachimbaji wadogo.


Yamebeba kauli mbiu: “Madini na Uwekezaji wa Fursa za Kiuchumi Lindi – Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025”, yakisisitiza uhusiano kati ya maendeleo ya sekta ya madini na ushiriki wa wananchi katika mustakabali wa taifa.

KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA

June 12, 2025 Add Comment

 

 



Na Mwandishi wetu Dodoma.

Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.

Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.

Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji.










Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.


Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.

Mwisho

WAZAZI WAASWA KUTOCHANGIA MMOMONYOKO WA MAADILI KWA WATOTO

June 12, 2025 Add Comment


Serengeti-Mara.


Polisi Kata wa Kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Sajenti Emmanuel, ametoa wito kwa wazazi kutokuwa chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa watoto wao. 


Ametoa kauli hiyo wakati akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wananchi wa kitongoji cha Momorogoro kijiji cha Robanda, kata ya Ikoma, katika mwendelezo wa kampeni ya Elimu ya Nyumba kwa Nyumba.


Katika maelezo yake, Sajenti Emmanuel amewakumbusha wazazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuiandaa vyema kesho ya watoto wao kwa kuwapatia malezi bora, ambayo yatawasaidia kuwa watu wenye tija na mafanikio katika nyanja za elimu, afya, na uchumi.

Aidha, aliwasisitiza wazazi kuwafundisha watoto wao kuvaa mavazi ya heshima yanayomstiri mtu, kudumisha usafi wa mwili, mavazi, na mazingira yanayowazunguka, kama njia ya kulinda maadili yao.


Aliwakumbusha wazazi kuwa urithi wa kudumu ambao wanaweza kuwaachia watoto wao ni elimu, alisema itawapatia maarifa muhimu katika kipindi chote cha ukuaji wao na kuwasaidia kuwa watu wanaofaa na kuheshimika katika jamii.

MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI YA 7 YA THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 WILAYA YA MUHEZA

June 11, 2025 Add Comment

 


Na Siwema Afisa Habari MUHEZA

MWENGE wa Uhuru unatarajiwa kuwasili katika wilaya ya Muheza Ijumaa June 13 ukitokea wilaya Korogwe ambapo utazindua miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Biloni 1.6 na utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 90.4.


Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema wataupokea mwenge huo ukitokea wilaya Korogwe na ukiwa kweye wilaya hiyo utaweka mawe ya msingi miradi miwili,miradi minne itazinduliwa na mmoja utakaguliwa

Akizungumza maandalizi ya ujio huo wa mwenge mwaka huu alisema kwamba mwaka jana walikuwa namba moja kimkoa wilaya ambapo alisem wamejipanga katika maeneo ya miradi kuhakikisha inakuwa bora na viwango lakini kuhakikisha hamasa ya kutosha inakuwepo eneo la mpokezi,kwenye miradi na mkesha.

Aidha alisema katika mkesha wa mwenge huo wa uhuru watakuwepo wasanii mbalimbali ili kuweza kutoa burudani mbalimbali kwa wakazi wa mji huo na wageni ambao watashiriki huku akitoa wito wajitokeze kwa wingi kwa maana utakuwa wa aina yake kutokana na namna walivyojipanga.

Hata hivyo alisema pia watakuwa na kongamano maalumu la vijana na Mgeni rasmi atakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchjini (TIC) Gilead Teri sambamba na watoa mada mashuhuri na wabobezi .

Mwishi

MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 18 KUKAGULIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI LUSHOTO

June 11, 2025 Add Comment

 



Na Ashrack Miraji, 

Mwenge wa Uhuru umeingia rasmi katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto leo, baada ya kukabidhiwa kutoka Halmashauri ya Bumbuli, ambapo utakimbizwa umbali wa kilomita 112.8 kupitia tarafa mbili, kata nne na vijiji 23. Katika mbio hizo, Mwenge utakagua na kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.8.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, alisema kuwa kaulimbiu ya Mwenge wa mwaka huu ni: “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu,” ambayo inaakisi dhamira ya kitaifa ya kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mchakato wa kidemokrasia kwa njia ya amani na utulivu.

“Tumepokea Mwenge wa Uhuru tukiwa na maandalizi kamili. Kauli mbiu ya mwaka huu ni wito kwa kila Mtanzania kushiriki uchaguzi mkuu ujao kwa njia ya amani, busara na utulivu,” alisema Sumaye.

Aliongeza kuwa Mwenge huo utakagua na kuzindua miradi saba ya maendeleo inayogusa sekta mbalimbali kama elimu, afya, maji na miundombinu, ikiwa ni ishara ya dhamira ya Serikali katika kuwahudumia wananchi, hasa wa maeneo ya vijijini.


“Kwa jumla, miradi tunayokwenda kukagua ina thamani ya shilingi bilioni 1.8. Hii inaonesha jitihada kubwa zinazofanywa kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi wote,” aliongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Sumaye pia alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge huo, sambamba na kudumisha mshikamano na amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenge wa Uhuru ni alama ya mshikamano wa kitaifa na maendeleo, ambao huzunguka nchini kote kila mwaka tangu mwaka 1961 kwa lengo la kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji wa kijamii, mshikamano wa kitaifa, na sasa zaidi — ushiriki wa amani katika chaguzi za kidemokrasia.