Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

BENKI YA CRDB YANG'ARA KATIKA TUZO ZA AFRICAN BANKER 2025,YATWAA TUZO YA BENKI BORA KWA WAJASIRIAMALI

June 05, 2025 Add Comment

 


Dar es Salaam, 05 Juni 2025 – Benki ya CRDB imeandika ukurasa mpya wa mafanikio baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME) katika hafla ya tuzo za sekta ya benki barani Afrika ‘African Banker Awards 2025,’ iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) jijini Abidjan, Côte d’Ivoire.

Kaulimbiu ya mwaka huu wa tuzo hizo ilikuwa “Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo Endelevu,” ikiakisi umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchochea ukuaji wa kijani, ujumuishi wa kijinsia na uhimilivu wa kiuchumi barani Afrika.

Katika mwaka huu ambapo Benki ya CRDB inaadhimisha miaka 30 ya huduma ubunifu, ilipata heshima ya kutajwa katika vipengele vinne vikuu, vikiwemo: Benki Bora kwa Wajasiriamali (Mshindi), Banker of the Year – kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki, Abdulmajid Mussa Nsekela, Benki Bora kwa maendeleo endelevu, Benki Bora ya mwaka (AFAWA).

Tuzo hiyo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali ilipokelewa na Afisa Mkuu wa Biashara, Boma Raballa, ambaye alieleza kuwa ushindi huo ni kielelezo cha dhamira ya Benki hiyo ya kuwapatia wateja na watanzania kwa ujumla wake huduma bunifu za fedha. Katika miaka 30 tokea kuanzishwa kwake, benki hiyo imeendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wajasiriamali, hususan vijana na wanawake. “Ushindi huu si wetu pekee, bali ni wa jamii nzima tunayoihudumia,” ameeleza Raballa.

Benki ya CRDB imejidhihirisha kuwa mshirika mkubwa wa wajasiriamali nchini ikitoa uwezeshaji wa hadi shilingi bilioni 5. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2024 mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.2 imetolewa kwa zaidi ya wajasiriamali 230,000 kutoka sekta mbalimbali.

Benki ya CRDB imekuwa kinara katika huduma bunifu kwa wajasiriamali nchini, ikiwa Benki ya kwanza kuanzisha kitengo maalum kwa ajili ya kuhudumia kundi hili la wateja mwaka 2000.

Mwaka 2024, Benki ya CRDB ilifanya maboresho makubwa ya akaunti ya wajasiriamali ‘Biashara Akaunti’, ikiboresha pia fursa za uwezeshaji kupitia mikopo, pamoja na kutoa suluhisho za kidijitali kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa upokeaji malipo kwa wateja kupitia huduma za ‘LIPA HAPA’ na mashine za manunuzi (PoS).

Aidha, Benki hiyo pia inazo bidhaa mahususi kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashra wanaogaiza bidhaa nje ya nchi kama ‘Mkopo wa Komboa,’ ukisaidia wateja kutoa mizigo yao bandarini kwa wakati. Hatua ambayo imeondoa ucheleweshaji katika uzalishaji na usambazaji wa bidhaa sokoni.

Sambamba na huduma, Benki pia inatoa huduma za ufadhili wa biashara (trade finance) na ufadhili wa rasilimali (asset financing), ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa wateja katika kukuza na kuimarisha biashara zao.

Benki ya CRDB pia imekuwa ikiwapatia wajasiriamali uzoefu wa biashara kimataifa kwa kuwapeleka nchi mbalimbali duniani ili kuwapa fursa za kujifunza na kuongeza thamani kwenye biashara wanazozifanya, huku ikiwajengea uwezo wa kushindana katika masoko ya kimataifa. Hii ni hatua muhimu katika kukuza ushindani wa bidhaa na huduma za Kitanzania.

Aidha Benki ya CRDB imekuwa ikishirikiana kimakakati na tasisi za kimataifa zinazolenga kuwasaidia wajasiriamali kama vile AGF, PROPARCO, DFC, GuarantCo na GCF pamoja na taasisi za hapa nchini kama vile PASS na TADB. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Benki hiyo imeweza kukusanya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 700, ikionyesha imani ya washirika wa kimataifa katika uwezo na utayari wa benki katika kuwawezesha wajasiriamali nchini.

“Katika miaka 30 ya uwepo wetu, tumejifunza kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila kuwainua wajasiriamali. Tunaendelea kujipanga kufikia wengi zaidi kupitia mikakati madhubuti ya ujumuishi, hasa kwa wanawake na vijana, kama sehemu ya kusaidia ajenda ya serikali ya maendeleo jumuishi,” aliongeza Raballa.
Tuzo hii ni ushahidi mwingine wa jinsi Benki ya CRDB imejikita kwa dhati katika kuwa daraja la mafanikio kwa maelfu ya wajasiriamali nchini. Kuelekea mbele, Benki hiyo imeendelea kuonyesha utayari wake katika kuwahudumia wajasiriamali kwa kutoa kipaumbele kikubwa kwa kundi hilo la wateja katika Mkakati wake wa Muda wa Kati wa Biashara wa 2023 – 2027.

MHE. MCHENGERWA AWAFUNDA WALIMU

June 04, 2025 Add Comment

Na John Mapepele

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa rai kwa walimu nchini kuwa wazalendo na kuzingatia weledi ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 95

June 04, 2025 Add Comment



📌 *Dkt. Biteko apongeza; akumbusha Watendaji umuhimu wa tathmini katika kuboresha utendaji kazi*


📌 *Ataka TANESCO kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme; kubuni vyanzo vipya*


📌 *Aziagiza Taasisi chini ya Wizara kuungana kuitekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia*


📌 *Ofisi ya Waziri Mkuu yaipongeza Wizara kutekeleza miongozo ya ufuatiliaji na Tathmini kwa asilimia 100*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza Watendaji wa  Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuimarisha utendaji kazi na hivyo kuifanya Sekta ya Nishati kuwa na matokeo chanya katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo kufuatia tathmini ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati ambayo imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi  wa Wizara/Taasisi umeimarika kwa zaidi ya asilimia 95.


Katika kikao cha Nne cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kilichofanyika jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema kuwa, tathmini hiyo inasaidia  kujiimarisha hasa ikizingatiwa kuwa Sekta ya Nishati ina muhimu mkubwa kiuchumi na kijamii.

“Sekta hii ni muhimu sana nchini kwa kuwa ni Sekta ya huduma na sekta ya uchumi hivyo ikilegalega italeta malalamiko, ningependa kuona sekta hii inaendelea kuwa na matokeo mazuri kwa wananchi.” Amesema Dkt. Biteko

Katika kikao hicho, Dkt. Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuendelea na kasi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme pamoja na kuendelea kutafuta vyanzo vipya vya umeme.


Aidha, ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kasi iliyofanya ya kupeleka umeme vijijini na kuwezesha vijiji vyote kupata umeme pia kwa kuendelea na kasi ya kupeleka umeme vitongojini.

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, Dkt. Biteko amezitaka Taasisi zilizo chini ya Wizara hususan, REA, TPDC na TANESCO kuunganisha nguvu katika kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili ikue na kufanikiwa na hivyo kutimiza lengo la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kuwa wananchi wanahama kutoka matumizi ya Nishati isiyo safi kwenda kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Dkt. Biteko amekipongeza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati  kwa kutekeleza jukumu lao kwa ufanisi na kukumbusha Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake  kuwa, zoezi hilo la tathmini linapaswa kuwa  ni endelevu kutokana na umuhimu wake katika kuboresha utendaji kazi.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith.Kapinga kwa upande wake, amezipongeza Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Idara na Vitengo vya Wizara ya Nishati kwa utendaji kazi wenye kuleta matokeo kama ambavyo tathmini ya utendaji kazi iliyotolewa ilivyoonesha kuwa ufanisi wa kazi umeendelea kuimarika.

Aidha amezitaka Taasisi chini ya Wizara ya Nishati kuibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo la Serikali la kufikisha asilimia 80 ya Watanzania wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema kuwa kikao hicho cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara na Taasisi zake ni cha nne kutoka vikao vivyo vimeanza kufanyika.

Alieleza kuwa, kutoka zoezi la kupima utendaji kazi wa Wizara na Taasisi lianze kufanyika limeleta ufanisi hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya Wizara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini  ya Utendaji wa Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Sakina Mwinyimkuu ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutekeleza miongozo iliyowekwa na Ofisi hiyo ya ufuatiliaji na tathmini ambapo ameeleza kuwa Wizara ya Nishati imetekeleza miongozo iliyowekwa kwa asilimia 100.

Pia amempongeza Dkt. Doto Biteko kwa dhamira yake ya dhati katika kusimamia utendaji kazi wa Serikali hasa Sekta ya Nishati ambayo anaisimamia akiwa ni Waziri wa Nishati.

Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutoa motisha kwa Taasisi na Idara/Vitengo zilizofanya vizuri zaidi katika tathmini ya utendaji kazi hali ambayo inaongeza ari ya kazi.

Taasisi zilizofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) aliyeshika nafasi ya kwanza, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) aliyeshika nafasi ya pili na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) aliyeshika nafasi ya tatu.  

Aidha, Idara/Vitengo vya Wizara ya Nishati vilivyofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni  Kitengo cha Ugavi na Manunuzi (nafasi ya kwanza), Kitengo cha Sheria (nafasi ya pili), na Kitengo cha TEHAMA (nafasi ya tatu).

Mikoa ya Kitanesco iliyofanya vizuri katika tathmni ya utendaji kazi ni Manyara (nafasi ya kwanza), Arusha (nafasi ya pili) na Simiyu (nafasi ya tatu).

Hata hivyo ilielezwa kuwa kwa ujumla ufanisi wa utendaji kazi wa Idara na Vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake umeendelea kuimarika kwa zaidi ya asilimia 95.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt, James Mataragio, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Menejimenti ya Wizara ya Nishati  na Taasisi zake pamoja na   Mameneja  wa Mikoa wa TANESCO.

ZAO LA PAMBA LINAWEZA KUPUNGUZA UMASKINI KUANZIA NGAZI YA KAYA MPAKA TAIFA

June 03, 2025 Add Comment

 


Na Oscar Assenga,TANGA

WANANCHI wanaoishi kwenye maeneo yanayostahimili kilimo cha Pamba wametakiwa kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo ambalo ni la kimkakati la kibiashara kutokana na kwamba linaweza kusaidia kupunguza kiasi cha umaskini kwenye ngazi ya kaya,wilaya na Taifa kwa ujumla

Hayo yalisemwa jana na Afisa wa Bodi ya Pamba Tanzania Alphonce Ngawagala wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya 12 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga.

Alisema kwamba leng la wao kushiriki kwenye maonyesho hayo ni kutangaza fursa zinazopatikana kwenye bodi hiyo kwa kuwaelimisha wananchi maeneo gani yanafaa kulima pamba na pembejeo  zinapatikana kwa utaratibu upi ambao ni bure.

Alisem kwamba pia baada ya mkulima na kuvuna wanaanzisha soko la mkulima ili aweze kuuza mazao yake kwa wakati ili aongeze kipato chake apate awekeze kwenye mambo mengine ya kimaendeleo.

Aidha alisema kwamba bodi hiyo imepewa dhamana ya kusimamia usindikaji,uzalishaji na kusimamia masoko pamoja na kuelimisha wananchi maeneo yanayotakiwa kulimwa pamba na pembejeo zinapatikana kwa utararibu upi ambao ni bure na baadae ya kulima hizo wao wanasimamia soko ili wakulima wauze.

“Lakini uchakataji wa Pamba inapokwenda kiwandani napo bodi ipo  kwa ajili ya kusimamia inasimamia kuhakikisha shughuli zote zinafuata utaratibu, sheria na kanuni zilizowekwa ikiwemo kuangalia ubora na usafi unapatikani”Alisema

Alisema wanafanya hivyo ili kumuwezesha yule mchambuaji baada ya kumaliza taratibu zake aweze kupata kibali kama maborota yake yanapelekwa nje ya nchi apeleke kwa wakati kwa kukamailisha tararibu zote.

Mwisho.

BALOZI DK.NCHIMBI AMWAKILISHA RAIS SAMIA KUMUAGA HAYATI SONGAMBELE MKOANI RUVUMA

June 02, 2025 Add Comment



Na Mwandishi Wetu,Songea

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika shughuli ya kuaga mwili wa Hayati Alhaj Mustafa Mohamed Songambele iliyofanyika nyumbani kwa marehemu eneo la Mahenge, mjini Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza katika shughuli hiyo, Dkt. Nchimbi amemuelezea Hayati Songambele kama mmoja wa mashujaa waliotoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanzania na kujenga misingi ya taifa jipya baada ya ukoloni.


Dk.Nchimbi amesema Hayati Songambele alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha TANU na alishiriki kikamilifu katika harakati za kujenga taifa huru na lenye mshikamano.


"Tuendelee kujifunza kutoka kwa wazee hawa ambao wamefariki wakiona amani na upendo wa Tanzania ukiendelea, heshima pekee tunayoweza kuwapa ni kuendeleza mshikamano, amani na maendeleo ya nchi yetu…


“Tuendelee kujua sisi ni Taifa moja, tuna wajibu wa kupendana na kujiepusha na vishawishi vyote ambavyo vinaweza vikavuruga amani na kuvunja mtangamano wa kitaifa," alisema Dkt. Nchimbi.


Dkt. Nchimbi aliongeza kuwa Rais Dkt. Samia ameguswa sana na msiba huo, akimwelezea Hayati Songambele kama kiongozi mwenye moyo wa kipekee wa kulitumikia taifa kwa hali na mali, na kwamba wananchi wa Ruvuma wana kila sababu ya kujivunia mchango wake mkubwa.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema kifo cha Mzee Songambele ni pigo kubwa kwa Taifa, akieleza kuwa marehemu alikuwa ni hazina ya busara na kumbukumbu muhimu ya historia ya Tanzania.


"Hakuwa tu kiongozi bali alikuwa taa na mwelekeo katika giza la ukoloni, aliyesimama kidete kwa ujasiri, hekima, na moyo wa kizalendo katika kuijenga Tanzania mpya. Alisimama kwa haki, kupitia juhudi zake na viongozi wenzake wa wakati huo, tunauona leo mwanga wa uhuru, umoja, na amani uliodumu kwa zaidi ya nusu karne," alisema Kanali Ahmed.


Akizungumza kwa niaba ya familia, Mtoto wa Hayati Songambele, Rajab Songambele amesema wataendelea kuyaenzi na kuyatekeleza mema yote waliyofundishwa na Mzee wao ili yadumu kwa vizazi vijavyo.

Hayati Alhaj Mustafa Mohamed Songambele alikuwa ni mmoja wa waanzilishi wa Chama cha TANU akiwa miongoni mwa wanachama wa kwanza 30 wa chama hicho, na alipata kadi ya uanachama namba 27.

Alizaliwa Mei 25, 1925 katika eneo la Bombambili, Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma na amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 100.