Waziri Mkuu
Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga amemtembelea Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyopo mapumzikoni
katika Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.
Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga amemtembelea Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyopo mapumzikoni
katika Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.
Mheshimiwa Odinga
ambaye ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie Raila Odinga,
wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari ya Chato leo tarehe 02
April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye kuelekea nyumbani kwa Rais
Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao Rais Magufuli mwenyewe na Mkewe
Mama Janeth Magufuli.
ambaye ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie Raila Odinga,
wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari ya Chato leo tarehe 02
April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye kuelekea nyumbani kwa Rais
Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao Rais Magufuli mwenyewe na Mkewe
Mama Janeth Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akimkaribisha Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga nyumbani kwake Chato mkoani Geita mara baada ya Kuwasili. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikumbatiana na Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Chato Mkoani Geita. |
Akizungumza
mara baada ya kuwasili Chato, Mheshimiwa Raila Odinga amesema yeye na
familia yake wapo likizo na wamekuja kumtembelea rafiki wa familia yao,
kwa lengo la kumsalimia.
“Nimekuja
kupumzika na nimekuja na Mama na Mtoto wangu wa kike, na vilevile kuja
kutoa pongezi kwa ndugu yangu kwani tangu achaguliwe sijakuja hapa
Chato, na nilisema siendi Dar es salaam nitakuja hapahapa Chato” Alisema Mheshimiwa Odinga.
Pamoja
na kukutana na Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu
Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Raila Odinga pia amemsalimu Mama wa Rais
Bibi Suzana Joseph Magufuli na pia amezulu Makaburi walimozikwa
wanafamilia wa Rais, akiwemo Baba Mzazi Mzee Joseph Magufuli.
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili Chato. |
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na
mama mzazi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bi Suzana Joseph Magufuli mara baada ya kuwasili Chato Mkoani Geita. |
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya
Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga amemtembelea Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyepo mapumzikoni katika
Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.
Mheshimiwa Odinga ambaye
ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie Raila Odinga,
wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari ya Chato leo
tarehe 02 April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye kuelekea
nyumbani kwa Rais Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao Rais
Magufuli mwenyewe na Mkewe Mama Janeth Magufuli.
Akizungumza mara baada ya
kuwasili Chato, Mheshimiwa Raila Odinga amesema yeye na familia yake
wapo likizo na wamekuja kumtembelea rafiki wa familia yao, kwa lengo la
kumsalimia.
“Nimekuja kupumzika na
nimekuja na Mama na Mtoto wangu wa kike, na vilevile kuja kutoa pongezi
kwa ndugu yangu kwani tangu achaguliwe sijakuja hapa Chato, na nilisema
siendi Dar es salaam nitakuja hapahapa Chato” Alisema Mheshimiwa Odinga.
Pamoja na kukutana na Rais
Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya
Mheshimiwa Raila Odinga pia amemsalimu Mama Mzazi wa Rais Bibi Suzana
Joseph Magufuli na pia amezulu Makaburi walimozikwa wanafamilia wa Rais,
akiwemo Baba Mzazi Mzee Joseph Magufuli.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato
02 April, 2016