Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts
WAZIRI NDUMBARO AIAGIZA BMT ISIMAMIE MICHEZO KUONGEZA PATO LA TAIFA

WAZIRI NDUMBARO AIAGIZA BMT ISIMAMIE MICHEZO KUONGEZA PATO LA TAIFA

October 17, 2023 Add Comment




NA Shamimu Nyaki

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amelielekeza Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kubuni vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitasaidia kuongeza Pato la Taifa kupitia Sekta ya Michezo.

Mhe. Ndumbaro amesema hayo wakati wa kikao na Baraza hilo kilichofanyika Oktoba 16, 2023 jijini Dar es salaam ambapo ameliagiza lisaidie Vyama na Mashirikisho ya Michezo kupata ushirikiano na Vyama wenza nje ya nchi hatua itakayoviwezesha vyama hivyo kubadilishana uzoefu katika Utawala na uendeshaji wa shughuli za Vyama hivyo.

“BMT pitieni muundo wa uendeshaji michezo kuanzia ngazi ya Mikoa hadi vijiji, michezo iwe ni biashara na ajira, ifike wakati Vilabu vijue idadi ya wanachama wao kwa kuzingatia jinsia ili iwasaidie kujua idadi ya waliyonayo na namna ya kuongeza wanachama wapya” amesema Mhe. Ndumbaro.

Dkt. Ndumbaro ametumia nafasi hiyo kuviasa Vyama na Mashirikisho viepuke migogoro ya mara kwa mara badala yake vizingatie Katiba zinazoongoza na kuzingatia Utawala Bora.

Awali, Katibu Mtendaji wa Barza hilo Bi. Neema Msitha amesema Baraza limeendelea kupata mafanikio mbalimbali kwa Timu za Taifa kupitia ufadhili wa Serikali chini ya Mfuko wa Maendeleo ya Michezo kufika mashindano ya Fainali ya Kombe la Dunia kwa Timu ya Wanawake chini ya Miaka 17 pamoja na Timu ya Walemavu.

Bi. Neema ameongeza kuwa kwa sasa Baraza hilo linatumia mfumo wa Kidigitali kusajili Vyama na Mashirikisho ambao umerahisisha gharama na muda wa kufanya Usajili.

SAFARI LAGER YAZINDUA KAMPENI YA KUSAKA VIPAJI VYA SOKA TANZANIA

SAFARI LAGER YAZINDUA KAMPENI YA KUSAKA VIPAJI VYA SOKA TANZANIA

September 19, 2023 Add Comment

 

Na Sophia Kingimali

Ili kuendelea kukuza vipaji vya vijana katika sekta ya mpira wa miguu kampuni ya bia ya safari imezindua kampeni ya kusaka vipaji nchi nzima lengo likiwa kuzalisha vipaji vipya nchini huku mshindi wa michuano hiyo kuibuka na kitita cha milion 44.

Akizungumza Leo septemba 19 jijini Dar es salaam wakati akizindundua kampeni hiyo meneja chapa ya Safari Lager Pamela Kikuli amesema mashindano hayo yatafanyika mikoa mbalimbali ambapo baada ya mashindano itaundwa timu itakayojulikana kama safari champions yaani mapigwa wapya katika mpira.

“Tumeamua Kuja na kampeni na kampeni hii ili kuibua vipaji vipya kabisa vya mpira wa miguu kwani tunaamini Kuna vipaji vingi nchini ambavyo avijaibuliwa”amesema Kikuli.


Amesema mashindano hayo yatafanyika katika mikoa minne ambayo ni Mbeya,Arusha,Mwanza na Dar es salaam huku mkoa wa Kwanza ukiwa mbeya ambapo mashindano hayo yatafanyika katika viwanja vya FFU Polisi octoba 7.

“Timu zile za mikoa zitatumika kuchagua vijana ambao wataunda timu moja kubwa ya wachezaji 22 ambao watacheza mechi ya kirafiki na timu mojawapo ya ligi kuu.”amesema

Ameongeza kuwa mchezaji mmoja kati ya Hao atapata fursa ya kuchaguliwa na mawakala wa ligi kuu Bara ili kuweza kuchezea timu kubwa baadae.

Amesema timu hiyo ya safari champions itakayocheza na timu ya ligi kuu itajinyakulia kitita cha million 44 kama kifuta jasho kwa ajili ya michuano hiyo.

“Hii michuano si midogo itakua na change changamoto nyingi hivyo tutawazawadia hao washindi kiasi hiko cha pesa ili kuendelea kuwapa motisha”ameongeza.

Kwa upande wake kocha Jamuhuri Kihwelo ambae ndio ataendesha mchakato kwa kushirikiana na Sekilojo Chambua amesema mchakato huo utakua wa wazi na wala hautakua na upendeleo wowote hivyo vijana wajitokeze kwa wingi ili kushiriki mchuano hiyo.

Nae kocha Sekilojo Chambua amesema uwepo wa michuano hiyo ni mapinduzi katika sekta ya mpira Kwani itasaidia kuibua vipaji vipya ambavyo vitakua rasilimali kwa nchi.

“Tukiwa na wachezaji wetu wenye viwango hapa nchini wataweza kwenda kucheza hata soka la kulipwa nje na hii itakua ni heshima kwa taifa”amesema Chambua”   

RAIS DKT SAMIA APONGEZWA KWA JUHUDI ZA KUENDELEZA MICHEZO, WAIPA TANO TAIFA STARS

September 11, 2023 Add Comment

 Na Mwandishi Wetu, Tanga


WABUNGE wa Kamati ya Kudumu ya Elimu, Utamaduni na Michezo, wamempongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuendeleza michezo nchini, kulikosabisha Taifa Stars kufudhu mashindano ya Afrika Mwakani (AFCON) nchini Ivory Coast.

Akizungumza katika majumuisho ya jumla baada ya Kamati hiyo kutembelea Kituo cha mafunzo cha TFF Mnyanjani, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Husna Sekiboko matokeo hayo ya kufudhu yamechagizwa na jitihada anazofanya Rais kwa shirikisho hilo pamoja na vilabu.

Amesema Kamati hiyo itaendelea kumuunga mkono na kumsaidia katika sekta hiyo ili iweze kuleta matokeo chanya ambayo yataifanya timu ya Taifa 'Taifa Stars' ione kawaida kufudhu fainali hizo.

"Tunampongeza Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuchagiza katika michezo, matokeo haya ya kufudhu kwenda Ivory Coast Mwakani hayakuja hivi hivi ni ushirikiano wa Rais na wadau wengine wa michezo nchini, sisi Kamati yetu tutaendelea kumuunga mkono," amesema Husna.

Pia kamati hiyo imelipongeza Shirikisho hilo la michezo nchini kwa kufanya vizuri katika uwekezaji wa miradi ya vituo hivyo vilivyojengwa Tanga na Dar es Salaam ikiwemo kuwa na Ligi bora yenye ushindani katika bara la Africa.

"TFF mmefanya vizuri katika miradi ya vituo hivi, lakini pia katika michezo mna Ligi bora ambayo sasa mnakwenda kumaliza lile la Tanzania kuitwa 'Kichwa Cha Mwendawazimu.

" Kamati hiii itaendelea kushirikiana na TFF katika suala la viwanja katika kila wilaya ili maeneo yatakayotengwa yatumike kwa ajili ya michezo na si vinginevyo."

Awali Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho hilo, Oscar Mirambo amesema taarifa ya mkakati wa muda mrefu wa Tanzania ni kupata vijana wenye vipaji ambao watapata mafunzo katika vituo hivyo ambako kwa Dar es Salaam pale Kigamboni watawekwa wachezaji wa rika tofauti kwa Wanawake na Tanga Mnyanjani watakaa wavulana wa umri tofauti.

Wakichangia baada ya wasilisho hilo baadhi ya wabunge wa Kamati hiyo waliipongeza TFF kwa malengo hayo lakini wakawataka wahakikishe wanalinda maadili ya vijana watakaokuwa katika vituo hivyo ili wasijiingize katika vitendo viovu ikiwa ni pamoja na utumiaji wa madawa ya kulevya na ndoa za jinsia moja.

Mbunge wa Magomeni Visiwani Zanzibar, Mwanahamisi Ali Kassim, licha ya kumpongeza Rais kwa kutoa fedha kuzisaidia timu za Simba na Yanga kununua magoli waliyofunga katika mashindano ya vilabu msimu uliopita halikuwa jambo dogo.

"Tumpongeze Rais kile kidogo alichotoa kwa timu zetu tumuungeni mkono na zile fedha zitumike vizuri tusimuangushe," alisema mbunge huyo na kulitaka shirikisho lihakikishe linalinda nidhamu kwa vijana.

Yanga iliyofunga magoli 15 ilipokea kiasi cha shilingi milioni 115 huku Simba iliyofika robo fainali ya Ligi ya Mabigwa Afrika ilifunga magoli 11 na kupata fedha za Rais kiasi cha shilingi milioni 55 na kufanya jumla ya fedha zote za Rais kuwa shilingi milioni 190 kwa magoli 26 yaliyofungwa na timu hizo.

Kamati hiyo ilionesha wasiwasi wa fedha kiasi Cha shilingi bilioni 4.513 zilizotumika kujenga viwanja viwili vya mpira pamoja na jengo la hostel la orofa mbili, jengo la utawala na jengo la mafunzo.

Makamo wa Rais wa Shirikisho hilo, Athumani Nyamlani aliwatoa wasiwasi wajumbe wa Kamati hiyo kwa kuwaeleza kwamba fedha hizo zimetumika kwa viwango vya Kimataifa vilivyowekwa na FIFA ikiwa ni pamoja na kutafuta wakandarasi waliojenga.

Nyamlani alisema uwepo wa vituo hivyo, utaleta tofauti mkubwa katika soka la Tanzania na kwamba uwepo wake vituo hivyo pia vitatumika kufunza waamuzi, wachezaji na viongozi wa mpira katika bara la Afrika.

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA, ameiongeza Kamati hiyo na kueleza maagizo waliyotoa watayafanyia kazi ikiwemo Kituo Cha michezo cha Malya kilichopo jijini Mwanza kinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na Serikali.








CRDB yainyamazisha NMB tamasha la Simba Day

August 08, 2023 Add Comment
Wakati maelfu ya Watanzania kutoka kila pembe ya nchi wakiacha shughuli zao na kuelekea Lupaso kushuhudia ‘Wenye Nchi,’ Klabu ya Simba ikiukaribisha msimu mpya kwa tamasha lililofana, kikosi cha timu ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB jana kiling’ara kwenye tamasha la Simba Day baada ya kuwanyamazisha wapinzani wao, Benki ya NMB kwa ushindi wa bao 1-0.
 
Kwenye tamasha hilo ambalo Simba iliendeleza utamaduni wake wa kuujaza uwanja kwa mashabiki wenye ari kubwa ya kuishangilia, walipata burudani murua kutoka kwa maofisa wa benki hizo mbili kubwa zaidi nchini walioziacha suti zao na kutupia bukta na fulana na kukiwasha mbele ya wapenda soka 60,000 walioujaza Uwanja wa Taifa almaarufu kama Uwanja wa Benjamini Mkapa au Lupaso jijini Dar es Salaam. 
Akizungumza baada ya kupata ushindi huo, Kapteni wa Timu ya Benki ya CRDB, Nicodemus Milinga amesema ilikuwa ni lazima washinde kwani walijiandaa vilivyo.
 
“Kujituma na kufuata maelekezo ya kocha. Wote tulikuwa na ari ya juu ya kuipigania brand (nembo) kama vile tunavyotoa huduma bora kwa wateja wetu kila siku, ndani na nje ya nchi,” amesema Milinga.
 
Twaha Beimbaya, kocha aliyejifunzia Uingereza na akaja akachukua kombe la U17 na JKT Tanzania mwaka 2021 halafu akaisaidia Pan Africa isishuke daraja la kwanza mwaka jana anayeinoa timu ya Benki ya CRDB, anasema uzoefu walioupata kwa kushiriki michuano ya Sikukuu ya Mei Mosi walikomenyana na vikosi vigumu vya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  umewaongezea kujiamini wachezaji wake.
“Tulipotoka huko, niliwaomba wachezaji kuhakikisha wanapata muda wa kufanya mazoezi ndio maana walikuwa vizuri kwenye pambano hili lililoshuhudiwa na mashabiki wengi zaidi nchini,” amesema Beimbaya.
 
Bao hilo pekee katika msimu huu wa 15 wa Simba Day, liliwekwa kimiani na mshambuliaji makini Abdallah Magohe baada ya makosa ya kipa wa Benki ya NMB kuanzisha mpira kimakosa hivyo kuwapa Benki ya CRDB ushindi ulioshangiliwa na Mkurugenzi Mtendaji wake, Abdulmajid Nsekela.
 
Kipindi cha kwanza cha mchezo huo uliokuwa burudani tamu kwenye tamasha hilo kutokana na soka la kitabuni lililoonyeshwa na timu zote huku washindi wakifunika, kilimalizika bila milango ya timu hizo kufunguliwa.
 
Kocha wa timu ya Benki ya NMB, nyota wa zamani wa Yanga, Mohammed Hussein almaarufu kama Mmachinga alikiri kuzidiwa na wapinzani wao waliotumia nafasi waliyoipata kushinda mchezo huo.

--

DKT SIMEO: MICHEZO NI NGUZO MUHIMU YA UTULIVU NA USALAMA KWENYE NCHI

August 06, 2023 Add Comment
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akizungumza wakati alipozindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime

 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akizungumza wakati alipozindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime
Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Tanga Edgar Mdime akizungumza kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo
MKUU wa Idara ya Maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Sinde Mtobu akieleza umuhimu wa uchangiaji damu
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kulia ni Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime

Mwenyekiti wa Matawi ya Simba Mkoa wa Tanga Edgar Mdime akichangia damu



Na Oscar Assenga, TANGA.

MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Japhet Simeo leo amezindua zoezi la wanachama,wapenzi na mashabiki wa timu ya Simba kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora Jijini Tanga huku akieleza kwamba michezo ni moja ya nguzo muhimu katika utulivu na usalama kwenye nchi.

Simeo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba kwenye uzinduzi huo alisema kwamba michezo ina tija sana katika maisha ya binadamu ikiwemo kuwaunganisha jamii na kutengeneza undugu.

Alisema kwamba uchangiaji wa damu ni muhimu ili kuokoa maisha ya wagojwa wahitaji wa damu wakiwemo waluopata ajali, wakina mama wajawazito na watoto waliopo katika hospital mbalimbali mkoani Tanga.

Mganga Mkuu huyo aliwapongeza wanachama hao kwa utayari wao wa kuona umuhimu wa kuchangia damu ambayo itakwenda kusaidia jamii yenye uhitaji huku akizitaka Taasisi, Vikundi na watu binafsi kuendelea kuwa na utamaduni huo ili kuweza kuokoa maisha ya watu wanaofika hospital kupata huduma hiyo.

"Nawapongeza mashabiki wa timu ya Simba SC kwa utayari wenu kuja kuchangia damu mimi nawaambia hii ni sadaka na thawabu kubwa sana mliyoitoa kwa wenzenu wenye uhitaji wa damu " Alisema Simeo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Matawi ya Klabu ya Simba SC Edgar Mdime alisema kwamba zoezi la uchangiaji wa damu imekuwa ni utaratibu waliojiwekea kila mwaka lengo likiwa kuhakikisha wanakuwa sehemu ya kuokoa maisha ya wahitaji.

Alisema bado wanasukumwa kuchangia damu katika hospitali wakitambua kuwa uhitaji wa damu ni mkubwa kwa wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu hivyo licha ya kushiriki siku hiyo adhimu kwao bado wanaendelea kuhamasishana kujitoa kwa pamoja katika zoezi hilo.

Aidha alisema walianza na zoezi la usafi kubwa zaidi ilikuwa ni kuchangia damu na hamasa kubwa sana ambayo imetokea kwa mkoa huo kwa wana Simba na matawi yote wameungana kwa pamoja kwa ajili ya zoezi hili la kuchangia damu

Hata hivyo alisema kwamba wanajua damu ni muhimu sana kwa kila mmoja hasa ukizingatia wapo wakina mama wanaojifungua katika hospitali ikiwemo ajali zinatokea watu wanahitaji kuwekewa damu kwa hiyo wao wamehamasika kama wanajamii ukiachana na suala la michezo.

Tambo 

Mwenyekiti huyo alisema kwamba dhamira yao kubwa msimu huu lazima timu yao ichukue Ubingwa kutokana na uwepo wa kikosi kipana kulingana na usajili mkubwa uliofanyika wakiamini lazima timu hiyo ifanye makubwa katika mashindano ya ndani na hata kimataifa pia.

Katika hatua nyengine, Mdime alituma salamu kwa watani zao timu ya wananchi Yanga kuelekea mechi za Ngao ya jamii zitakazo chezwa Mkwakwani Tanga ambapo ametamba kwa kusema kuwa hawatakuwa tayari ngao hiyo aichukue tena mtani mbele yao.

Mchezo huo unatarajiwa kucheza Agosti 9 mwaka huu katika uwanja wa CCM Mkwakwani Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa Ngao ya jamii watakutana na matajiri wa Chamanzi Azam FC huku Simba SC wao wakiminyana na Singida Fountain Gate katika hatua ya nusu fainali timu zote zikitafuta nafasi ya kuanza vyema msimu 2023/2024 .