Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

TASAC YATOA ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA DODOMA

June 02, 2025 Add Comment



Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania TASAC, leo tarehe 02 Juni, 2025 limetoa elimu ya utunzaji wa mazingira majini kwa wadau waliotembelea banda lao jijini Dodoma.

TASAC imetoa elimu hiyo kwa wadau na wananchi wa Dodoma katika Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani 2025 yanayofanyika kuanzia tarehe 01 - 05 Juni, 2025 jijini humo. 



Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wataalamu wa TASAC wameeleza wananchi namna wanavyotekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na jukumu la kusimamia na kudhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira pamoja na kupambana na umwagikaji wa mafuta majini.

Baadhi ya wadau waliotembelea banda hilo ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Ladislaus Chang’a ambapo amepongeza juhudi za TASAC katika kutumia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA.

TASAC ni moja ya taasisi za umma zinazoshiriki maadhimisho hayo yenye kauli mbiu: “Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo Tuwajibike Sasa, Dhibiti Matumizi ya Plastiki”. Kilele cha maadhimisho hayo ni tarehe 05 Juni 2025.

NSSF YAWATAKA WAAJIRI KULIPA MICHANGO KWA WAKATI WASISUBIRI MPAKA WAPELEKWE MAHAKAMANI

June 01, 2025 Add Comment




Na Oscar Assenga,Tanga

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) umewataka waajiri kuhakikisha wanalipa michango ya watumishi wao kwa wakati na wasisubiri mpaka wapelekwe mahakamani kutokana na kutokuiwasilisha .

Hayo yalisemwa leo na Meneja wa NSSF Mkoa wa Tanga Nuhu Mbaga katika maonyesho ya 11 ya Biashara na Utalii yanayoendelea katika eneo la Mwahako Jijini Tanga.

Ambapo alisema wanashiriki maonyesho hayo kwa lengo la kutoe elimu kwa wananchi juu ya mafao mbalimbali wanayoyatoa wanapojiunga nao.

Alisema kwamba wanatakiwa kulipa michango kwa sababu ipo kwa mujibu wa sheria na wasipofanya hivyo kifungu cha 72 wanaweza kukitumia kwa ajili ya wao kupelekwa mahakamani.

“Hivyo nitumie nafasi hii kuwataka waajiri tusisubiri mpaka mpelekwe mahakamani bali wahakikisheni mnatekeleza wajibu wenu kupeleka michango ya watumishi wenu”Alisema

Aidha alitumia wasaa huo kuwahamasisha wananchi waliojiajiri kufika kwenye banda lao kuweza kupata elimu ya kuweza kujiunga na kunufaika na mafao mbalimbali yanayotolewa kwenye mfuko huo ikiwemo ya kupata matibabu kama ilivyo kwa wengine

“Yote haya ni kutokana na sera nzuri ya awamu ya sita chiini ya Rais Dkt Samia Suluhu kwa sababu mtu akiwa na afya njema ataweza kwenda kujishughulisha na kufanya kazi ya kupata kipato cha mtu mmoja mmja na kuweza kujikwamua kiuchumi”Alisema

GCLA KANDA YA KATI YATOA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAJANGA YA KEMIKALI KWA WAKAZI WA RUAHA MBUYUNI

May 31, 2025 Add Comment
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilolo, Eston Kyando (aliyesimama) akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa makundi mbalimbali ya viongozi wa Kata ya Ruaha Mbuyuni juu ya namna ya kukabiliana na majanga ya kemikali ikiwemo ajali za magari yanayosafirisha kemikali. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa shule ya msingi Mbuyuni A, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, Mei 30, 2025. Kulia ni Meneja wa Usajili wa Kemikali na Maabara za Kemia, Musa Kuzumila.