Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

TANZANIA,MOROCCO KUCHOCHEA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI

May 14, 2025 Add Comment

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morroco

Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini
Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini


Sehemu ya wajumbe mbalimbali alioambatana nao Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko wakati wa mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Morocco, Mei 14, 2025.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali mara baada ya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.

katika mazungumzo hayo, Dkt. Biteko aliongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na mwakilishi katika eneo la Morocco, Mhe. Ali Jabir Mwadini pamoja na Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  nishati vijijini (REA), Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Mei 14, 2025.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morocco.



📌 Matumizi ya teknolojia kupewa kipaumbele Sekta ya Nishati


📌 Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Tanzania na Ufalme wa Morocco zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa matumizi ya teknolojia katika Sekta ya Nishati ili kuiwezesha sekta hiyo kuwa na mchango endelevu nchini.


Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa  Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko alipokutana na Mwenyeji wake Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.


"Mwaka 2016 Tanzania na Morocco zilisaini hati ya makubaliano (MoU) ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya umeme, mafuta na matumizi ya nishati mbadala ili yapewe kipaumbele katika nchi hizo, ". Amesema Dkt. Biteko


Mhe. Dkt. Biteko amesema pamoja na maendeleo ya nishati yaliyofikiwa, bado nchi inahitaji uwekezaji zaidi katika sekta ya nishati mbadala ikiwa na matarajio ya kukuza shughuli za kiuchumi hususan katika sekta za viwanda na madini jambo ambalo linahitaji uwekezaji wa kimkakati zaidi katika sekta ya nishati.


Ametaja mambo mengine ni pamoja na kubadilishana uzoefu miongoni mwa wataalam katika sekta ya nishati ikilenga kuifanya kuwa na tija kwa taifa na uchumi kwa ujumla.


Kwa upande wake, Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali amesema kuwa Tanzania inaweza kubadilisha sura yake kwa kuwa na juhudi za pamoja za kuunganisha rasilimali zilizopo kuhakikisha nishati ya umeme inawafikia wananchi wengi zaidi. 


Amesema hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana gizani hivyo, njia ya kuleta maendeleo na ustawi wa watu ni kuwaangaza maisha yao kwa kupitia sekta ya Nishati.


Aidha, Mhe. Benali amepongeza kwa dhati juhudi za Rais Samia kuwa kinara wa maendeleo ya nishati safi ya kupikia, Tanzania na Afrika kwa ujumla. 


Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi katika eneno la Morocco, Mhe. Ally Mwadini, Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).


Mwisho.

ZAIDI YA BILIONI 17 KUSAMBAZA UMEME VITONGOJINI SINGIDA

May 14, 2025 Add Comment
-Kunufaisha Kaya 3,960 kutoka katika Vitongoji 120 ndani ya Wilaya Tano

KATIBU TAWALA MKOA WA KATAVI, AHITIMISHA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU KITAIFA (GAWE) 2025

May 14, 2025 Add Comment

 

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akisisitiza jambo kwenye kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Na Mwandishi Wetu, Katavi

MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET) kwa kushirikiana na wanachama wake, imekusanya nguvu ya pamoja na kujitolea kiasi cha shilingi milioni 35,000,000 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika Halmashauri ya Mpimbwe, mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliofanyika mkoani hapa.

Akizungumza katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro alisema wametoa fedha hiyo ili iweze kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu katika Mkoa wa Katavi.

Akifafanua zaidi Bw. Nanyaro alisema wameguswa na muitikio mkubwa wa wazazi/walezi, viongozi wa mila na dini katika shule walizozitembelea wakiwa katika ziara za maadhimisho kwani walijumuika pamoja kujadili mambo mbali mbali muhimu yanayohusu elimu, ikiwemo jitihada kubwa za walimu katika kuendelea kuwafundisha wanafunzi wengi licha ya changamoto zinazowakumba katika mazingira ya ufudishaji hali inayoonyesha kufanya kazi kwa bidii, kujitolea na dhamira ya kuinua kiwango cha Elimu nchini.

"Tumeshuhudia changamoto kadha wa kadha zinazozikabili shule zetu zinazohitaji kushughulikiwa ili kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji: ikiwemo upungufu na uchakavu wa miundombinu ya madarasa kwa baadhi ya shule, upungufu wa walimu, hasa wa kike, ukosefu nyumba za walimu, hasa katika baadhi ya shule, ukosefu wa mabweni kwa wanafunzi, hasa wanaotoka vijiji vya mbali, unaolazimu watoto kutembea hadi kilometa 12 kila siku Kwenda na kurudi shuleni jambo linalochangia utoro na wengine kuacha shule kabisa." Alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro.

Aidha wadau hao wa elimu walipendekeza msaada walioutoa kusaidia kutatua changamoto ya jumla ya madawati 407 meza 10 na viti 10 kwa mchanganuo ufuatao; Madawati 250 yaende shule ya Msingi Migunga, Madawati 47 yasaidie Shule ya Msingi Ikulwe, Madawati 110 yapelekwe katika Shule ya Msingi Minyoso na meza 10 na Viti 10 ziende kwa ajili ya walimu wa shule ya sekondari Mirumba.

Pamoja na hayo walipendekeza viongozi wa Serikali kuandaa mpango na kutenga bajeti ya ujenzi wa hostel za wanafunzi wa kike na wakiume, kujenga matundu ya vyoo, vyumba vya kujisitiri wanafuzi wa kike wakati wa hedhi na upatikanaji wa maji safi na salama; utakaoendana sambasamba na ujenzi wa madarasa ili kukidhi uhitaji uliopo kwa sasa ili kulinda afya na usalama wa Watoto.

Wada wa elimu tunashauri viongozi katika sekta ya elimu ngazi ya wilaya na mkoa kuandaa ziara za mara kwa mara kutembelea shuleni kukutana na wanafunzi, walimu, kamati za shule na wazazi/walezi kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wanafunzi na walimu shuleni.  

"...Tunawahimiza wazazi na walezi kuendelea kuchangia utoaji wa chakula na lishe shuleni ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni na kusoma bila njaa ili kuongeza ufaulu wao na kupunguza utoro shuleni. Kuzingatia sheria na Kanuni za utoaji wa adhabu kwa Wanfunzi kama ilivoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu No. 24 wa mwaka 2002, unaotoa mwongozo namna ya utolewaji wa adhabu ya viboko shuleni. ili kuepuka kutoa adhabu kali za viboko kwa wanafunzi shuleni," alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro akiwasilisha taarifa ya wadau wa elimu baada ya kilele cha maadhimisho.

Baadhi ya viongozi na wananchi wakiwa katika hafla ya  Maadhimisho ya kilele cha Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.

UPANUZI WA KITUO CHA KUPOZA UMEME MBAGALA MBIONI KUKAMILIKA

May 14, 2025 Add Comment

 



Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange amesema wananchi wa maeneo ya Mbagala na viunga vyake sasa wanatarajia kupata umeme wa uhakika baada ya Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mbagala kuongezewa uwezo kutoka Megawati 45 za awali na kufikia Megawati 165.

Akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kutembelea Kituo hicho Bw. Twange alisema kuwa Kituo hicho kimeongezewa uwezo mara mbili ya awali hivyo kitakuwa na uwezo mkubwa wa kusambaza umeme na kuondoa kabisa changamoto ya kukatika kwa umeme katika maeneo hayo.

“Kituo hiki kimeongezewa uwezo mara mbili ya awali na mpaka sasa utekelezaji wa Mradi huu umefikia asilimia 70. Wananchi wa Mbagala na viunga vyake sasa wategemee umeme wa uhakika’’ alisisitiza Bw. Twange.

Pia, Mkurugenzi Mtendaji Bw. Lazaro amemshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa kiasi cha fedha Dola za Kimarekani milioni 6.4  ili kufanikisha Mradi huu wenye tija na manufaa kwa wananchi wa maeneo hayo na nchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sixtus  Mapunda, akizungumza wakati wa ziara hiyo amepongeza jitihada zinazofanywa na TANESCO ambapo amefafanua kuwa kukamilika kwa Mradi huo kutasaidia kumaliza  kero ya umeme katika maeneo mengi ya Mbagala, Temeke na Mkuranga.

“Kwa namna ya pekee tunaishukuru sana TANESCO kwa mradi huu, kwa awamu ya kwanza Mradi huu ulipaswa kujaribiwa mwezi Juni mwaka huu lakini Mradi umeweza kuonesha mafanikio kabla ya wakati kutokana na jitihada kubwa zinazofanywa’’ alifafanua Mhe. Mapunda

Uboreshaji wa Mradi huu wa Kituo cha Kupokea na Kupoza na Kusambaza umeme cha Mbagala umegharimu Dola za Kimarekani milioni 6.4 ambapo sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji wake na kukamilika kwake kunatarajia kusambaza umeme wa Megawati 165.



UWEKEZAJI WA NSSF MKULAZI WAONGEZA AJIRA KWA WANANCHI NA UZALISHAJI WA SUKARI

May 14, 2025 Add Comment


*Bodi ya Wadhamini ya NSSF yaridhishwa na uwekezaji huo wa ubia na Jeshi la Magereza


Na MWANDISHI WETU,

Morogoro. Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeendelea kudhihirisha mafanikio ya uwekezaji wake mkubwa katika sekta ya viwanda kupitia mradi wa kimkakati wa kiwanda cha sukari cha Mkulazi kilichoko mkoani Morogoro, ambacho kimeanza rasmi uzalisha Julai 2024, kimezalisha ajira kwa Watanzania na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii kwa Wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara ya Bodi ya Wadhamini ya NSSF,  Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Bi. Mwamini Malemi, alieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa kwa ubia kati ya NSSF na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri, hongereni sana. Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini tumejionea na tunathamini mnachokifanya,” alisema Bi. Mwamini mara baada ya kupokea taarifa ya Kiwanda kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Mkulazi (MHCL), Bw. Selestine Some.

Kwa upande wake, Bw. Masha Mshomba, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF alisema kupitia ziara hiyo ya kikazi, Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wameweza kushuhudia shughuli mbalimbali za uendeshaji wa mradi huo ulioanzishwa na Serikali kwa lengo la kupunguza nakisi ya sukari nchini.

Akisoma taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Mkulazi Bw. Some alisema katika msimu wa mwaka 2024/25, kampuni ilipanga kuzalisha tani 20,000 za sukari ya majumbani, ambapo hadi mwisho wa msimu kiasi cha tani 19,124 sawa na asilimia 96 kilizalishwa.

Alisema pia, katika msimu wa 2025/26, Kampuni itaanza pia kuzalisha sukari ya viwandani ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati wa uzinduzi wa kiwanda,uliofanyika tarehe 8 Agosti 2024.

Bw. Some alisema uzalishaji wa sukari ya viwandani utapunguza uagizwaji wa bidhaa hiyo nje ya Nchi.  

Alisema pia katika msimu wa uzalishaji wa sukari 2024/25 kiwanda kimetoa ajira za moja kwa moja kwa Watanzania 2,172 na zisizo za moja kwa moja 8,000, na kuongeza biashara, shughuli za kiuchumi na kipato kwa Wananchi wa Mji wa Dakawa, Dumila na vijiji jirani.

MWISHO