Oryx Gas yakabidhi vifaa vya kuhifadhia taka kwa Shule ya Msingi Kisiwani.
habariNa Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Oryx Gas imewakumbusha Watanzania kuhakikisha wanaendelea kutunza mazingira kwa kuhakikisha wanatumia nishati safi ya kupikia ambayo ni rafiki wa mazingira.
BENKI YA CRDB YANG'ARA KATIKA TUZO ZA AFRICAN BANKER 2025,YATWAA TUZO YA BENKI BORA KWA WAJASIRIAMALI
habari

Dar es Salaam, 05 Juni 2025 – Benki ya CRDB imeandika ukurasa mpya wa mafanikio baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME) katika hafla ya tuzo za sekta ya benki barani Afrika ‘African Banker Awards 2025,’ iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) jijini Abidjan, Côte d’Ivoire.
Kaulimbiu ya mwaka huu wa tuzo hizo ilikuwa “Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo Endelevu,” ikiakisi umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchochea ukuaji wa kijani, ujumuishi wa kijinsia na uhimilivu wa kiuchumi barani Afrika.
Katika mwaka huu ambapo Benki ya CRDB inaadhimisha miaka 30 ya huduma ubunifu, ilipata heshima ya kutajwa katika vipengele vinne vikuu, vikiwemo: Benki Bora kwa Wajasiriamali (Mshindi), Banker of the Year – kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki, Abdulmajid Mussa Nsekela, Benki Bora kwa maendeleo endelevu, Benki Bora ya mwaka (AFAWA).
Tuzo hiyo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali ilipokelewa na Afisa Mkuu wa Biashara, Boma Raballa, ambaye alieleza kuwa ushindi huo ni kielelezo cha dhamira ya Benki hiyo ya kuwapatia wateja na watanzania kwa ujumla wake huduma bunifu za fedha. Katika miaka 30 tokea kuanzishwa kwake, benki hiyo imeendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wajasiriamali, hususan vijana na wanawake. “Ushindi huu si wetu pekee, bali ni wa jamii nzima tunayoihudumia,” ameeleza Raballa.
Benki ya CRDB imejidhihirisha kuwa mshirika mkubwa wa wajasiriamali nchini ikitoa uwezeshaji wa hadi shilingi bilioni 5. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2024 mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.2 imetolewa kwa zaidi ya wajasiriamali 230,000 kutoka sekta mbalimbali.
Benki ya CRDB imekuwa kinara katika huduma bunifu kwa wajasiriamali nchini, ikiwa Benki ya kwanza kuanzisha kitengo maalum kwa ajili ya kuhudumia kundi hili la wateja mwaka 2000.
Mwaka 2024, Benki ya CRDB ilifanya maboresho makubwa ya akaunti ya wajasiriamali ‘Biashara Akaunti’, ikiboresha pia fursa za uwezeshaji kupitia mikopo, pamoja na kutoa suluhisho za kidijitali kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa upokeaji malipo kwa wateja kupitia huduma za ‘LIPA HAPA’ na mashine za manunuzi (PoS).
Aidha, Benki hiyo pia inazo bidhaa mahususi kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashra wanaogaiza bidhaa nje ya nchi kama ‘Mkopo wa Komboa,’ ukisaidia wateja kutoa mizigo yao bandarini kwa wakati. Hatua ambayo imeondoa ucheleweshaji katika uzalishaji na usambazaji wa bidhaa sokoni.
Sambamba na huduma, Benki pia inatoa huduma za ufadhili wa biashara (trade finance) na ufadhili wa rasilimali (asset financing), ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa wateja katika kukuza na kuimarisha biashara zao.
Benki ya CRDB pia imekuwa ikiwapatia wajasiriamali uzoefu wa biashara kimataifa kwa kuwapeleka nchi mbalimbali duniani ili kuwapa fursa za kujifunza na kuongeza thamani kwenye biashara wanazozifanya, huku ikiwajengea uwezo wa kushindana katika masoko ya kimataifa. Hii ni hatua muhimu katika kukuza ushindani wa bidhaa na huduma za Kitanzania.
Aidha Benki ya CRDB imekuwa ikishirikiana kimakakati na tasisi za kimataifa zinazolenga kuwasaidia wajasiriamali kama vile AGF, PROPARCO, DFC, GuarantCo na GCF pamoja na taasisi za hapa nchini kama vile PASS na TADB. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Benki hiyo imeweza kukusanya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 700, ikionyesha imani ya washirika wa kimataifa katika uwezo na utayari wa benki katika kuwawezesha wajasiriamali nchini.
“Katika miaka 30 ya uwepo wetu, tumejifunza kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila kuwainua wajasiriamali. Tunaendelea kujipanga kufikia wengi zaidi kupitia mikakati madhubuti ya ujumuishi, hasa kwa wanawake na vijana, kama sehemu ya kusaidia ajenda ya serikali ya maendeleo jumuishi,” aliongeza Raballa.
Tuzo hii ni ushahidi mwingine wa jinsi Benki ya CRDB imejikita kwa dhati katika kuwa daraja la mafanikio kwa maelfu ya wajasiriamali nchini. Kuelekea mbele, Benki hiyo imeendelea kuonyesha utayari wake katika kuwahudumia wajasiriamali kwa kutoa kipaumbele kikubwa kwa kundi hilo la wateja katika Mkakati wake wa Muda wa Kati wa Biashara wa 2023 – 2027.
UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 95
habari📌 *Dkt. Biteko apongeza; akumbusha Watendaji umuhimu wa tathmini katika kuboresha utendaji kazi*
📌 *Ataka TANESCO kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme; kubuni vyanzo vipya*
📌 *Aziagiza Taasisi chini ya Wizara kuungana kuitekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia*
📌 *Ofisi ya Waziri Mkuu yaipongeza Wizara kutekeleza miongozo ya ufuatiliaji na Tathmini kwa asilimia 100*
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuimarisha utendaji kazi na hivyo kuifanya Sekta ya Nishati kuwa na matokeo chanya katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo kufuatia tathmini ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati ambayo imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi wa Wizara/Taasisi umeimarika kwa zaidi ya asilimia 95.
Katika kikao cha Nne cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kilichofanyika jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema kuwa, tathmini hiyo inasaidia kujiimarisha hasa ikizingatiwa kuwa Sekta ya Nishati ina muhimu mkubwa kiuchumi na kijamii.
“Sekta hii ni muhimu sana nchini kwa kuwa ni Sekta ya huduma na sekta ya uchumi hivyo ikilegalega italeta malalamiko, ningependa kuona sekta hii inaendelea kuwa na matokeo mazuri kwa wananchi.” Amesema Dkt. Biteko
Katika kikao hicho, Dkt. Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuendelea na kasi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme pamoja na kuendelea kutafuta vyanzo vipya vya umeme.
Aidha, ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kasi iliyofanya ya kupeleka umeme vijijini na kuwezesha vijiji vyote kupata umeme pia kwa kuendelea na kasi ya kupeleka umeme vitongojini.
Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, Dkt. Biteko amezitaka Taasisi zilizo chini ya Wizara hususan, REA, TPDC na TANESCO kuunganisha nguvu katika kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili ikue na kufanikiwa na hivyo kutimiza lengo la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kuwa wananchi wanahama kutoka matumizi ya Nishati isiyo safi kwenda kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.
Dkt. Biteko amekipongeza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati kwa kutekeleza jukumu lao kwa ufanisi na kukumbusha Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kuwa, zoezi hilo la tathmini linapaswa kuwa ni endelevu kutokana na umuhimu wake katika kuboresha utendaji kazi.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith.Kapinga kwa upande wake, amezipongeza Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Idara na Vitengo vya Wizara ya Nishati kwa utendaji kazi wenye kuleta matokeo kama ambavyo tathmini ya utendaji kazi iliyotolewa ilivyoonesha kuwa ufanisi wa kazi umeendelea kuimarika.
Aidha amezitaka Taasisi chini ya Wizara ya Nishati kuibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo la Serikali la kufikisha asilimia 80 ya Watanzania wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034.
Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema kuwa kikao hicho cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara na Taasisi zake ni cha nne kutoka vikao vivyo vimeanza kufanyika.
Alieleza kuwa, kutoka zoezi la kupima utendaji kazi wa Wizara na Taasisi lianze kufanyika limeleta ufanisi hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya Wizara.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Sakina Mwinyimkuu ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutekeleza miongozo iliyowekwa na Ofisi hiyo ya ufuatiliaji na tathmini ambapo ameeleza kuwa Wizara ya Nishati imetekeleza miongozo iliyowekwa kwa asilimia 100.
Pia amempongeza Dkt. Doto Biteko kwa dhamira yake ya dhati katika kusimamia utendaji kazi wa Serikali hasa Sekta ya Nishati ambayo anaisimamia akiwa ni Waziri wa Nishati.
Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutoa motisha kwa Taasisi na Idara/Vitengo zilizofanya vizuri zaidi katika tathmini ya utendaji kazi hali ambayo inaongeza ari ya kazi.
Taasisi zilizofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni Wakala wa Nishati Vijijini (REA) aliyeshika nafasi ya kwanza, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) aliyeshika nafasi ya pili na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) aliyeshika nafasi ya tatu.
Aidha, Idara/Vitengo vya Wizara ya Nishati vilivyofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni Kitengo cha Ugavi na Manunuzi (nafasi ya kwanza), Kitengo cha Sheria (nafasi ya pili), na Kitengo cha TEHAMA (nafasi ya tatu).
Mikoa ya Kitanesco iliyofanya vizuri katika tathmni ya utendaji kazi ni Manyara (nafasi ya kwanza), Arusha (nafasi ya pili) na Simiyu (nafasi ya tatu).
Hata hivyo ilielezwa kuwa kwa ujumla ufanisi wa utendaji kazi wa Idara na Vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake umeendelea kuimarika kwa zaidi ya asilimia 95.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt, James Mataragio, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Menejimenti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake pamoja na Mameneja wa Mikoa wa TANESCO.