Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga ameongoza wadau mbalimbali kujadili utekelezaji wa Mpango Mahsusi wa Nishati wa Misheni 300.
Mjadala huo umefanyika katika Wiki ya Nishati Jadidifu 2025 inayoendelea jijini Dar es Salaam.
Masuala mbalimbali yamejadiliwa ikiwemo namna ya kuvutia na kushirikisha wawekezaji kutoka sekta binafsi na taasisi za kifedha, ili kufikia malengo yaliyowekwa katika Mpango Mahsusi wa Nishati ikiwemo kuhakikisha asilimia 75 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2030.
EmoticonEmoticon