TAASISi 762 ZATUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA NCHINI-DKT.MPANGO

June 07, 2025 Add Comment


📌 Taasisi chini ya Wizara ya Nishati zqpewa tuzo kutambua mchango wao katika Gesi, Umeme na Nishati Jadidifu


Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Philip Isdor  Mpango ameeleza kuwa jumla ya taasisi 762 nchini zinatumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni jitihada za kuepuka athari za kimazingira, kiafya, kijamii na kiuchumi.


Amesema hayo tarehe 5 Juni 2025 katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani ambayo  kitaifa imeadhimishwa jijini Dodoma katika kituo cha  Mikutano cha Jakaya Kikwete.


 "Taasisi nyingi za Serikali na Binafsi zimeanza kutekeleza katazo la matumizi ya nishati isiyo safi na  kuanza kutumia nishati safi ya kupikia ambapo  hadi Machi 2025 jumla ya Taasisi 762 zilikuwa zimeanza kutumia nishati safi ya kupikia." Amesema Dkt. Mpango


Ameongeza kuwa,  kati ya taaisis hizo, taaisisi za Umma ni 495 na taasisi binafsi ni 267.i 


 Makamu wa Rais amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kuendeleza na kusukuma matumizi ya nishati safi ya kupikia Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla.

Sambamba na hilo Dkt. Mpango amezipongeza taasisi zote zilizotekeleza katazo hilo la kutotumia nishati isiyo safi  na kutoa rai kwa taasisi ambazo hazijatekeleza agizo hilo ziendelee kuwekeza katika matumizi ya nishati safi ya kupikia. 


Katika hafla hiyo ya Siku ya Mazingira dunian,   Dkt. Mpango ametoa Tuzo kwa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ikiwa upande wa REA tuzo imepokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bw. Renatus Msangira tuzo ya kutambua mchango wa REA katika kutunza mazingira  kupitia utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia.

Miradi hiyo ambayo ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ni pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi pamoja na majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia vijijini .


Aidha, TANESCO tuzo hiyo imepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange,ikiwa ni kutambua mchango wa TANESCO katika kuhifadhi mazingira kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ambao umeendelea kuzingatia misingi ya utunzaji wa mazingira sambamba na kuchangia kupunguza gesi joto.

Huku, CPA Mussa M. Makame - Mkurugenzi Mtendaji TPDC, amepokea TUZO  ya kutambua mchango wa TPDC katika kuhifadhi  na kutunza mazingiza kupitia matumizi ya gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG).



DKT.BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO KIKUBWA CHA GESI AFRIKA MASHARIKI

June 05, 2025 Add Comment


📌 *Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini*


📌 *Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa*


📌*Kampeni ya Rais Samia ya Nishati Safi ya Kupikia  Yavutia Wawekezaji*


📌*Matumizi ya Gesi ya Kupikia Yaongezeka Kila Mwaka*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa wawekezaji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa Watanzania ili kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.


Amewaomba wawekezaji wa mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy licha ya kuwa zitazalishwa ajira zaidi ya 300 na baadae zaidi ya 2,000, waangalie utaratibu katika ujenzi wa mradi huo ambao utawezesha wazawa kupata kazi na hakuna sababu ya kutafuta watu kutoka mbali.


Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Juni 5, 2025 jijini Tanga wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy mkoani humo.


“ Mradi huu uwe mfano wa kielelezo kila kazi anayoweza kufanya Mtanzania apewe, ili asilimia 40 ya fedha za ujenzi wa mradi zizunguke nchini. Nitasikitika nikiona kila aina ya kazi analetwa mtu kutoka nje kuja kufanya,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kutoa wito kwa wawekezaji kufikiria namna ya kupeleka huduma ya ujazaji mitungi ya gesi katika maeneo ya vijijini ikiwa ni pamoja na kuanzisha teknolojia ya kusaidia mtu aweze kulipia gesi kulingana na mahitaji yake badala ya kujaza mtungi mzima.


Dkt. Biteko amesema kwa mujibu wa taarifa ya utendaji sekta ndogo ya mafuta ya EWURA ya mwaka 2024, matumizi ya gesi ya kupikia yaani (LPG) huongezeka kwa kasi kila mwaka. Ambapo kwa mwaka 2023/24 matumizi yalifikia zaidi ya tani 403,000 ikilinganishwa na tani 293,000 mwaka wa fedha 2022/23 sawa na ongezeko la asilimia 38.


Amewahakikishia Kampuni ya Tanga Energy International Ltd kuwa mradi wao utakuwa na uhakika wa soko ndani na nje ya nchi na kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao  ili kufikia malengo yao ya kuleta huduma bora na nafuu kwa Watanzania.

Katika kuthibitisha hilo, Dkt. Biteko amesema kupitia Wakala wa Nishati Vijijini, Serikali inaendelea na programu ya kutoa ruzuku ili wananchi wapate mitungi ya gesi ya kupikia kwa punguzo la bei hadi kufikia asilimia 50 na kusambaza mitungi 452,445 ambapo hadi kufikia Aprili, 2025 jumla ya mitungi 154,225 imeshasambazwa.


“ Tarehe 2 Juni, 2025 pale jijini Dodoma tumezindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia. Hivyo, kupitia Mkakati huu, Serikali itaendelea kutoa elimu nchi nzima na hivyo kuinua uelewa wa wananchi na hatimaye kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo LPG ni chanzo kikuu,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Rais Samia anataka Mkoa wa Tanga uwe kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, na hivyo ameendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kutimiza lengo hilo ikiwemo kupanua mfumo wa kusafirisha umeme kutoka Majani mapana hadi Pemba kutoka kilovoti 33 hadi 132.


Pamoja na hayo ametoa wito kwa Watanzania kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kuchagua viongozi wanaofaa “ Tumuunge mkono Rais Samia kwa kuwa kinara wa Kampeni ya Nishati Safi kimataifa ili Watanzania wengi watumie nishati safi ya kupikia,” amemaliza Dkt. Biteko.


Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amesema kuwa utendaji kazi wa Dkt. Biteko umesaidia kuimarika kwa sekta ya nishati huku akisisitiza kuwa kukamilika kwa mradi huo mkubwa wa Kituo cha Gesi kutaifanya Tanzania kuwa msafirishaji mkubwa wa gesi  na kuchochea ukuaji wa viwanda nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burian amesema mradi huo utasaidia kuitangaza Tanga kimataifa, kuongeza ajira na pato la mkoa na Taifa kwa ujumla.

Akitoa salamu za Chama cha Gesi na Mafuta, Mkurugenzi Mtendaji wa TOAG, Abdulsamad Abdulrahim amesema mradi huo utaisaidia Tanzania kuleta mapinduzi ya nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki, kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi.


Bw. Abdulrahim amebainisha kuwa Watanzania wako tayari na hiyo ni fursa kwa wawekezaji wazawa kuonesha uwezo wao na wako tayari kufanya kazi.


“Tunaishukuru Serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kusaidia utekelezaji wa miradi kama hii ambayo ni zao la ushirikiano wa wageni na wazawa wenye kufanya mawazo kuwa uhalisia,” amesema Abdulrahim.


Awali akitoa maelezo ya mradi, Michael Dimond amesema LPG ni suluhu ya nishati safi ya kupikia na kuwa Kampuni ya Pretedec imefurahishwa jitihada za Rais Samia katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na lengo la Serikali la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


“Leo tunajivunia kuwekwa kwa jiwe la msingi katika mradi huu wa kipekee Tanzania ambao umezingatia usalama wa usambazaji wa LPG katika ukanda wa Afrika Mashariki,” amesema Dimond.


Mwakilishi wa Kampuni ya Asas, Bw. Ahmed Asas amesema mbali na manufaa ya kiafya na mazingira mradi huo utachochea uchumi jumuishi na kuchangia katika ukuaji wa viwanda vya ndani.


Mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy unatekelezwa kwa ushirikiano wa Kampuni ya Pretedec na Asas ambao unatagharimu dola za marekani milioni 100 utakuwa mradi mkubwa wa LPG nchini. Aidha, kupitia mradi huo unaotarajiwa kukamilika 2027 utanufaisha pia nchi za Burundi, Kenya, Uganda, Burundi na Zambia kwa kuagiza gesi kutoka nchini Tanzania.


Mwisho

DKT.BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO CHA GESI AFRIKA MASHARIKI

June 05, 2025 Add Comment


📌 *Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini*


📌 *Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa*


📌*Kampeni ya Rais Samia ya Nishati Safi ya Kupikia  Yavutia Wawekezaji*


📌*Matumizi ya Gesi ya Kupikia Yaongezeka Kila Mwaka*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa wawekezaji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa Watanzania ili kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.



Amewaomba wawekezaji wa mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy licha ya kuwa zitazalishwa ajira zaidi ya 300 na baadae zaidi ya 2,000, waangalie utaratibu katika ujenzi wa mradi huo ambao utawezesha wazawa kupata kazi na hakuna sababu ya kutafuta watu kutoka mbali.


Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Juni 5, 2025 jijini Tanga wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy mkoani humo.

“ Mradi huu uwe mfano wa kielelezo kila kazi anayoweza kufanya Mtanzania apewe, ili asilimia 40 ya fedha za ujenzi wa mradi zizunguke nchini. Nitasikitika nikiona kila aina ya kazi analetwa mtu kutoka nje kuja kufanya,” amesema Dkt. Biteko.


Ameendelea kutoa wito kwa wawekezaji kufikiria namna ya kupeleka huduma ya ujazaji mitungi ya gesi katika maeneo ya vijijini ikiwa ni pamoja na kuanzisha teknolojia ya kusaidia mtu aweze kulipia gesi kulingana na mahitaji yake badala ya kujaza mtungi mzima.


Dkt. Biteko amesema kwa mujibu wa taarifa ya utendaji sekta ndogo ya mafuta ya EWURA ya mwaka 2024, matumizi ya gesi ya kupikia yaani (LPG) huongezeka kwa kasi kila mwaka. Ambapo kwa mwaka 2023/24 matumizi yalifikia zaidi ya tani 403,000 ikilinganishwa na tani 293,000 mwaka wa fedha 2022/23 sawa na ongezeko la asilimia 38.

Amewahakikishia Kampuni ya Tanga Energy International Ltd kuwa mradi wao utakuwa na uhakika wa soko ndani na nje ya nchi na kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao  ili kufikia malengo yao ya kuleta huduma bora na nafuu kwa Watanzania.


Katika kuthibitisha hilo, Dkt. Biteko amesema kupitia Wakala wa Nishati Vijijini, Serikali inaendelea na programu ya kutoa ruzuku ili wananchi wapate mitungi ya gesi ya kupikia kwa punguzo la bei hadi kufikia asilimia 50 na kusambaza mitungi 452,445 ambapo hadi kufikia Aprili, 2025 jumla ya mitungi 154,225 imeshasambazwa.

“ Tarehe 2 Juni, 2025 pale jijini Dodoma tumezindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia. Hivyo, kupitia Mkakati huu, Serikali itaendelea kutoa elimu nchi nzima na hivyo kuinua uelewa wa wananchi na hatimaye kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo LPG ni chanzo kikuu,” amesisitiza Dkt. Biteko.


Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Rais Samia anataka Mkoa wa Tanga uwe kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, na hivyo ameendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kutimiza lengo hilo ikiwemo kupanua mfumo wa kusafirisha umeme kutoka Majani mapana hadi Pemba kutoka kilovoti 33 hadi 132.


Pamoja na hayo ametoa wito kwa Watanzania kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kuchagua viongozi wanaofaa “ Tumuunge mkono Rais Samia kwa kuwa kinara wa Kampeni ya Nishati Safi kimataifa ili Watanzania wengi watumie nishati safi ya kupikia,” amemaliza Dkt. Biteko.


Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amesema kuwa utendaji kazi wa Dkt. Biteko umesaidia kuimarika kwa sekta ya nishati huku akisisitiza kuwa kukamilika kwa mradi huo mkubwa wa Kituo cha Gesi kutaifanya Tanzania kuwa msafirishaji mkubwa wa gesi  na kuchochea ukuaji wa viwanda nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burian amesema mradi huo utasaidia kuitangaza Tanga kimataifa, kuongeza ajira na pato la mkoa na Taifa kwa ujumla.


Akitoa salamu za Chama cha Gesi na Mafuta, Mkurugenzi Mtendaji wa TOAG, Abdulsamad Abdulrahim amesema mradi huo utaisaidia Tanzania kuleta mapinduzi ya nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki, kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi.


Bw. Abdulrahim amebainisha kuwa Watanzania wako tayari na hiyo ni fursa kwa wawekezaji wazawa kuonesha uwezo wao na wako tayari kufanya kazi.


“Tunaishukuru Serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kusaidia utekelezaji wa miradi kama hii ambayo ni zao la ushirikiano wa wageni na wazawa wenye kufanya mawazo kuwa uhalisia,” amesema Abdulrahim.


Awali akitoa maelezo ya mradi, Michael Dimond amesema LPG ni suluhu ya nishati safi ya kupikia na kuwa Kampuni ya Pretedec imefurahishwa jitihada za Rais Samia katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na lengo la Serikali la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


“Leo tunajivunia kuwekwa kwa jiwe la msingi katika mradi huu wa kipekee Tanzania ambao umezingatia usalama wa usambazaji wa LPG katika ukanda wa Afrika Mashariki,” amesema Dimond.


Mwakilishi wa Kampuni ya Asas, Bw. Ahmed Asas amesema mbali na manufaa ya kiafya na mazingira mradi huo utachochea uchumi jumuishi na kuchangia katika ukuaji wa viwanda vya ndani.


Mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy unatekelezwa kwa ushirikiano wa Kampuni ya Pretedec na Asas ambao unatagharimu dola za marekani milioni 100 utakuwa mradi mkubwa wa LPG nchini. Aidha, kupitia mradi huo unaotarajiwa kukamilika 2027 utanufaisha pia nchi za Burundi, Kenya, Uganda, Burundi na Zambia kwa kuagiza gesi kutoka nchini Tanzania.


Mwisho

JAB YAANZA KUGAWA PRESS CARD KWA WAANDISHI WA HABARI

June 05, 2025 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Zikiwa zimesalia siku 17 kwa Waandishi wa Habari Kujisajili katika Mfumo wa TAI-HABARI ili kuomba Ithibati na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card), tayari waliokidhi vigenzo vilivyoanishwa Kisheria wameanza kupewa Vitambulisho hivyo.

Waandishi wa Habari wa kwanza kufika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri Jijini Dar es Salaam kuchukua vitambulisho vyao ni David Mayunga, Erasto Vedasto na Fredrick Mwantandi wote kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Wengine waliokabidhiwa vitambulisho vyao ni Mhariri wa gazeti la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar- Zanzibaleo Mwanajuma Hassan na Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Goshen Tanzania-goshenonlinetv Isaya Momba.
Mfumo huo uliofunguliwa rasmi Mei 19 mwaka huu, unatoa fursa kwa Wahariri, Waandishi wa Habari, Wapiga Picha, Watangazaji wa Radio na Televisheni, Waandishi wa Kujitegemea na Waandaaji wa Vipindi, waliokidhi vigezo vya Kitaaluma kujisali na kujaza taarifa zao kupitia kiunganishi cha https://taihabari.jab.go.tz ili kuomba Ithibati na Kitambulisho ambapo mwisho wa kujisajili ni Juni 21 mwaka huu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Wakili Patrick Kipangula amewapongeza waandishi hao na kutoa wito kwa waandishi wengine kuutumia vema muda uliotolewa.