DC KOROGWE AIPA KONGOLE MUHIMBILI NA VODACOM TANZANIA FOUNDATION KWA HUDUMA ZA MATIBABU MKOANI TANGA
habariMkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilema amekoshwa na huduma za uchunguzi na matibabu ya ubingwa bobezi bure zinazotolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila kwa kushirikiana na Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation katika kambi inayofanyika viwanja vya Chuo cha Ualimu Korogwe mkoani Tanga.
Akizunguza katika kambi hiyo Mhe. Mwakilema amesema serikali inaendelea kufanya uwekezaji katika sekta ya afya kwa kutambua umuhimu wa sekta hiyo kwa wananchi na namna inavyoweza kuchochea Uchumi wa nchi kwa kuwa jamii yenye afya madhubuti itakuwa imara katika shughuli mbalimbali za uwekezaji
“Nawapongeza sana Muhimbili na Vodacom Foundation Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuboreshaji wa huduma za afya, wanaamini sana huduma za ubingwa bobezi zinazotolewa nanyi kutokana na historia na uwezo wenu wa muda mrefu hapa nchini ndio maana mnaona wamejitokeza kwa wingi” amebainisha mhe. Mwakilema.
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Watoto MNH. Dkt Aika Shoo amesema timu hiyo imejipanga kwa kuhakikisha kuwa wananchi wote wanaofika katika kambi hiyo wanapata huduma bora kwa wakati bila gharama yeyote na hivyo amewaomba waendelee kujitokeza kwa wingi.
Naye Meneja wa Eneo -Vodacom Korogwe Bw. Kaanankira Nanyaro amesma Vodacom Tanzania Foundation wataendelea kushirikiana bega kwa bega na Muhimbili katika kuhakiisha kuwa wananchi wanapatiwa huduma za afya kadri itakavyowezekena.
MNH na Vodacom Tanzania wameanza kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya ubingwa bobezi bila malipo kuanzia Julai 21 hadi 23, kwa wakazi wa Tanga ambapo baadaye huduma hizo zitahamia katika Mkoa wa Kiliamjaro kuanzia Julai 25 hadi 27, 2025
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ASHIRIKI KIKAO CHA KIMATAIFA CHA SHERIA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI
habariTANESCO YAANDIKA HISTORIA AJIRA MPYA
habari📍Waajiriwa wapya 555 wapata ajira kwa mara moja
📍Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO afungua rasmi mafunzo elekezi kwa waajiriwa hao
Na: Mwandishi Wetu, Dodoma
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeandika historia kwa kuajiri watumishi wapya 555 kwa mara moja, hayo yameelezwa katika uzinduzi wa mafunzo elekezi kwa waajiriwa hao, huku Mgeni rasmi akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Rhimo Nyansaho, jijini Dodoma.
Mafunzo hayo yamefunguliwa tarehe 21 Julai, 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, yakilenga kuwapa uelewa mpana kuhusu majukumu yao ndani ya Utumishi wa Umma na ndani ya Shirika, kabla ya kuanza kazi rasmi katika maeneo waliyopangiwa kote nchini.
Akifungua mafunzo hayo, Dkt. Nyansaho aliwataka watumishi hao wapya kutambua uzito wa fursa waliyoipata na kuitumikia kwa bidii, uadilifu, na uaminifu mkubwa.
“Kipekee namshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia kibali cha kuajiri. Hii ni fursa ya kipekee, na ni wajibu wenu kuithamini kwa kufanya kazi kwa juhudi na weledi mkubwa,” alisisitiza Dkt. Nyansaho.
Akiwaasa kuhusu mwenendo wao wa kikazi, aliwakumbusha kuwa TANESCO imepiga hatua kubwa katika utoaji wa huduma bora kwa wateja, hivyo wanapaswa kuendeleza juhudi hizo kwa kuwahudumia wateja kwa kuwajibika na kuwa na maadili ya hali ya juu.
“Tumepiga hatua kwenye utoaji wa huduma bora kwa wateja, hivyo ni muhimu muiendeleze kwa kuwahudumia wateja kwa uaminifu na uadilifu kwa maslahi mapana ya Shirika na Taifa kwa ujumla" alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, aliwataka waajiriwa hao kuwa mabalozi wa Shirika katika maeneo yao ya kazi kwa kutekeleza majukumu yao kwa bidii, uaminifu, na kwa kutoa huduma bora kwa wateja.
“Katika majukumu yenu, mnakwenda kukutana na wateja wetu. Wahudumieni kwa heshima na kwa moyo wa kujitolea, ili kwa pamoja tuendelee kujenga taswira chanya ya TANESCO,” alieleza Bw. Twange.
Waajiriwa hao wameajiriwa na TANESCO hivi karibuni baada ya kupitia mchakato wa ajira, huku awali wakiwa wafanyakazi wa mikataba ya muda na ajira hizi mpya zinawapa fursa ya kupata ajira za kudumu.
RAIS SAMIA ATOA BILIONI NNE UJENZI KIWANDA CHA KUZALISHA NISHATI MBADALA*
habari
📌Kiwanda kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati safi nchini
📌REA kugharamia ununuzi wa mtambo wa STAMICO
📌Stamico yapania kusambaza Nishati Safi ya Rafiki Briquettes kila kona
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na Shirika la Taifa la Madini (STAMICO) leo tarehe 22 Julai, 2025 wamesaini mkataba wenye lengo la kujenga kiwanda kipya cha kuzalisha nishati mbadala (Mkaa mbadala wa Rafiki Briquettes) mkoani Geita ambapo mkataba huo una thamani ya shilingi bilioni 4.5.
Katika hafla iliyofanyika katika Ofisi ndogo ya REA, Jijini, Dar es Salaam, REA itatoa jumla ya shilingi bilioni tatu na STAMICO itatoa shilingi bilioni 1.5; kwa mchanganuo huo, REA itagharamia ununuzi wa mtambo wakati STAMICO italipia upatikanaji wa kiwanja, ujenzi wa jengo la kiwanda na gharama za ufungaji wa mitambo.
Mkataba huo umesainiwa na Mhandisi, Hassan Saidy, Mkurugenzi Mkuu wa REA pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse.
Mkataba huo utaifanya STAMICO kuwa na viwanda vikubwa vitano vya kuzalisha mkaa mbadala wa Rafiki Briquettes; viwanda vingine ambavyo vinaendelea na uzalishaji wa mkaa mbadala vipo wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani, Kiwira mkoani Songwe, na viwanda vingine viwili vipo mkoani Dodoma na Tabora ambapo vipo kwenye hatua za mwisho za ukamilishwaji kabla kuanza uzalishaji.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mhandisi, Hassan Saidy, amesema kuwa Wakala umepewa jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia unafikia asilimia 80 kwa Watanzania wote ifikapo mwaka 2034.
“Katika kufanikisha lengo hilo, Wakala unatekeleza Miradi mbalimbali ikiwemo uwezeshaji katika kuongeza uzalishaji na usambazaji ili kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa Watu wa vijijini.”
“Utiaji wa saini wa Mkataba huo kati ya REA na STAMICO ni moja wapo ya utekelezaji wa maagizo ya Mheshiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Wakala ili kushirikiana na Shirika la Madini la Taifa kuona namna ya kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati safi kwa Wananchi ili waondokane na matumizi ya nishati zisizo safi na salama”. Amesema Mhandisi, Hassan Saidy, Mkurugenzi Mkuu REA.
“Ni matumaini yetu kuwa Mkataba huu utaende kuongeza kasi ya upatikaji wa mkaa mbadala na kwa bei nafuu ikiwa ni mojawapo ya lengo la Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia. Tunatambua kuwa utunzaji wa mtambo huu ni muhimu sana ili huduma iliyokusudiwa iendelee kutolewa kwa wakati bila kuathili uchumi wa Wananchi, afya na pamoja na mazingira kwa ujumla”. Amekaririwa, Mhandisi, Hassan Saidy.
Mhandisi, Saidy ameongeza kuwa Wakala unaendelea kushirikiana na Wadau mbalimbali ili kuhakikisha Mkakati wa Nishati safi ya kupikia unatimiza malengo yaliyowekwa, ikiwa ni pamoja na kuongeza upatikanaji na usambazaji wa mkaa mbadala, Wakala unaendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ikiwemo usambazi wa majiko banifu, usambazaji wa majiko ya umeme, usambazaji wa mitungi ya gesi ya kupikia majumbani (LPG ya kilo 6 na 15); usambazaji wa gesi asilia katika mkoa wa Lindi na Pwani pamoja na ujenzi wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia katika Taasisi za Umma.
Kwa upande wake, Dkt. Venance Mwasse, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO ameishukuru Serikali kupitia REA kwa mchango huu ambao utasaidia Shirika hilo kutimiza ndoto yake ya kuhakikisha wananchi wote wanaachana na nishati isiyo safi na salama ya kupikia ifikapo mwaka 2034 na hivyo kuunga mkono juhudi za Serikali za kutunza mazingira.
“Hii ajenda ya matumizi ya nishati safi ambayo kinara wake ni Rais wa Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan inalenga kumkomboa Mwanamke ili aachane na nishati isiyo safi na salama. STAMICO tumejipanga kutekeleza maono haya ya Kiongozi wetu”, amesema Dkt. Mwasse.
Ameongeza kuwa nishati ya Rafiki Briquettes kwa sasa inatumiwa na Jeshi la Magereza ambapo Magereza yote 129 nchini kote yanatumia nishati hii kama aina mojawapo ya nishati ya kupikia, vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Taasisi nyingine ni pamoja na vyuo mbalimbali vya mafunzo, shule za msingi na sekondari, hoteli, migahawa, na sehemu wanazochoma nyama na chipsi.
Dkt. Mwasse amesisitiza kuwa STAMICO itaendelea kutunza mitambo hiyo ili iendelee kutoa huduma kwa Wananchi.
MWISHO!!!