Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

KATIBU TAWALA MKOA WA KATAVI, AHITIMISHA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU KITAIFA (GAWE) 2025

May 14, 2025 Add Comment

 

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akisisitiza jambo kwenye kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Na Mwandishi Wetu, Katavi

MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET) kwa kushirikiana na wanachama wake, imekusanya nguvu ya pamoja na kujitolea kiasi cha shilingi milioni 35,000,000 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika Halmashauri ya Mpimbwe, mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliofanyika mkoani hapa.

Akizungumza katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro alisema wametoa fedha hiyo ili iweze kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu katika Mkoa wa Katavi.

Akifafanua zaidi Bw. Nanyaro alisema wameguswa na muitikio mkubwa wa wazazi/walezi, viongozi wa mila na dini katika shule walizozitembelea wakiwa katika ziara za maadhimisho kwani walijumuika pamoja kujadili mambo mbali mbali muhimu yanayohusu elimu, ikiwemo jitihada kubwa za walimu katika kuendelea kuwafundisha wanafunzi wengi licha ya changamoto zinazowakumba katika mazingira ya ufudishaji hali inayoonyesha kufanya kazi kwa bidii, kujitolea na dhamira ya kuinua kiwango cha Elimu nchini.

"Tumeshuhudia changamoto kadha wa kadha zinazozikabili shule zetu zinazohitaji kushughulikiwa ili kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji: ikiwemo upungufu na uchakavu wa miundombinu ya madarasa kwa baadhi ya shule, upungufu wa walimu, hasa wa kike, ukosefu nyumba za walimu, hasa katika baadhi ya shule, ukosefu wa mabweni kwa wanafunzi, hasa wanaotoka vijiji vya mbali, unaolazimu watoto kutembea hadi kilometa 12 kila siku Kwenda na kurudi shuleni jambo linalochangia utoro na wengine kuacha shule kabisa." Alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro.

Aidha wadau hao wa elimu walipendekeza msaada walioutoa kusaidia kutatua changamoto ya jumla ya madawati 407 meza 10 na viti 10 kwa mchanganuo ufuatao; Madawati 250 yaende shule ya Msingi Migunga, Madawati 47 yasaidie Shule ya Msingi Ikulwe, Madawati 110 yapelekwe katika Shule ya Msingi Minyoso na meza 10 na Viti 10 ziende kwa ajili ya walimu wa shule ya sekondari Mirumba.

Pamoja na hayo walipendekeza viongozi wa Serikali kuandaa mpango na kutenga bajeti ya ujenzi wa hostel za wanafunzi wa kike na wakiume, kujenga matundu ya vyoo, vyumba vya kujisitiri wanafuzi wa kike wakati wa hedhi na upatikanaji wa maji safi na salama; utakaoendana sambasamba na ujenzi wa madarasa ili kukidhi uhitaji uliopo kwa sasa ili kulinda afya na usalama wa Watoto.

Wada wa elimu tunashauri viongozi katika sekta ya elimu ngazi ya wilaya na mkoa kuandaa ziara za mara kwa mara kutembelea shuleni kukutana na wanafunzi, walimu, kamati za shule na wazazi/walezi kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wanafunzi na walimu shuleni.  

"...Tunawahimiza wazazi na walezi kuendelea kuchangia utoaji wa chakula na lishe shuleni ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni na kusoma bila njaa ili kuongeza ufaulu wao na kupunguza utoro shuleni. Kuzingatia sheria na Kanuni za utoaji wa adhabu kwa Wanfunzi kama ilivoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu No. 24 wa mwaka 2002, unaotoa mwongozo namna ya utolewaji wa adhabu ya viboko shuleni. ili kuepuka kutoa adhabu kali za viboko kwa wanafunzi shuleni," alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro akiwasilisha taarifa ya wadau wa elimu baada ya kilele cha maadhimisho.

Baadhi ya viongozi na wananchi wakiwa katika hafla ya  Maadhimisho ya kilele cha Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.

UPANUZI WA KITUO CHA KUPOZA UMEME MBAGALA MBIONI KUKAMILIKA

May 14, 2025 Add Comment

 



Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Lazaro Twange amesema wananchi wa maeneo ya Mbagala na viunga vyake sasa wanatarajia kupata umeme wa uhakika baada ya Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mbagala kuongezewa uwezo kutoka Megawati 45 za awali na kufikia Megawati 165.

Akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kutembelea Kituo hicho Bw. Twange alisema kuwa Kituo hicho kimeongezewa uwezo mara mbili ya awali hivyo kitakuwa na uwezo mkubwa wa kusambaza umeme na kuondoa kabisa changamoto ya kukatika kwa umeme katika maeneo hayo.

“Kituo hiki kimeongezewa uwezo mara mbili ya awali na mpaka sasa utekelezaji wa Mradi huu umefikia asilimia 70. Wananchi wa Mbagala na viunga vyake sasa wategemee umeme wa uhakika’’ alisisitiza Bw. Twange.

Pia, Mkurugenzi Mtendaji Bw. Lazaro amemshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa kiasi cha fedha Dola za Kimarekani milioni 6.4  ili kufanikisha Mradi huu wenye tija na manufaa kwa wananchi wa maeneo hayo na nchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sixtus  Mapunda, akizungumza wakati wa ziara hiyo amepongeza jitihada zinazofanywa na TANESCO ambapo amefafanua kuwa kukamilika kwa Mradi huo kutasaidia kumaliza  kero ya umeme katika maeneo mengi ya Mbagala, Temeke na Mkuranga.

“Kwa namna ya pekee tunaishukuru sana TANESCO kwa mradi huu, kwa awamu ya kwanza Mradi huu ulipaswa kujaribiwa mwezi Juni mwaka huu lakini Mradi umeweza kuonesha mafanikio kabla ya wakati kutokana na jitihada kubwa zinazofanywa’’ alifafanua Mhe. Mapunda

Uboreshaji wa Mradi huu wa Kituo cha Kupokea na Kupoza na Kusambaza umeme cha Mbagala umegharimu Dola za Kimarekani milioni 6.4 ambapo sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji wake na kukamilika kwake kunatarajia kusambaza umeme wa Megawati 165.



UWEKEZAJI WA NSSF MKULAZI WAONGEZA AJIRA KWA WANANCHI NA UZALISHAJI WA SUKARI

May 14, 2025 Add Comment


*Bodi ya Wadhamini ya NSSF yaridhishwa na uwekezaji huo wa ubia na Jeshi la Magereza


Na MWANDISHI WETU,

Morogoro. Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeendelea kudhihirisha mafanikio ya uwekezaji wake mkubwa katika sekta ya viwanda kupitia mradi wa kimkakati wa kiwanda cha sukari cha Mkulazi kilichoko mkoani Morogoro, ambacho kimeanza rasmi uzalisha Julai 2024, kimezalisha ajira kwa Watanzania na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii kwa Wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara ya Bodi ya Wadhamini ya NSSF,  Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Bi. Mwamini Malemi, alieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa kwa ubia kati ya NSSF na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri, hongereni sana. Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini tumejionea na tunathamini mnachokifanya,” alisema Bi. Mwamini mara baada ya kupokea taarifa ya Kiwanda kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Mkulazi (MHCL), Bw. Selestine Some.

Kwa upande wake, Bw. Masha Mshomba, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF alisema kupitia ziara hiyo ya kikazi, Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wameweza kushuhudia shughuli mbalimbali za uendeshaji wa mradi huo ulioanzishwa na Serikali kwa lengo la kupunguza nakisi ya sukari nchini.

Akisoma taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Mkulazi Bw. Some alisema katika msimu wa mwaka 2024/25, kampuni ilipanga kuzalisha tani 20,000 za sukari ya majumbani, ambapo hadi mwisho wa msimu kiasi cha tani 19,124 sawa na asilimia 96 kilizalishwa.

Alisema pia, katika msimu wa 2025/26, Kampuni itaanza pia kuzalisha sukari ya viwandani ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati wa uzinduzi wa kiwanda,uliofanyika tarehe 8 Agosti 2024.

Bw. Some alisema uzalishaji wa sukari ya viwandani utapunguza uagizwaji wa bidhaa hiyo nje ya Nchi.  

Alisema pia katika msimu wa uzalishaji wa sukari 2024/25 kiwanda kimetoa ajira za moja kwa moja kwa Watanzania 2,172 na zisizo za moja kwa moja 8,000, na kuongeza biashara, shughuli za kiuchumi na kipato kwa Wananchi wa Mji wa Dakawa, Dumila na vijiji jirani.

MWISHO

WAZIRI ULEGA AUNDA TIMU KUCHUNGUZA KIVUKO CHA MV TANGA

May 13, 2025 Add Comment

 



Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega ameunda timu ya wataalamu na kuipa siku saba kuchunguza changamoto zinazojitokeza mara kwa mara katika Kivuko cha MV TANGA kilichopo wilayani Pangani, mkoani Tanga baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu kusuasua kwa utendaji wake.

Pia, katika ziara yake mkoani Tanga, Ulega pia amemtaka mkandarasi aliyepewa kazi ya kujenga barabara ya Tanga - Pangani - Mkwaja - Bagamoyo (Makurunge) sehemu ya Tungamaa - Mkwaja – Mkange, kuilipa serikali fidia kutokana na uzembe uliofanya ujenzi usikamilike kwa wakati ilhali tayari serikali imetimiza upande wake wa mkataba ikiwamo kumlipa mkandarasi huyo.

Akizungumza kwa nyakati tofauti mkoani humo, Ulega alisema serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inafanya jitihada kubwa za ukarabati na ununuzi wa vivuko ili kurahisisha maisha ya wananchi na kwamba wananchi hawapaswi kupata shida wakati miundombinu ipo.

Kivuko aambacho kimeundiwa tume ni ya uchunguzi kinatoa huduma kati ya Pangani na Bweni na Ulega alisema lengo ni kuhakikisha kuwa kivuko hicho kinafanya kazi kwa wakati wote kama ilivyokusudiwa.

Naunda timu ya watu watatu, mmoja kutoka Ofisi ya Rais wa kutoka hapa na wawili Katibu Mkuu wa Ujenzi atawateua kutoka wizarani ili iniambie ni nini hasa kinaendelea hapa Pangani, haiwezi ikawa kila siku wananchi wanapata usumbufu”, amesisitiza Ulega.

Ulega amefanya maamuzi hayo kutokana na Kivuko hicho cha MV TANGA kushindwa kufanya kazi kwa siku nne huku watendaji na wasimamizi wakishindwa kufanya maamuzi ya haraka ya upatikanaji wa vipuri vya kufungwa katika kivuko hicho na kusisitiza kuwa endapo itabainika kuna hujuma zinafanyika katika kivuko hicho atachukua hatua za kinidhamu.

Akizungumza kabla ya Ulega, Mbunge wa Jimbo la Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso alimuomba waziri huyo kushughulikia changamoto ya usafiri wa Kivuko cha MV TANGA ambacho ni muhimu na msaada kwa wananchi wa Pangani.

Katika hatua nyingine, Waziri Ulega amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Pangani lenye urefu wa mita 525 na kuridhishwa na hatua zilizofikiwa.






MAWAZIRI WA SADC WAKUTANA KUJADILI USIMAMIZI WA MAAFA

May 13, 2025 Add Comment

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga, ameshiriki mkutano wa dharura wa Kamati ya Mawaziri wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa SADC, uliofanyika leo tarehe 13 Mei 2025 kwa njia ya mtandao.

Mkutano huo wa dharura umelenga kujadili hatua za kuimarisha mfumo wa usimamizi wa maafa na huduma za kibinadamu kwa nchi wanachama wa SADC.

Pia Mkutano huo umelenga kujadili hatua za kuimarisha usimamizi wa maafa na kuunga mkono ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na maafa na kuendelea kujenga usalama wa watu na mali, Aidha Waziri wa Serikali za Mitaa na Kazi za Umma wa Zimbabwe, Bw. Daniel Garwe, ameongoza mkutano huo kama Mwenyekiti.

Pamoja na hayo Mhe. Ummy Nderiananga ameutumia mkutano huo kutoa pongezi kwa Sekretarieti ya SADC kwa kuanzisha kituo cha huduma za kibinadamu na operesheni za dharura kilichopo Msumbiji, akisisitiza umuhimu wa kituo hicho katika kuimarisha ushirikiano na kukabiliana na maafa. Pia, amekubaliana na ongezeko la wataalamu 35 katika timu ya SADC ya utayari wa kukabiliana na dharura. 

Mkutano huu umeonesha mshikamano wa kikanda katika kuimarisha usalama na kukuza uchumi wa nchi za SADC kupitia usimamizi bora wa maafa.