WAZIRI MKENDA AVALIA NJUGA SAKATA LA MADEREVA KWENDA QATAR

May 28, 2025 Add Comment
Watu wanaowapeleka madereva kufanya kazi nje ya nchi wanawajibu wa kufanya utafiti kujua mahitaji ya eneo wanaloenda ni yapi tofauti na mahitaji ya magari ya Tanzania.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Profesa Adolf Mkenda amesema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Wizara hiyo katika miaka minne ya serikali ya awamu ya sita.

Waziri Mkenda amesema wahitaji hao wa madereva wanatakiwa kujua aina ya magari yaliyopo Tanzania ni ya namna gani, yanayoenda Kongo ni ya namna gani, madereva wa Tanzania wanajifunza nini, hivyo mtu akiwachukua watu nchini na kuwapeleka Qatar ni vizuri kwanza akaangalie, asiwachukue na kuwakimbiza kule halafu wakaenda kupimwa hilo ni jambo la muhimu kulifanya.

“Lakini pia tuna haja ya kuwafundisha magari yote hata yale ambayo hayajaingia nchini lakini sisi tulishatoa maelekezo miaka miwili iliyopita kwamba Chuo cha Ufundi Arusha kiingie makubalianao na makampuni ya magari na tayari wameanza mazungumzo na wengine wanaingia mkataba lakini pia tulishawaambia VETA kufanya jambo hilo” Amekaririwa Prof Mkenda

Hata hivyo amesema hata kwenye magari wanahitaji siyo fundi Mechanical pekee bali wanahitaji fundi ambaye anajihusisha na shughuli zote za mfumo wa magari ya kisasa (Mechatronics).






KAFULILA ATETEA REKODI YA RAIS DKT.SAMIA SULUHU KATIKA UBIA WA SEKTA BINAFSI NA UMMA

May 27, 2025 Add Comment


Na Ashrack Miraji Tanga Raha 


Dar es Salaam, Mei 27, 2025 — Kongamano muhimu kuhusu Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi limefanyika leo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, likikutanisha wadau mbalimbali wa maendeleo, viongozi wa serikali, sekta binafsi na wasomi mashuhuri. Kongamano hili limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya PPPC na REDET kwa lengo la kuimarisha mjadala kuhusu mchango wa ubia katika maendeleo ya taifa.


Miongoni mwa wageni waalikwa walioshiriki ni pamoja na Prof. Rwekaza Mukandala, Prof. Abel Kinyondo na Prof. Anna Tibaijuka, ambao waliwasilisha mada mbalimbali zinazohusu mchango wa sera, tafiti na uzoefu wa nchi nyingine katika kukuza ubia wenye tija. Washiriki walijadili umuhimu wa kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), David Kafulila, alitumia jukwaa hilo kutetea kwa nguvu rekodi ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kukuza ushirikiano wa sekta hizi mbili. Alisema kuwa tangu kuingia madarakani kwa Rais Samia, kumekuwa na mageuzi makubwa yanayolenga kuwezesha sekta binafsi kushiriki katika miradi ya kimkakati ya maendeleo.

David Kafulila alifafanua kuwa serikali haitegemei tena kodi na mikopo pekee kugharamia maendeleo, bali sasa inachochea ubia na sekta binafsi kama chanzo mbadala cha mitaji. Alieleza kuwa hadi kufikia Machi 2025, Tanzania ilikuwa na miradi 83 ya ubia yenye thamani ya zaidi ya Sh trilioni 30, hatua inayodhihirisha dhamira ya serikali katika kuchochea uchumi shirikishi.

Akigusia deni la taifa, Kafulila alisema kuwa ni himilivu na linatumika kwa uwekezaji wa maendeleo. “Deni la taifa la Sh trilioni 97 si tatizo ikiwa linachochea maendeleo. Tunapaswa kuelekeza nguvu katika usimamizi bora wa mikataba ya PPP badala ya kuogopa ubia,” alisisitiza.


Aidha, mchango wa sekta binafsi hauishii kwenye uwekezaji tu bali una nafasi kubwa katika kuongeza ajira kwa Watanzania na kukuza ujuzi wa kitaalamu. Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya asilimia 70 ya ajira nchini hutolewa na sekta binafsi, jambo linalosaidia kupunguza ukosefu wa ajira na kukuza kipato cha wananchi. Kupitia ajira hizi, wananchi huweza kuchangia zaidi kwenye mzunguko wa uchumi kwa njia ya matumizi, kodi na uwekezaji wa ndani.

Vilevile, sekta binafsi huchochea ubunifu na ushindani wa kibiashara, jambo linalosaidia kuboresha ubora wa bidhaa na huduma. Ushindani huu huongeza tija na kuwafanya wawekezaji kuboresha miundombinu, kuongeza matumizi ya teknolojia na kutoa mafunzo kwa wafanyakazi. Mchango huu unaiwezesha serikali kuelekeza rasilimali zaidi kwenye huduma za kijamii huku pato la taifa likiendelea kukua.


Kwa upande wake, Prof. Abel Kinyondo alitoa tahadhari kuhusu changamoto za usimamizi na ukosefu wa uelewa wa kina kuhusu PPP, akiitaka serikali kuweka mfumo madhubuti wa kuwajengea uwezo watendaji wa umma. Naye Prof. Tibaijuka aliitaka serikali kushirikisha wananchi kwa uwazi zaidi ili kuongeza uaminifu wa umma katika miradi ya ubia.

Kongamano hilo lilihitimishwa kwa mapendekezo ya kuimarisha ushirikiano wa sekta hizi mbili kupitia maboresho ya sera, uwazi katika mikataba na ushirikiano wa karibu na taasisi za elimu na utafiti. Washiriki walisisitiza kuwa ubia wa sekta binafsi na umma ni nyenzo muhimu ya kuifikisha Tanzania katika maendeleo jumuishi na endelevu ifikapo mwaka 2050.

DKT.BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA PUMA DUNIANI

May 27, 2025 Add Comment


📌 Tanzania na PUMA kuimarisha ushirikiano


📌 PUMA kuendelea kuwekeza zaidi Tanzania


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Duniani Bw. Mark Russell.


Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Mei 27, 2025 jijini Dodoma, Dkt. Biteko ameipongeza Kampuni ya PUMA Energies kwa kuwekeza nchini na kutoa huduma ya viwango vya juu katika bidhaa zake pamoja na kuzingatia wazawa katika nafasi za juu za utendaji za Kampuni hiyo nchini. 


Vilevile, ametoa rai kwa PUMA Energies kuendelea kuwekeza zaidi nchini na kusema kuwa Kampuni hiyo inaweza kujenga vituo zaidi vya kuweka gesi kwenye magari ili kusaidia upatikanaji wa huduma kwa wananchi. 

Kuhusu nishati safi ya kupikia, Dkt. Biteko ametoa wito kwa Kampuni ya PUMA kuwekeza katika eneo hilo na kusema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano wake kwa Kampuni hiyo.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Bw. Mark Russell amesema kuwa Kampuni yake imewekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 24 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vitatu vya kujaza gesi kwenye magari katika mikoa ya Dar es salaam na kimoja Dodoma.


MWISHO.

VERTEX YAJA NA UWEKEZAJI KIGANJANI

May 27, 2025 Add Comment



NA MWANDISHI WETU

MTENDAJI Mkuu wa Vertex International Securities limited Mateja Mgeta amewataka watu kuwekeza kupitia huduma ya Vertex Mobile Trading App ambayo itawasaidia wananchi kufanya uwekezaji kwa wepesi kwa kuwa ni moja ya njia nyepesi kwa watumiaji.

Mateja amebainisha hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Vertex Mobile Trading App yenye lengo la kuwapa wepesi wawekezaji kupitia simu janja zao.

Amesema lengo la ujio wa app hiyo una sura mbili ambazo ni kuwapa watu maarifa ya uwekezaji kwa urahisi iwe mtu anahitaji kuwekeza hisa katika makampuni yaliyoorodheshwa na soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) hivyo imani ni kubwa kuwa elimu ndio funguo ya ushiriki wa uwajibikaji.

Sababu ya pili iliyowasukuma kuanzisha Vertex Mobile Trading App kulenga kurahisisha mfumo wa uwekezaji kuufanya uwe wazi, rahisi na salama kwa watumiaji ambao mwekezaji au mwekezaji mtarajiwa anayetumia simu janja (smart phone) anaweza kufungua akaunti ya hisa, kununua au kuuza hisa kupitia kiganjani pasipokuwa na ulazima wa kufika ofisni kwao.

"Masoko ya mitaji yana jukumu muhimu sana katika kukusanya fedha kwa ajili ya matumizi yenye tija yanayotumika kama njia ambazo akiba inaweza kuelekezwa kwenywe miradi inayochochea ukuaji wa uchumi, ubunifu na kutengeneza ajira,"amesema Mateja.

Aidha Mateja amesema uwekezaji uchangia kikamilifu katika ajenda ya uchumi wa Taifa, hivyo kutokana na uwekezaji unaweza kuimalisha masoko ya mitaji ya ndani, kupunguza utegemezi wa ufadhili kutoka nje na kukuza uwekezaji utakaochochea ustawi wa pamoja.

Mateja ametoa pongezi kwa mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Tanzania (CMSA) chini ya Mtendaji wake Mkuu CPA Nicodemus Mkama kwa kuweka mazingira wezeshi katika soko kwani bila miongozo yao wasingeweza kufika walipo sasa.

Pia alitoa pongezi kwa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Peter Nalitolela kwa mchango wao mkubwa kuhakikisha Vertex Mobile Trading App mafanikio ya hisa kiganjani ambayo yamefanywa na wao Vertex International Securities limited.

Kwa upande wa mwakilishi kutoka CMSA Alfred Mkombo amesema wao mamlaka ya msoko ya mitaji wanafurahi kuona maendeleo kama haya ambayo yanawapa watu urahisi wa kuwekeza kupitia simu zao viganjani.

"Simu imekuwa kitu kikubwa zipo hadi vijijini mtu anaweza kushiriki minada inayotokea Dar es Salaam bila kusafiri na kutumia gharama kubwa, Vertex Mobile App imetengenezwa ili kuleta mageuzi na ni tekinolojia ambayo inatumika kwa wepesi bila hata kutumia nguvu,"

"Tunapenda kuona teknolojia hizi zinaleta tija zaidi tunawapongeza sana Vertex kwa namna ya kipekee kufikia hatua hii kubwa sana ya mafanikio ambayo inaakisi sera na sheria usimamizi unaoleta mazingira bora,"amesema Mkombo.

Huku Ali Othman kutoka DSE amesema jambo lililofanywa na Vertex ni kubwa na litaleta mafanikio makubwa kwa kuwa ni njia nzuri na rahisi kwa watu kutumia.

"App ina kila kitu kwa mtumiaji wa mtandao wowote Vertex Mobile Trading App imewarahisishia hii ni hatua nzuri inaongeza ushindani na ubunifu mpya kwa watu wote kuwekeza iwe mjini na hata vijini,"amesema Othman.









SERIKALI YAITAKA COMMUNITY NETWORK KUSAMBAZA TEHAMA VIJIJINI

May 27, 2025 Add Comment
Serikali kupitia Tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeitaka Taasisi ya School of Community Network kuongeza juhudi za kuanzisha vituo vya mafunzo ya TEHAMA katika mikoa mbalimbali nchini, hususan vijijini, ili kuwajengea vijana ujuzi wa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidigitali.