Naibu
Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji, Mwenyekiti wa Maendeleo
Benki, Amulike Ngeliama (kushoto) na Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na
Mipango wa(CMSA) Nicodemus Mukama wakifuatilia jambo katika hafla hiyo.
Naibu
Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji akipiga kengele kuashiria
uorodheshwaji rasmi wa Maendeleo Benki katika soko la hisa DSE jana.
Kushoto ni Mwenyekiti wa Maendeleo Benki, Amulike Ngeliama na Mkurugenzi
wa Capital Markets na Securities Authoriy (CMSA) Nicodemus Mukama
Emmanuel Nyalali, Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji DSE akizungumza katika hafla hiyo.
Naibu
Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji akiongea wakati wa hafla
ya kuorodheshwa kwa Maendeleo Benki katika soko la hisa DSE
Mkurugenzi
mtendaji wa Maendeleo Benki, Ibrahim Mwangalaba akitoa hotuba yake
kabla ya kumkaribisah Mwenyekiti wa Benki hiyo kuzungumza na washiriki
wa hafla hiyo.
……………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
Bank
PLC ni benki iliyoanzishwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania,
Dayosisi ya Mashariki na Pwani na inamilikiwa na Wananchi mbalimbali
kwa njia ya HISA bila kujali, kabila, itikadi, dini wala rangi, kwani
benki hii imesajiliwa na soko la hisa la Dar es Salaam (DSE), kupitia
dirisha dogo yaani Enterprise Growth Market (EGM) na inaendeshwa kwa
kufuata taratibu zote za BOT na Soko la Hisa la Dar es S alaam.
Maendeleo Bank ilianza kutoa huduma za kibenki tarehe 9/9/2013 baada ya
kupewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania na tarehe 05/11/2013 ilisajiliwa
rasmi katika soko la hisa la Dar es Salaam baada ya kukidhi vigezo vyote
vilivyowekwa na mamlaka husika. Benki hii ilianza na mtaji wa shilingi
bilioni 4.5 kutoka kwa wanahisa zaidi ya 3,000 wa rika na itikadi
mbalimbali walionunua wakati wa mauzo ya awali (IPO) yaliyofanyika mwaka
2013.
Tarehe
9/11/2015 benki ilipata kibali cha kuuza hisa stahili ambapo matarajio
yake yalikuwa kupata shilingi bilioni 3.06 ambazo zitatumika kuimarisha
shughuli za uendeshaji wa benki pamoja na kuongeza matawi. Katika zoezi
la uuzaji wa hisa stahili benki imeweza kupata jumla ya shilingi bilioni
2.8 na kufikisha jumla ya mtaji wa benki kuwa shilingi bilioni 7.3.
Kusudi
kubwa la kuanzishwa kwa Maendeleo Bank PLC ni kufikisha huduma za
kibenki kwa wananchi wa kipato cha chini na cha kati kwani hao ndio
walio wengi na upatikanaji wa huduma za kibenki kwao ni changamoto
kubwa. Benki hii imepata mafanikio mengi tangia kuanzishwa kwake
takribani miaka miwili iliyopita ambapo mpaka tarehe 31/12/2015, benki
imefikisha wateja zaidi ya 12,000, amana zaidi ya shilingi bilioni 46.0,
mali za benki zimefikia zaidi ya shilingi bilioni 55, imetoa mikopo
zaidi ya shilini bilioni 21.0 na mwaka 2015 imepata faida ya takribani
shilingi milioni 200.0 baada ya kodi.
Benki
hii inatoa huduma mbalimbali za ubunifu ambazo zinawalenga wananchi wa
kada mbalimbali, zikiwemo: huduma za kibenki kwa njia ya simu, huduma za
BIMA, ATM kupitia mtandao wa UMOJA Switch, akaunti mbalimbali zenye
gharama rafiki, kutuma na kupokea pesa kutoka nje na ndani ya nchi, na
kutoa mikopo ya aina mbalimbali, ikiwemo kwa wajasiliamali wadogo ambayo
haina dhamana, yaani mikopo ya vikundi.
EmoticonEmoticon