Waziri Makamba awasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Bishara na Mazingira

March 22, 2018
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Innocent Bashungwa akisisitiza jambo kwa watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais (hawapo pichani) mara baada ya kupokea taarifa ya Ofisi ya Makamu wa Rais na kujadili utelekezaji wa Bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka fedha 2017/2018 na mapendekezo ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19. Taarifa iliyowasilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. Kulia ni Katibu wa Kamati Bw. Wilfred Magova.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)Mhe. January Makamba, Naibu Waziri Mhe. Kangi Lugola na  Katibu Mkuu Mhandisi Joseph Malongo wakifuatilia majadiliano ya wajumbe wa kamati mara baada ya kuwasilisha taarifa yao kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, hii leo Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri  Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola, Katibu Mkuu Mhandisi Joseph Malongo na Naibu Katibu Mkuu Bi. Butamo Phillip wakifuatilia majadiliano ya wajumbe wa kamati mara baada ya kuwasilisha taarifa yao kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda Biashara na Mazingira, hii leo Mjini Dodoma.

Pichani wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda Biashara na Mazingira Mhe. Hawa Subira Mwaifunga na Mhe. Omary Ahmed Badwel wakifuatilia majadiliano katika Kamati yao hii leo Mjini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda Biashara na Mazingira Mhe. Kanali (Mst) Masoud Ali Khamis na Mhe. Zainab Mdolwa Amiri wakifuatilia majadiliano kikaoni hapo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba
#Kwa kiasi kikubwa kiwango cha uelewa kwa wananchi na jamii kwa ujumla juu ya masuala ya mazingira kimeongezeka na Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kutoa elimu kwa Umma na suala hili litapewa kipaumbele
#Ofisi ya Makamu wa Rais inashirikiana na wadau mbalimbali katika kuhamasisha uwekezaji endelevu na rafiki kwa mazingira.
#Matumizi ya nishati mmbada wa mkaa yanaendea kuhimizwa ikiwa ni pamoja na matumizi ya gesi na matumizi ya majiko banifu na matumizi ya tungamotaka (Bio-Mass).
#Zaidi ya Maafisa Mazingira mia tano (500) wameteuliwa kwa ajili ya kuwa ’wakaguzi wa Mazingira’ambao watafanya kazi kwa mujibu wa sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 kifungu namba 182 (2)
#Serikali inaendelea kujenga uwezo wa Taasisi ikiwemo NEMC ili iweze kutimiza majukumu yake ipasavyo kwa mujibu wa Sheria.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola
#Serikali imeanzisha Mfuko wa Mazingira ambao pamoja na mambo mengine fedha yake itasaidia kampeni kubwa ya upandaji miti hapa nchini
#Taasisi/Vikundi vinavyojihusisha na masuala ya hifadhi na usimamizi wa mazingira nchini vinaweza kupewa tuzo ili kutoa chachu kwa vikundi vingine pia
#Kila Wilaya na Halmashauri zinatakiwa kuanzisha Sheria ndogo ndogo kwa ajili ya Hifadhi na usimamizi wa Mazingira katika maeneo yao.
#Serikali imeanza mchakato wa kuandaa orodha ya wachimbaji wadogo wadogo wote hapa nchini ili uandaliwe utaratibu maalumu wa kuwaratibu kwa ujumla wao.


Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Innocent Bashungwa
#Kampeni za kitaifa za Mazingira zinaonekana na vema juhudi hizi ziendelee kwa kushirikisha wadau wote
#Serikali iangalie upya matumizi ya Mkaa wa kuja na nishati mbadala ili kunusuru ukataji wa miti unaoendelea kwa kasi, ikiwa ni pamoja na kushirikiana na SIDO katika kutengeneza majiko banifu
#Usimamizi wa Sheria ya Mazingira uzingatiwe ikiwa ni pamoja na kuitaka Migodi mikubwa kufuata taka la kisheria la kurudhisha hali ya mazingira ya awali mara baada ya kukamilika kwa uchimbaji.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »