WAKUU WA VITENGO REA,TARURA,RUWASA WAKUTANA KUJENGEANA UWEZO

June 11, 2025 Add Comment

 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bi. Martha Chassama amekutana na kuzungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasilino wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Bi. Catherine Sungura na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Masoko wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Bw. Athumani Shariff katika kikao kifupi kilichofanyika jijini Dodoma.   Kikao hicho kifupi kililenga kujengeana uwezo wa taasisi hizo hususan katika maeneo ya vijijini ili kuongeza chachu katika maeneo hayo.







VIJANA ZAIDI YA 350 KATIKA JIJI LA TANGA KUNUFAIKA NA MRADI WA INCLU-CITIES PROJECT

June 11, 2025 Add Comment





Na Oscar Assenga, TANGA

ZAIDI ya Vijana 350 Jijini Tanga wanatarajiwa kunufaika na mradi wa Inclu-Cities Project uliopo chini ya Programu ya SASA kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Ubelgiji (ENABEL) kupitia ufadhili wa Umoja wa Ulaya .

Hayo yalisemwa leo wakati wa uzinduzi wa utambulisho wa mradi huo uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian uliofanyika kwenye ukumbi wa chuo hicho.
Akizungumza katika uzinduzi huo wakati akitoa taarifa yake wakati wa utambulisho wa mradi huo ,Mkuu wa Chuo cha Veta Tanga Gidioni Lairumbe alisema wakiwemo wanawake asilimia 50 katika Jiji la Tanga bila kusahau uchumi wa bluu ambapo program hiyo ni kuwaandaa na kuwajengea uwezo wa kujiajiri au kuajiwa vijana 150 asilimia 50 wasio na ujuzi kabisa katika fani mbalimbali.

Alizitaja fani hizo ni usindikaji na uandaaji wa chakula,Umeme wa Sola,Uchomeleaji na uungaji wa vyumba pamoja na utengenezaji wa mkaa mbadala ikiwemo mpango wa kuwapa ujuzi vijana walio sokoni ambao utawagusa vijana 150 ikilenga asilimia 50 ya wanawake katika fani.

Mkuu huyo wa chuo cha Veta alizitaja fani hizo ni Usindikaji na uandaaji wa chakula,uvuvi,Umeme wa sokla na uchomeleaji na uungaji wa vyuma sambamba na program ya utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo usio rasmi ambao utawagusa vijana 150 ukilenga wanawake kwa asilimia 50 katika fani za usindikaji na uandaaji wa chakula,uchomeleaji na uungaji wa vyuma,matengenezo ya pikipiki za umeme na matengenezo ya siku za mkononi.

Alisema kupitia mradi wa utekelezaji wa mradi huo wa Inclu –Cities uliopo chini ya Programu ya SASA kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Ubelgiji (ENABEL) kwa ufadhili wa umoja wa ulaya pia kitaanzishwa kitengo cha utoaji wa ushauri wa masuala mbalimbali yahusuyo ujuzi na huduma mbalimbali kwa wanafunzi ,Ukarabati wa jengo la mgahawa pamoja na jiko kama eneo la kujifunzia wanafunzi wa mapishi na kupata vifaa mbalimbali vya kujifunzia

“Lengo kuu la mradi huu ni kuimarisha mafunzo ya ufundi stadi kwa lengo la kuzalisha wahitimu wanaohitajika katika soko la ajira na kuifanya VETA Tanga kuwa kituo cha Umahiri wa Utoaji wa Mafunzo ya Ufundi Stadi katika Sekta husika waweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kukamilika mafunzo hayo “Alisema Mkuu huyo wa chuo cha VETA Tanga.

Alisema kwamba wanaimani kwamba elimu ya vitendo na ushirikiano kati ya waajiri na wadau mbalimbali wa maendeleo itasaidia kuelekea kupunguza ukosefu wa ajira na kuongeza kipato kwa wahitimu na kuwategemea baada ya mafunzo haya zaidi ya asilimia 75 ya wahitimu watakaopata ujuzi watakuwa katika nafasi nzuri ya kuingia kwenye soko kwa kujiamini.

Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian alisema kwamba wanaendelea kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa mambo makubwa anayoyafanya yanayopelekea kuungwa mkono na nchi mbalimbali wakiwemo umoja wa ulaya na wamefurahi mradi huo ambao una jumla ya Uero milioni 75 ambazo ni sawa na Bilioni 190 ni jambo kubwa ambalo litasaidia katika mipango ya program mbalimbali

“Lakini niwapongeze Veta kama sehemu ya mradi mliwasiliana na Umoja na Ulaya walipokuja kuwaona wakawa tayari kutekeleza mradi na Jiji na Veta Makao Makuu ambao walikubali mpango huo kuweza kufanyika kwenye maeneo yao na Tanga kwa moja wapo na sisi tunashukuru na kuwapongeza kwa hatua hii nzuri na muhimu kwa maendeleo na huo ndio umuhimu wa uwepo wa chuo hiki”Alisema

Aidha alitaka mchakato wa kuwapata walengwa katika mradi huo wapate vijana wanaotoka kwenye familia ambazo hazina uwezo na ambao watakaotoka wataweze kuwasaidia familia wachague mchanganyiko na wasaidiane na madiwani kuwaibuua watu ambao watakwenda kuwaheshimisha fursa hiyo na kupata kitu baadae cha kubadilisha maisha yao.

Alisema kwamba katika miaka 50 ya chuo cha Veta ndio ambao ambacho kitawakomboa watanzania hasa vijana katikati kulikuwa na wimbi la vyuo vyote za ufundi kuwa kuwa vyuo vikuu lakini misingi ya Baba wa Taifa na dhana ya ujamaa wa kujitegemea ilikuwa ni kupitia mifumo ya vyuo vya ufundi lakini na shule za amali ambazo sasa serikali imerudisha zitawakomboa vijana

Aliongeza kwamba vitawakomboa kwa sababu watatoka wakiwa na maarifa ya jinsi ya kumudu mazingira yao na kinachofanyika ni kuzuri kitasaidia vijana wao huku akiwataka chuo hicho kuendelea kuwapika vijana vizuri waandalieni stadi mbalimbali ikiwemo bustani za maua za kisasa.


Naye kwa upande wake Mshauri Mtaalamu wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Ubelgiji (ENABEL) Thomas Aikaruwa Aliwapongeza Veta Tanga kwa kuamua kuanza safari ya maboresho kwenye chuo chao na kuwa kituo cha umahiri kwenye maeneo walioyaainisha.

Alisema kwamba Umoja wa Ulata kupitia Mpango wa Green City chini ya Mpango wa SASA watafanya kazi na Serikali ili kuchangia kwenye mikoa ya Tanga,Mwanza na Pemba lengo kusaidia kuboresha maisha ya watanzania wa kawafikia kwenye miji hiyo mitatu kwa kuboresha miundombinu inayozingatia mabadiliko ya tabia ya nchi.

Alisema pia katika kuboresha hudumu za kijamii kwa wananchi wanaopatikana kwenye mikoa hiyo kwa kuongeza ukuaji uchumi wa mwananchi wa kawaida katika mikoa hiyo katika ukuaji wa uchumi wa mwananchi huyo ambapo mradi huo chini ya shirika la Ujerumani Enable linafanya kazi kwa ukaribu na wadau muhimu katika sekta hiyo ya kukuza ujuzi hasa wadau wanaofanya shughuli zao kwenye maeneo hayo wanafanya kazi.

Aidha aliwataja wadau hao kuwa ni Veta na Veta ya Pemba na Sido Tanga na Mwanza ikiwemo sekta binafsi ambazo zinapatikana kwenye mikoa hiyo mitatu chini ya uangalizi wa Halmashauri zinazopatikana kwenye mikoa hiyo ya Tanga,Ilemela ,Nyamagana-Mwana na Chakechake-Pemba na nyengine ambazo zinavutiwa kuingia kwenye mpango huo.

Hata hivyo alisema kwamba ujuzi ni dhana muhimu katika kipindi waliochopo hasa ukizingatia mabadiliko ya mitaala ya elimu na wanategemea kutoka na ujuzi hasa mabadiliko ya kisasa na kuibua na kutengeneza ajira ili kuimarisha zilizopo ili viweze kuwa na tija na maeneo yanayotazamiwa kufikiwa.

“Maeneo tunayotazamiwa kufikiwa ni utumiaji huduma za kibiashara na kifedha na uwekezaji kuwe na ubora na mafunzo ya ujuzi yanayotolewa na taasisi zilizotajwa yanayozingata mahitaji ya sasa na ujasiriamali na bajeti ya shughuli zao ni Bilioni 190 ambazo ni kama euro milioni 75 na muda wa mradi huo ulianza mwaka 2022 na utakwenda mpaka mwaka 2027”Alisema

Mwisho.

TPDC YATOA GAWIO LA SHILINGI BILIONI 11.7 KWA SERIKALI

June 10, 2025 Add Comment
SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imetoa gawio la shilingi Bilioni 11.7 kwa Serikali kwa mwaka 2025, likiwa ni ongezeko mara mbili walilotoa mwaka jana 2024 shilingi Bilioni 5.8.

MD TWANGE AENDELEA KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

June 10, 2025 Add Comment


📌Atumia sehemu ya ziara yake kuelimisha na kugawa zawadi za majiko janja kwa viongozi wa Serikali za Mikoa na Wilaya Kanda ya ziwa


📌Asisitiza wananchi wasiogope kupika kwa umeme kwani ni gharama nafuu.


Katika kuhakikisha elimu ya  nishati safi ya kupikia inamfikia kila Mtanzania, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ametumia sehemu ya ziara yake ya kukagua maendeleo ya miradi ya umeme katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupika kwa umeme kwa viongozi wa  Serikali za Mikoa na Wilaya ili kuongeza uelewa zaidi kwa wananchi.

Bw. Twange ametumia nafasi hiyo  kuelimisha na kutoa zawadi za majiko janja yenye teknolojia inayotumia umeme kidogo kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  Mhe.Saidi Mtanda, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi Pamoja na  Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Wakili Julius Mtatiro ikiwa ni sehemu ya Kampeni ya TANESCO ya kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia umeme.

Amesema  licha ya  Shirika hilo kujikitika katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme wa uhakika bado wanajukumu la kutekeleza kwa vitendo Ajenda  ya Mhe. Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanatumia nishati safi kwa ajili ya kupikia na ametoa majiko hayo kwa viongozi wa Serikali ili kupata picha halisi ya unafuu wa kutumia umeme kupikia ili kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi.

‘’Vifaa hivi vinatumia umeme kidogo kwenye kupika na tumetoa majiko haya kwa ajili ya matumizi ya kupikia  ili mtusaidie kuwahamasisha na kuongeza uelewa kwa wananchi kwa kuwa mtakuwa mashahidi na  mabalozi wazuri wa kueleza faida za majiko hayo hatua itakayowavutia  zaidi wananchi kisha kubadili mitazamo’’ amesisitiza Bw Twange

Naye Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Wakili Julius Mtatiro ameipongeza TANESCO kwa mkakati huo ambao unadhamira ya dhati ya kufanya mageuzi ya elimu ya matumizi ya nishati safi ili kuwafanya wananchi kuachana na matumizi ya nishati isiyo salama  zenye athari kiafya kwa watumiaji na chanzo cha uharibifu wa mazingira.

‘’Tumepokea zawadi ya jiko hili tunashukuru, tutaitumia mikutano yetu na wananchi kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi na wananchi wetu ni waaminifu ninaamini wataelewa na kwa sasa  tutawaelimisha kwa vitendo,’’ alifafanua Mhe. Mtatiro.


Ziara ya Mkurugenzi wa TANESCO Bw. Lazaro Twange katika Mikoa ya kanda ya ziwa imelenga kukagua miradi mbalimbali ya uzalishaji umeme lakini pia ametumia nafasi hiyo kuongeza msisitizo wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ya umeme ikiwa ni muendelezo wa kampeni inayofanywa na TANESCO ya kuhakikisha ajenda ya Serikali inafanikiwa.

TUME YA UCHAGUZI YAPONGEZWA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU 2025

June 09, 2025 Add Comment

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kilichokutana Mjini Unguja Zanzibar leo Juni 9,2025.
 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume akizungumza mapema kabla ya ufunguzi wa kikao hicho.




Wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia mada katika Mkutano huo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  wakati Katibu Mkuu huyo alipofika kufungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kushoto)  na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  pamoja na wajumbe wa baraza la Wafanyakazi la Tume wakiimba wimbo wa wafanyakazi wakati kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Wafanyakazi  Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025. 


Na. Mwandishi Wetu, Zanzibar
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz ameipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kukamilisha zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuendelea vyema na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
 
Dkt. Yonazi ametoa pongezi hizo leo tarehe 09 Juni, 2025 Kisiwani Unguja, Zanzibar wakati wa kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi la INEC,  ambapo imewaasa viongozi wa Tume kuendelea kuwa imara na kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakwenda vizuri.
 
“Kwanza niwapongeze sana kwa kukutekeleza jukumu hili kubwa ambalo mmekabidhiwa na Taifa letu na kwa namna ya pekee kabisa Mwenyekiti wa Baraza unifikishie salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele pamoja na wajumbe wa Tume kwa kazi kubwa ambayo mmeifanya katika kuhakikisha kuwa shughuli za uchaguzi nchini kwetu zinakwenda vizuri,” amesema Dkt. Yonazi.
 
Ameeleza kuridhishwa na jinsi Tume ilivyotekeleza kwa ufanisi zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuongeza kuwa ni matarajio ya Serikali kuwa utendaji huo mzuri wa Tume utaendelea kwa viwango vya juu kwa mujibu wa katiba, sheria na taratibu mbalimbali ambazo zimewekwa.
 
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndugu. Kailima Ramadhan amesema tayari Tume imekamilisha awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kwa sasa inaendelea na uboreshaji wa awamu ya pili.
 
“Tume imeshakamilisha uboreshaji wa awamu ya kwanza na imeshachakata na kutoa daftari la awali na imeshakamilisha uboreshaji wa awamu ya pili mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili. Tunategemea kuanzia tarehe 28 mwezi huu (tarehe 28 Juni, 2025) tutaanza mzunguko wa tatu wa uboreshaji katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar na Magereza Tanzania Bara kwa wanafunzi na wafungwa waliohukumiwa kifungo chini ya miezi sita,” amesema Kailima.
 
Katibu huyo wa Baraza amesema mzunguko huo wa tatu utahusisha vituo 140 vya kuandikisha wapiga kura ambapo 130 vipo kwenye magereza Tanzania Bara na vituo 10 vipo kwenye vyuo vya mafunzo Tanzania Zanzibar. Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku saba hadi tarehe 04 Julai, 2025.
 
Ameongeza kuwa Tume imekamilisha maandalizi ya nyaraka mbalimbli kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja na Kanuni za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025, Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025 na maelekezo mbalimbali kwa ajili ya watendaji wa uchaguzi na wadau wa uchaguzi kupata miongozo kwa ajili ya utekelezaji wa uchaguzi.
 
Alimkumbusha mgeni rasmi kuwa tayari Tume imekamilisha zoezi la ugawaji wa majimbo na kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutakuwa na jumla ya majimbo 272 yatakayofanya uchaguzi wa wabunge katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kata 3960 kwa ajili ya uchaguzi wa madiwani kwa Tanzania Bara.