Kampuni 3 Kuuza Tanzanite katika Mnada Wa Mirerani

December 20, 2017
Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila( katikati) akielezwa jambo na Vikosi vya ulinzi na usalama, katika eneo linalotumika kufanyia mnada wa Madini ya Tanzanite katika eneo la Naisinyai lililoko kwenye mji mdogo wa Mirerani.
Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila( katikati) akiangalia mapambo na vitu mbalimbali vinavyotengezwa na Kituo cha Uongezaji thamani Madini ya vito na Miamba( TGC),kilichopo mkoani Arusha, wakati Mnada wa Madini ya Tanzanite unaofanyika katika Mji mdogo wa Mirerani mkoani Manyara.
Wanunuzi kutoka mataifa mbalimbali wakifanya uthamini wa Madini ya Tanzanite kabla ya mnada kufanyika katika eneo la Naisinyai lililoko kwenye mji mdogo wa Mirerani.
Vifaa maalum( drum) vilivyohifadhia madini ya Tanzanite.
Madini ya Tanzanite yakipimwa kabla ya kuanza kufanyiwa mnada.
Mjiolojia Ester Njiwa wa Kituo cha Jemolojia Tanzania( TGC)akionenya vitu Mbalimbali vinavyotengenezwa na kituo hicho, wakati mnada wa Madini ya Tanzanite utakaofanyika katika mji mdogo wa Mirerani.
Usajili wa washiriki wa Mnada wa Madini ya Tanzanite ukiendelea katika mji mdogo wa Mirerani mkoani Manyara.
Ukaguzi ukiendelea kwa wanunuzi wanaofika katika eneo linalofanyika mnada wa Madini ya Tanzanite katika Mji mdogo wa Mirerani.




Na Zuena Msuya, Manyara.

Kampuni tatu za uchimbaji madini ya Tanzanite zimejitokeza kuuza madini hayo katika mnada wa tatu wa madini ya Tanzanite unaofanyika katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.

Mshindi wa mnada huo atatangazwa Desemba 21 katika eneo la Naisinyai lililoko kwenye mji mdogo wa Mirerani.

Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka amezitaja kampuni hizo kuwa ni Tanzaniteone yenye ubia na Shirika la Madini Tanzania( STAMICO), Tanzanite Afrika na Classic Gems.

Akizungumzia mnada huo, Kamishna Mchwampaka alisema kuwa utaratibu wa kufanya Mnada wa Tanzanite ni jitihada za Serikali za kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo nje nchi na pia kuwasaidia wachimbaji na wafanyabiashara wazalendo kuuza madini yao kwa bei ya ushindani inayoendana na soko la dunia.

Mchwampaka alifafanua kuwa, mnunuzi atakayefanikiwa kununua madini katika mnada huo ni yule tu atakayetoa bei ya juu ambayo imefikia au kuvuka bei inayotokana na Wathamini wa Serikali (Reserve Price).

Aliweka wazi kuwa zoezi hilo linafanyika kwa njia ya uwazi ambapo wanunuzi wa ndani na nje wanapata fursa ya kutazama madini na hatimaye kupata nafasi ya kutayarisha bei zao kwa siri ambazo zitatumbukizwa kwenye sanduku la Zabuni. Aidha, viongozi wa Wizara ya Madini, Wizara ya Fedha, Viongozi wa Mkoa wa Manyara, TRA na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vya mkoa wa Manyara wanashirikiana kwa pamoja kuhakikisha kuwa mnada huo unafanyika kwa ufanisi.

Aidha, mnada huo utaiwezesha Serikali kupata mrabaha stahiki na kodi nyingine ikiwa ni pamoja na tozo ya Halmashauri ya wilaya ya Simanjiro.

Hadi kufikia Desemba, 19,2017, zaidi ya wanunuzi 55 tayari wamejaza fomu za kuwawezesha kushindana kwenye zabuni za kununua madini hayo,wakiwepo watanzania 39 na wanunuzi 16 kutoka nje ya Tanzania

Kamishna Mchwampaka alisema kuwa minada kama hiyo pia hufanyika kwa nchi za Afrika zenye madini ya Vito kama vile Zambia( emerald), Zimbabwe ( Almasi) pamoja na Afrika kusini ( Almasi).

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »