Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

MBUNGE NEEMA LUGANGIRA-AKILI MNEMBA INA TIJA NA FURSA NYINGI IKITUMIKA IPASAVYO

May 11, 2025 Add Comment

Na Mwandishi Wetu,DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalumu Kupitia Kundi la Asasi za Kiraia Tanzania (NGOs) Neema Lugangira amesema kwamba akili mnemba (artificial intelligence - AI) ina tija na fursa nyingi katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya,Kilimo na Elimu na nyenginezo hapa nchini.

Aliyasema hayo wakati akizungumza katika Semina ya Akili Mnemba kwa Wabunge Wanawake iliyoandaliwa kwa Ushirikiano na Shirika ambalo alilianzisha la Omuka Hub pamoja na Bunge la Tanzania kupitia Mradi wa Female Al Leaders chini ya Women Political Leaders (WPL) na GIZ unaolenga kuimarisha Utawala Bora wa Akili Mnemba “Artificial Intelligence #Al” kwa kuimarisha Wanawake Wanasiasa barani Afrika ili waweze kuibeba ajenda hiyo na kuwa Vinara.

Alisema katika Semina hiyo wamejadiliana mambo mengi na imeonyesha akili mnemba inafursa nyingi lakini alitoa angalizo pia isipotumika kwa usahihi ina changamoto ikiwemo ukatili wa kijinsia, kurubuni watoto na inaweza kupelekea kufifisha uwezo wa kufikiria kutokana na kutufanya sisi kuwa tegemezi sana.

“Katika semina hii, akili mnemba imetushangaza sisi kama Wabunge sababu niliamua kufanya jaribio la kuiuliza hii AI swali kuwa mimi ni Mbunge na naelekea kwenye uchaguzi, naomba inisaidie kuniandalia mkakati wa kampeni na baada ya dakika chache AI ikanipa mkakati kabambe kwa usahihi hadi mwenyewe unashangaa na inakuwa na uwezo wa muda mfupi wa kupima kila kilicho kwenye mitaandao yote yenye uwezo nayo inakupa picha pana”, Alisema Mbunge Neema Lugangira.

Alisema kwamba Akili Mnemba ni kitu ambacho kina tija lakini tija hiyo ili iweze kupatikana lazima itumike kwa ufasaha na wao kama Wabunge ni kitu ambacho wanakwenda kukiangazia; ni lazima kama Tanzania iwepo sera ya akili mnemba pamoja na sheria ili kama taifa linufaike na faida zake na pia kujikinga na kudhibiti na madhara yanayoweza kupatikana kwenye eneo hilo la akila memba.

Awali akizungumza Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (CCM) Jesca Msambatavangu alisema niwaondolee hofu akili mnemba haijaja kupora ajira za watu  bali imekuja kuboresha ajira na  kukuanzisha ajira na haijaja kumbagua mtu yoyote lakini lazima tutambue dunia ina mambo mazuri na mabaya hayo mambo wanatakiwa kujifunza mambo muhimu hivyo tunashukuru kuletewe semina hii ambavyo tunaamini itakuwa na tija”.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Fatma Toufiq alisema Bunge linatambua fursa na changamoto za akili mnemba hivyo Bunge wanajipanga kuandaa Sheria za Usimamizi.

Mbunge Fatma ambaye alimwakilisha Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson kwenye Semina hiyo ya Wabunge Wanawake kuhusu Akili Mnemba “Artificial Intelligence” ambapo alisema kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limefurahi kuwa sehemu ya kunufaika na mafunzo ya teknolojia ya akili mnemba.

Mhe Neema Lugangira (MB) ni mwakilishi Afrika wa Women Political Leaders (WPL)amefanikiwa kufanikisha mradi wa Female Al Leaders kuja hapa Tanzania ambapo sehemu ya kwanza ilikuwa ni kuandaa Semina ya Wabunge Wanawake kwa kushirikiana na Shirika ambalo alilianzisha la Omuka Hub pamoja na Bunge la Tanzania.


MWISHO.

MCC LAILAH NGOZI MGENI KONGAMANO LA NASIMAMA NA MAMA LITAKALOFANYIKA JIJINI TANGA

May 09, 2025 Add Comment
Na Mwandishi WETU,TANGA.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Lailah Burhan Ngozi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano linalohusu Mchango wa Rais Samia Suluhu kwa mabinti na Wanawake wa Tanzania katika miaka minne ya uongozi wake litakalofanyika Mei 11 mwaka huu Jijini Tanga .

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi swa Regail Naivera Jijini Tanga Mei 11 ambayo ni siku ya Mama Duniani ambalo litaanza saa tatu hadi saa kumi jioni

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwanamke na Uongozi ambao wameandaa Kongamano hilo Shamira Mshangama alisema lengo ni kuonesha mchango wa Rais Dkt Samia Suluhu kwa mabinti na wanawake wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Alisema kwamba kongamano hilo limejikita katika kutambua jitihada zilizofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika Sekta ya Afya,Elimu,Uchumi na Uongozi.

Shamira alisema kwamba Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na mabinti na wanawake takribani 400 kutoka mkoa wa Tanga na mikoa ya Jirani .

CCM TANGA YASAJILI ZAIDI WANACHAMA 500,000 KIELETRONIKI KWA MUDA WA SIKU 10

April 24, 2025 Add Comment

Na Oscar Assenga, TANGA

CHAMA cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga (CCM) wamefanikiwa kusajili zaidi ya wanachama 550,000 kwa mkoa wa huo kwa mfumo wa kieletroniki kwa muda wa siku 10 wakiziita siku 10 za moto, katika zoezi hilo wamefanikiwa kuhakiki Taarifa za wanachama wao na sasa wako kwenye siku 10 za moto za kugawa kadi za kieletroniki kwa Wilaya za Mkoa huo baada ya usajili na uhakiki kukamilika.

Akizungumza na Mtandao huu,Katibu wa Siasa,Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Tanga Ndugu Samwel Kiondo Mngazija alisema kwamba wanaendelea na zoezi hilo katika Wilaya mbalimbali za mkoa huo huku usajili nao ukiwa unaendelea na kwa sasa kwenye mfumo wana wanachama zaidi ya 700,000 mpaka 800,000 ambao wamesajiliwa.

“Zoezi hili la uhakiki wa wanachama wetu tunalifanya kwa umakini mkubwa na weledi na tunazunguka Mkoa mzima kwa siku 10 za moto kugawa kadi za kieletroniki za CCM kwa wanachama wetu na tunaendelea na uhakiki wa Taarifa na usahihishaji wa taarifa za wanachama wetu na zoezi la usajili wanachama wapya linaendelea”Alisema



Aidha alisema kwamba awali kwenye mkoa wa Tanga walikuwa na zaidi ya wanachama 200,000 wanatarajia kufikiwa na mfumo wa kadi za kieletroniki ambao usajili ulianza 2018 na mwaka huu walihuisha zoezi kwa maana watu wengi walikuwa hawajaingia kwenye mfumo na usajili ulikuwa unaendelea.

“Kutokea mwaka huu tulikuwa na siku 10 za moto ambapo wilaya zote za Mkoa wa Tanga tumezifikia kwa Maelekezo ya Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa Dkt Samia Suluhu Hassan kuleta Vitendea Kazi kila kata kwa ajili ya kurahisisha usajili na kwenda na kasi kutokana na uhitaji wa kadi kwa wanachama wetu hivyo kupelekea zoezi la siku 10 za moto kuwa na tija kubwa pamoja na Usimamizi wa Jemedari wa Vita Ustadhi Rajab Abrahamani Abdallah Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa” Alisema  

Hata hivyo alisema kwamba kila siku wanachama wanajiunga nao kutokana na maendeleo makubwa yanayofanywa na Serikali inayoongozwa na CCM chini ya Daktari Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na wasaidizi wake. 

BALOZI NCHIMBI AFUNGA KAZI RUVUMA

April 07, 2025 Add Comment

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amehitimisha ziara yake ya siku tano mkoani Ruvuma, akisisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa chama cha wanachama, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote na kuwa mtetezi wa wanyonge.

Balozi Nchimbi amesema kwamba katika kuendeleza nafasi yake kama taasisi imara inayohusika na uongozi wa nchi, CCM hakina budi kuendeleza misingi ya sera zake zinazolenga kubadilisha hali za maisha ya watu, kuendana na mahitaji ya nyakati, na kuzingatia maslahi ya taifa.

Dkt. Nchimbi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wanaCCM na wananchi wa mji wa Songea, waliokusanyika kumpokea alipofika kufungua mradi wa kitega uchumi wa Tawi la CCM la Mshangano mjini Songea, Jumapili tarehe 6 Aprili 2025, ikiwa ni siku ya tano tangu alipoanza ziara hiyo tarehe 2 Aprili 2025.

Katika ziara hiyo aliyoanzia katika Wilaya ya Tunduru, Namtumbo, Nyasa, na hatimaye Songea mjini, Balozi Nchimbi alitoa pongezi kwa Serikali ya CCM, inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, kwa jinsi inavyotafsiri kwa vitendo na ufanisi, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, kupitia miradi ya maendeleo na huduma kwa wananchi.

Balozi Nchimbi alitoa maelekezo kwa Serikali kuendelea kusimamia na kubuni mipango inayolenga kuongeza matokeo chanya kwenye shughuli za uzalishaji mali, ikiwemo kilimo na madini, ili wakulima na wachimbaji madini waendelee kuzalisha kwa tija itakayoongeza pato la taifa na kuboresha maisha ya wananchi.


Aidha, Balozi Nchimbi alitembelea na kutoa maelekezo mahsusi katika miradi kadhaa ya maendeleo na ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali kupitia wizara na taasisi zake, ikiwemo mradi wa uzalishaji mbegu chini ya Mamlaka ya Mbegu Nchini (ASA) na ujenzi wa Bandari ya Nyasa, kwa lengo la kuendelea kutafsiri utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.


Katika mikutano ya hadhara katika wilaya mbalimbali, pamoja na kusalimia wananchi katika maeneo ya Songea Vijijini, Mbinga na Songea mjini, Balozi Nchimbi alipokea taarifa za utendaji wa kazi kutoka kwa viongozi wa Chama na Serikali, na pia alipokea maoni ya wananchi kuhusu changamoto zinazowakabili, kupitia kwa wabunge na wananchi moja kwa moja, kisha kutoa maelekezo ya kutatuliwa kwa kero hizo.


Balozi Nchimbi, ambaye amehitimisha rasmi ziara yake kwa kuondoka mkoani humo Jumatatu tarehe 7 Aprili 2025, alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wanaCCM na Watanzania wote kwa ujumla kwa ushirikiano wao na Serikali ya CCM katika kulinda tunu za taifa, ikiwemo amani na utulivu. Alitoa wito wa kuendeleza hali hiyo wakati nchi inapoelekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


#Ends

DKT.SAMIA AMETENDA MAAJABU SEKTA YA NISHATI MIAKA MINNE YA UONGOZI -DKT.BITEKO

March 24, 2025 Add Comment


📌 Mashine ya 9 yakabidhiwa, yakamilisha MW 2115 - JNHPP


📌 Aitaka Jumuiya ya Wazazi ieleze Watanzania mafanikio ya Serikali


📌 Asema kuongezeka kwa mahitaji ya umeme nchini kunachochea ukuaji wa viwanda


📌 Atoa wito kwa Watanzania kuzingatia matumizi bora ya umeme


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sekta ya nishati imepiga hatua kubwa nchini sambamba na kuzalisha umeme wa ziada dhidi ya mahitaji ya Watanzania.

Dkt. Biteko amesema hayo Machi 23, 2025 jijini Arusha wakati akitoa takwimu kuhusu  ongezeko la mahitaji  ya umeme nchini katika Kikao cha Baraza Kuu la Wazazi Taifa.


“ Rais Samia amefanya kazi kubwa katika sekta ya nishati nchini na hivi karibuni, tulikuwa nchini Barbados kueleza  mafanikio yetu katika sekta hii kwa kuwa Rais Samia amefanya jitihada kubwa sana katika ya nishati,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza “Ili uchumi wa nchi yoyote duniani upatikane lazima kuwe na sekta ya nishati. Aidha, katika sekta ya nishati ili viwanda viweze kuendelea umeme unaohitajika ni asilimia 40 na katika sekta ya madini umeme unaohitajika ni asilimia 30,” 


Dkt. Biteko amesema mwaka 2017 hadi 2018 mahitaji ya juu ya umeme nchini yalikuwa megawati 1045, mwaka 2018 hadi 2019 mahitaji ya juu ya umeme yalikuwa megawati 1,116 mwaka 2021 hadi 2022 megawati 1,340.7.

“ Mwaka 2022 hadi 2023 mahitaji ya juu yaliyoongezeka na kufikia  megawati 1,470 na mwaka 2024 hadi kufikia sasa mwaka 2025 ni megawati 1,908 ikiwa ni sawa na megawati 262, ongezeko la mahitaji ya namna hii haliwezi kutokea kama hakuna uwekezaji katika sekta ya nishati,” amesema Dkt. Biteko.


Aidha, Dkt. Biteko amesema kuwa Mashine ya tisa ya mtambo wa kuzalisha umeme katika Bwawa la Julius Nyerere Machi 22, 2025 imekabidhiwa na kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa. Amesisitiza kuwa kutokana na ongezeko hilo la megawati za umeme Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere pekee linaweza kutosheleza mahitaji ya nchi licha ya kumalizika kwa muda uzalishaji wa umeme kwa kutumia mitambo ya Songas.

 “Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sekta ya nishati imefanya kazi kubwa, Rais Samia ametenda maajabu katika sekta hii na ameweza kuvutia wawekezaji wengi sana kuja kuwekeza nchini,” amesema Dkt. Biteko.

Aidha, amesema kuwa Jumuiya ya Wazazi nchini ina wajibu wa malezi na mazingira na kuwa nishati safi ni eneo mojawapo hivyo Wizara ya Nishati ina wajibu wa kushirikiana  na wadau mbalimbali ikiwemo Jumuiya hiyo, sambamba na kushirikiana nayo katika kampeni zake za kupeleka ujumbe kwa jamii.

Pamoja na hayo, Dkt. Biteko amewaasa Watanzania kuzingatia matumizi bora ya umeme kwa kuacha mazoea yanayosababisha upotevu wa umeme ikiwemo kuwashaa taa bila kuwa na matumizi nazo.


Ametolea mfano kuhusu matumizi mabaya ya umeme kupitia utafiti uliofanywa na Wakala wa Nishati wa Kimataifa (International Energy Agency) ambapo asilimia 30 ya umeme unapotea kutokana na mazoea.


Katika hatua nyingine, taasisi mbalimbali ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) zimewasilisha mada mbalimbali katika semina hiyo.


Pia, Wizara ya Nishati kupitia taasisi zake za TPDC, REA na TANESCO zimetoa semina kwa wajumbe wa kikao hicho kuhusu Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024 hadi 2034, Matumizi Sahihi ya Nishati Safi ya Umeme.


Ambapo, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Ngeleja Mugejwa ameeleza faida mbalimbali za matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan kwa watoto wa kike ambapo  kupitia matumizi ya nishati hiyo itawasaidia kupata muda mwingi wa kujisomea kuliko kuandaa na kupika chakula.