TUME YA HAKI ZA BINADAMU YAENDESHA MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU NA WAJIBU WA ASKARI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

September 19, 2025



Tume ya Haki za Binadamu imeendesha mafunzo ya haki ya binadamu na wajibu wa Askari Polisi wakati wa uchaguzi kwa askari Polisi ngazi ya kata wilaya ya Tanga. 

Mafunzo hayo  yamefanyika katika Ukumbi wa mikutano wa jiji la Tanga leo Septemba19, 2025 ikiwa ni sehemu ya kuwakumbusha  askari hao  kuhusu umuhimu wa kufuata sheria, kanuni na misingi ya haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yao, hususan kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma, Mawasiliano, Utafiti na Nyaraka wa Tume ya Haki za Binadamu, Bi Monica Mnanka, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu,.

Amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwakumbusha  Askari Polisi umuhimu wa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia haki za binadamu ili kutoa fursa kwa wananchi kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.

Nao baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi mkoani Tanga waliopata nafasi ya kuhudhuria mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo  yatakuwa msaada mkubwa kwao katika kutoa elimu kwa wananchi kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi.




Tume ya Haki za Binadamu inaendelea na zoezi la kutoa mafunzo hayo kwa makundi mbalimbali, yakiwemo Jeshi la Polisi,pamoja na waandishi wa habari, Tanzania Bara na  Zanzibar.



Share this

Related Posts

Previous
Next Post »