KAMATI YA PIC YARIDHISHWA NA THAMANI YA FEDHA KATIKA MRADI WA MAJI SAME MWANGA KOROGWE.
habariNA WILLIUM PAUL, MWANGA.
WAJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imeridhishwa na ubora wa mradi wa maji Same Mwanga Korogwe ambao umegharimu zaidi ya Bilioni 400 na kudai kuwa thamani ya fedha inaonekana katika mradi huo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Augustine Vuma mara baada ya kutembelea mradi huo ambapo alisema kuwa, hali ya upatikanaji wa maji kwa sasa katika miji ya Mwanga na Same ni ya kuridhisha kwani wananchi wanapa maji kwa masaa 24.
“Kamati imeridhishwa na ubora wa mradi pamoja na upatikanaji wa maji kwa sasa hivyo kamati inaipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongpzwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kujenga mradi huo na zimetolewa kwa wakati” alisema Vuma.
Alisema kuwa, jukumu la sasa kwa Wizara ya maji kupitia mamlaka yake ya Mwanga Same ni kutunza mradi huo kwa kushirikiana na Wananchi ili uendelea kuwa bora na kudumu muda mrefu ili kuhakikisha kuwa wananchi hawarudi kule walipotokea kukosa maji au kupata kwa mgao.
Aidha wameiagiza mamlaka hiyokuhakikisha inatekeleza mpango wa usambazaji maji kikamilifu katika maeneo ya mamlaka ili kuwafikiwa wahitija na kutimiza adhima ya Serikali ya kuwafikia wananchi wengi huduma.
Alisema kuwa, mamlaka hiyo inatekeleza mpango wa ulinzi wa vyanzo vya maji na miundombinu yake pamoja na kuweka mpango wa muda mfupi na mrefu wa ukarabati wa miundombinu ya maji ili kuhakikisha mradi unaendeshwa kwa ufanisi na katika hali ya uendelevu ambapo jambo hilo litapelekea mradi huo kutoa tija.
“Mamlaka ya maji Same Mwanga hakikisheni mnaimarisha mkakati wenu wa ushirikiano wa kibiashara na wadau mbalimbali wakiwemo wateja wakubwa ili kuweza kuwafikia kihuduma jambo ambalo litawezesha kuongeza wigo wa kiwango cha ukusanyaji wa mapato pamoja na kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kulipia Ankara za maji kikamilifu na kwa wakati ili kuepuka changamoto za madeni ambayo imekuwa kikwazo kwa mamlaka nyingi nchini” alisema Vuma.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa mamlaka ya Maji Same Mwanga (SAMWASA), Mhandisi Rashid Mwinjuma alisema kuwa, kupitia mradi huo kwa sasa wananchi wa Mwanga na Same wanapata maji ya uhakika masaa 24, ambapo hali hiyo imesaidia mapato yameongezeka kutoka milioni 40 kwa mwezi hadi kufikia milioni 70.
Mhandisi Mwinjuma alisema kuwa, hata wateja wameongezeka kutoka 4000 hadi kufikia 6000 huku akidai kuwa mwamko wa wananchi kuomba kuunganishiwa huduma ya maji umekuwa mkubwa.
“Kwa sasa tunajukumu la kuendelea kusambaza mtandao wa maji ili kuwafikia wateja wengi ili kusaidia kukusanya fedha za kuweza kuendeshea mradi huu na kwa siku tumekuwa tukipokea wastani wa watu 50 wanaotaka kuunganishiwa na huduma ya maji lakini tumeendelea kutoa elimu ili watambue umuhimu wa kulipia Ankara zao kwa wakati” alisema Mhandisi Mwinjuma.
SimBanking kugawa milioni 240, magari matano kwa wateja wake
habariAkizindua kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul amesema kwa mwaka huu benki imejipanga kutoa magari manne aina ya Toyota IST na Toyota Harrier ‘New Model’ moja kwa wateja watakaoibuka kuwa vinara katika matumizi ya SimBanking katika kukamilisha miamala yao na huduma nyingine.
Katika kampeni ya mwaka huu ya SimBanking amesema kutakuwa na washindi wa kila siku na kila wiki watakaopata zawadi za fedha taslimu na gari aina ya Toyota IST na mshindi wa jumla ataondoka na Toyota Harrier.
“Tumetenga zaidi ya shilingi milion 240 zitakazotolewa kwa washindi wetu na kila baada ya miezi miwili tutatoa zawadi ya gari aina ya IST wakati mshindi wa jumla tutakayemtangaza mwishoni mwa mwaka atapata gari aina ya Toyota Harrier. Magari haya yote tutakayoyatoa kwa washindi wetu ni ‘New Model’ na yamekatiwa bima kubwa. Kwa wanafunzi wa vyuo, kuna simu za kisasa aina ya Iphone 16 zitakazokuwa zinatolewa kila baada ya miezi mitatu,” amesema Bonaventura.
Bonaventura amesema Benki ya CRDB inaamini katika kutoa huduma bora na za kisasa ili kuchangia maendeleo ya wateja wake na taifa hivyo kuhitaji kuwekeza katika ubunifu unaoendana na mabadiliko ya teknolojia duniani. Amesisitiza kuwa SimBanking ni kati ya huduma bora inayotambulika duniani kutokana na urahisi, usalama na uhakika wa kukamilisha miamala kidijitali.
“SimBanking ni kati ya huduma za Benki yetu ya CRDB ambazo zimeleta mapinduzi makubwa katika kuchochea ujumuishi wa huduma za fedha nchini. Kwa zaidi ya muongo mmoja sasa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2011, SimBanking imetoa fursa kwa Watanzania wengi kujiunga na mfumo rasmi wa huduma za benki.
TBS YASISITIZA UMUHIMU WA KUHAKIKI USAHIHI WA VIPIMO ( UGEZI ) WA VIFAA VYA HOSPITALI , KULINDA AFYA ZA WATANZANIA.
habariNa Mwandishi Wetu.
Machi 26 , 2025 Shirika la Viwango Tanzania ( TBS ) limewasihi Watumiaji mbalimbali wa Vifaa Tiba kuhakikisha wanapeleka Vifaa vyao TBS katika Maabara ya Taifa ya Ugezi ili kuhakiki Usahihi wa Vipimo wa Vifaa hivyo utakaowasaidia kuwa na uhakika wa majibu yanayotolewa na Vifaa hivyo suala litakalopelekea kujenga uaminifu na kulinda Afya za Wateja wanaowahudumia.

" Mfano katika Hospitali , Vifaa vinapokua vimefanyiwa Ugezi vitatoa majibu sahihi ya Vipimo ambayo yatamwezesha Daktari kujua mgonjwa ana tatizo gani na kuchukua hatua stahiki za kupambana na ugonjwa husika kwa haraka sana, *daktari hutoa matibabu kutegemea Majibu yaliyotoka maabara, hivyo kama maabara imefanyiwa ugezi daktari atatoa matibabu sahihi kwa mgonjwa na kumhakikishia usalama wake, hii pia itapunguza upotevu wa muda na fedha kwa kufanya ufuatiliaji wa matibabu sehemu nyingine ama kupewa dawa wakati hakuna ugonjwa. Kufanya ugezi kunachangia maendeleo katika Jamii " amesema Mahilla .
Kwa upande wake Bi. Clara Mwinami Afisa Vipimo TBS ametoa wito kwa Hospitali ambazo hazijafanya Ugezi wa Vifaa katika Maabara zao kufika TBS kwa maana Uhakiki wa Usahihi wa Vipimo wa Vifaa vyao utawasaidia kuaminika kwa Huduma wanazozitoa .

COSTECH WAKABIDHI RASMI ENEO LA MRADI KWA MKANDARASI KWA AJILI YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA STI JIJINI DODOMA
habari
TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imekabidhi rasmi eneo la mradi kwa mkandarasi TIL Construction Limited kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo jipya la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STI) jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kukabidhi eneo hilo la mradi Machi 25,2025 jijini Dodoma Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kutoka COSTECH, Dkt. Aloyce Andrew, amesema hatua hiyo inalenga kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau wa taasisi hiyo.
"COSTECH ina jengo Dar es Salaam lakini tumeamua kujenga Dodoma kwa ajili ya kuwahudumia wadau wetu kwa ukaribu zaidi...,Jengo hili litakuwa na sehemu ya kuhudumia wabunifu, kuatamia kampuni changa, na kuratibu masuala ya utafiti," amesema Dkt. Andrew.
Amesema ujenzi wa jengo hilo, ambalo litajengwa eneo la Azina jijini humo lenye mita za mraba 4,800, unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 12 kufuatia kusainiwa kwa mkataba Machi 24, 2025.
Kwa upande wake, Mshauri Elekezi wa mradi huo kutoka Kampuni ya MEKON, Benedict Martin, amesema wamekuwa wakihusika katika usanifu wa jengo hilo tangu mwaka jana (2024) baada ya kushinda zabuni kutoka COSTECH.
"Tulishirikiana na COSTECH kuhakikisha jengo hili linakidhi mahitaji yao yote. Pia tuna uhakika kwamba mkandarasi tuliyempata ana uwezo wa kutekeleza mradi huu kwa ubora unaotakiwa," alisema Martin.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa TIL Construction Limited, Ding Fubing, ameahidi kwamba kazi itafanyika kwa ufanisi na kumalizika kwa wakati.
"Tunaanza rasmi kesho kwa kulisafisha eneo lote, na baada ya wiki mbili hadi tatu, tutaingia kwenye ujenzi wenyewe. Tunaahidi kufanya kazi nzuri na kukamilisha mradi kwa muda uliopangwa au hata kabla," alisema Fubing.
Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa COSTECH, Imanuel Mgonja, amesema taasisi hiyo ina imani na mshauri elekezi pamoja na mkandarasi, akiwashukuru kwa kujitolea kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora unaohitajika..