“COASTAL UNION KUANZA NA U-20”

April 21, 2018
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union “Wagosi wa Kaya”umesema utaanza na usajili wa timu ya vijana chini ya miaka ishirini U-20 wiki ijayo huku wakiendelea kusaka wachezaji watakaokitumikia kikosi hicho msimu mpya
wa Ligi kuu soka Tanzania bara.

Coastal Union ambayo imepanda msimu huu kucheza Ligi kuu baada ya kusota kwenye michuano ya Ligi Daraja kwanza kwa kipindi kirefu inakusudia kuweka mazingira mazuri ya kuwawezesha kucheza mashindano hayo kwa mafanikio.

Akizungumza jana,Mwenyekiti wa timu hiyo Steven Mguto alisema lengo la kuanza na kikosi hicho ni kuona namna ya kukiimarisha ili baadae watakaposaka hitajika kupandishwa kucheza kwenye timu ya wakubwa waweze kuchagua.

“Kama unavyojua timu zinazoshiriki michuano ya Ligi kuu zinapaswa pia kuwa na U-20 hivyo kwa kuliona hilo tunakusudia kuanza mchakato huu wiki ijayo kwani tunapokuwa na kikosi hicho baadae tutaekeleza nguvu
kwenye usajili wa watakaocheza timu ya wakubwa “Alisema.

Hata hivyo alisema hivi sasa wanasaka wafadhili ambao watawasaidia kwenye harakati zao za usajili na ushiriki wao kwenye michuano hiyo ya Ligi kuu kutokana na kikosi kutokuwa na fedha za kuwawezesha kufanya
mambo hayo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »