Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

TANESCO MUHEZA: KATIKATIKA YA UMEME ILITOKANA NA WIZI WA NYAYA ZA KOPA KWENYE TRANSFOMA

May 22, 2025 Add Comment


Na Paskal Mbunga, MUHEZA.

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) katika wilaya ya Muheza Mkoani Tanga limetolea ufafanuzi katikakatika ya Umeme katika wiki mbili zilizopita ilitokana na kuibiwaa kwa wizi wa nyaya za kopa kwenye Transfoma 18 katika maeneo tofauti tofauti wilayani humo na hivyo kupelekea kuungua na kusababisha umeme kuzima.

Hayo yalisemwa na Meneja wa TANESCO wilaya ya Muheza African Chuwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kutolea ufafanuzi suala hilo lililosababisha baadhi ya wananchi kulalamika, ambapo alisema jitahada zilifanywa ili kuurejesha umeme kwa haraka.

Alisema wakati wa zoezi la kurejesha umeme, walilazimika kufanya majaribio ili kutambua eneo lenye matatizo kwani wilaya hiyo pia inapeleka huduma ya umeme kwenye wilaya za Mkinga na Pangani.

Alibainisha kwamba kwa vile baadhi ya maeneo yanachukua umeme kutoka Muheza, na kwamba ili kubaini tatizo lipo upande upi, ilikuwa lazima kwanza kuurejesha umeme ili endapo itazima, watabaini changamoto ipo wapi. Alieleza kwamba wanaendelea kufuatilia vitendo vya wizi wa waya unaofanywa na baadhi ya watu uliosababisha b umeme kukatika mara kwa mara.

“Lakini niwaambie kwamba tatizo jingine linalosababisha umeme kukatikakatika ni matengenezo makubwa yanayofanyika pale kituo cha kuzalisha umeme Hale yanayopelekea kuzimwa kwa line inayokwenda Muheza na kusisitiza kwamba wanalazimika kuzima umeme wakati wa matengenezo wa line inayotoka Hale kwenda Songa na kwenda Muheza na line inayotoka Kituo cha Hale Songa kwenda Korogwe.

Hata hivyo alibainisha kwamba Ofisi ya TANESCO wilayani Muheza inatoa taarifa kwa wananchi ya uwepo wa matengenezo na kwamba wakati wa matengenezo hayo, umeme huzimwa. Meneja huyo wa TANESCO wilayani hapa alifahamisha kwamba kutakuwa na katikakatika kwa umeme wakati wa matengenezo yanayoendelea kwa kipindi cha miezi minne hadi mwezi Agosti, 2025 ambapo yatakuwa yamekamilika.



(Mwisho)

Tanzania na Umoja wa Ulaya kuendeleza Ushirikiano wa Kimkakati

May 22, 2025 Add Comment
Brussels, 21 Mei,2025

Tanzania na Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuendeleza ushirikiano wa kimkakati baina yao.

DKT. KILABUKO AZINDUA MWONGOZO WA KITAIFA KWA WATOA HUDUMA ZA MAENDELEO YA BIASHARA

May 21, 2025 Add Comment
NA. MWANDISHI WETU - DAR ES SALAAM

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. James Kilabuko amezindua rasmi Mwongozo wa Kitaifa kwa Watoa Huduma za Maendeleo ya Biashara katika hafla iliyofanyika kwenye Hoteli ya Four Points by Sheraton, Jijini Dar es Salaam.

KUPITIA MRADI WA FEMA AILEADERS WABUNGE WABUNIFU NA MAKUNDI MENGINE WAPIGWA MSASA AKILI MNEMBA

May 21, 2025 Add Comment





Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam


Kupitia Mradi wa FemAILeaders, Shirika la Women Political Leaders (WPL), GIZ Makao Makuu, GIZ Tanzania na Omuka imeandaa Mafunzo ya Akili Mnemba “Artificial Intelligence - AI” yaliyoanza Mei  19 hadi 20 mwaka 2025, Dar es Salaam yaliyolenga mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa mtandao,ubunifu na matumizi ya AI.

 

Mafunzo haya yaliwaleta pamoja Wabunge, Wabunifu na Makundi mengine kwa lengo la kuangazia ubunifu na matumizi ya AI, ulinzi wa kimtandao, utatuzi wa changamoto za AI na uhitaji wa kisera.

Delegation ya Bunge iliongozwa na Mhe Salome Makamba na kujumisha Mhe Prof Joyce Ndalichako, Mhe Esther Matiko, Mhe Ng’wasi Kamani na Makatibu wa Kamati za Bunge, Adv Ganjatuni Kilemile na Pius Katabazi.

 

Tanzania imeendelea kuongoza barani Afrika kwa Kuimarisha Uelewa na Ushawishi wa Wabunge Wanawake ili wawe Vinara wa AI hivyo kuchangia kwa Tanzania kunufaika na fursa zinazotokana na Akili Mnemba - AI. Tanzania imechaguliwa kuwa Mfano wa Kuigwa barani Afrika katika eneo hili. 

 

Aidha, Mradi wa FemAILeaders umeweza kufanyika Tanzania kufuatia jitihada za Mhe Neema Lugangira (Mb) ambae pja ni Mwakilishi wa Afrika/Mjumbe Maalum wa Afrika wa Shirika la Women Political Leaders (WPL) hivyo ametumia nafasi hiyo kuileta fursa hii Tanzania.
 

DC SAME APIGA MARUFUKU MAJI MACHAFU YA KIWANDA KUINGIA MTONI

May 21, 2025 Add Comment

 




Na Ashrack Miraji

Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amepiga marufuku mara moja utiririshaji wa maji machafu yenye kemikali kutoka katika Kiwanda cha kuchakata mkonge kinachomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MELT), kilichopo katika shamba la mkonge la Hassan Sisal Estate, Kata ya Makanya.

Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia wasiwasi wa uchafuzi wa mazingira na athari za kiafya kwa wakazi wa Makanya na maeneo jirani yanayopata huduma ya maji kupitia mto unaopita karibu na kiwanda hicho.

Mhe. Kasilda alitembelea baadhi ya maeneo ya mto huo na kujionea hali ya maji yaliyobadilika rangi kuwa nyeusi na kutoa harufu kali, hali iliyomsukuma kufika kiwandani kujiridhisha na chanzo cha uchafuzi huo.


“Kuanzia sasa ni marufuku kuelekeza maji machafu yenye kemikali kwenye mto ambao maji yake yanatumika kwa shughuli mbalimbali za kibinadamu, hususan kilimo na mifugo. Baadhi ya wananchi wanayatumia moja kwa moja,” alisema DC Kasilda.

Alisisitiza kuwa uamuzi huo unalenga kulinda afya za wananchi na mazingira kwa ujumla.

Aidha, Mhe. Kasilda alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same kuhakikisha wataalam wa mazingira na afya wanafika kiwandani hapo kufanya uchunguzi wa kina ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria.


“Serikali inathamini uwekezaji, lakini ni lazima wawekezaji wazingatie sheria na taratibu ili kulinda afya za wananchi na kukuza uchumi wa taifa kwa njia endelevu,” alisema.

Katika ziara hiyo, Mkuu huyo wa wilaya pia alieleza kutoridhishwa na hali ya usafi kiwandani hapo na kuwataka wasimamizi wa kiwanda kufanya usafi wa maeneo yao ya kazi ili kuepuka hatari ya magonjwa ya mlipuko kwa wafanyakazi.

Kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004, kifungu cha 129 kinakataza mtu yeyote kuachilia maji taka au taka hatarishi moja kwa moja kwenye mazingira bila kibali au bila kuyatibu.

Sheria hiyo pia inataka viwanda kuwa na mitambo ya kisasa ya kutibu majitaka kabla ya kuyamwaga kwenye mazingira. Endapo ukiukwaji utabainika, Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira (NEMC) itachukua hatua kali dhidi ya wahusika.