Dr.
Servacius Likwelile Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa
serikali wa katikati akiwa pamoja na Gavana wa Benki kuu ya Tanzania
Prof. Benno Ndulu kushoto na Bi. Natujwa Mwamba Naibu Gavana wa Benki
kuu ya Tanzania kulia, wakiwa katika mkutano wa chombo kinachotoa
mafunzo ya kusimamia mambo ya uchumi (MEFMI) nchini Peru – Lima.
Picha na Eva Valerian
…………………………………………………………………………………………….
Mikutano ya mwaka ya Bodi ya
Magavana ya Shirika la fedha la Kimataifa na kundi la Benki ya Dunia kwa
mwaka 2015 imeanza rasmi hapa mjini Lima –Peru na kuhudhuriwa na maelfu
ya watu kutoka nchi mbalimbali Duniani ambapo kilele chake kitakuwa
tarehe 12 mwezi Octoba 2015.
Bodi ya Magavana wa Shirika la
Fedha la kimataifa ( Mfuko) na Bodi ya Magavana wa kundi la Benki (
Benki ) kwa kawaida hukutana mara moja kwa mwaka kujadili kazi za
Taasisi ambazo ziko chini yao. Mikutano hii ya mwaka huwa inafanyika
mwishoni mwa mwezi Septemba na mwanzoni mwa mwezi Octoba. Mikutano hii
hufanyika mjini Washington kwa miaka miwili mfululizo na kwa mwaka wa
tatu hufanyika kwa nchi mwanachama ambaye amepitishwa kutokanana na
viwango vilivyowekwa.
Mikutano hii ya Bodi ya Magavana
ilizinduliwa huko Savannah, Georgia, Amerika mwaka 1946 na ikaanza
kufanyika mjini Washington DC mwaka huo huo.
Mikutano hii ya mwaka itaambatana
pamoja na mikutano ya kimataifa ya kifedha, kamati za fedha, Kamati za
maendeleo, kundi la nchi kumi, kundi la nchi ishirini na nne, na makundi
mbalimbali ya nchi wanachama.
Aidha katika kuhitimisha mikutano
hii, Shirika la fedha la kimataifa, kamati ya mambo ya fedha, Kamati ya
maendeleo pamoja na makundi mengine watapata nafasi ya kuwasiliana na
kutoa mapendekezo yao ya kipi kifanyike ili kuhakikisha mambo
wanayojipangia yanatekelezwa.
Magavana watakitumia kipindi hiki kwa kuzungumzia masuala ya kibiashara na
kushauriana. Bodi ya Magavana inatumia kipindi hiki kufanya
maamuzi ya ni vipi mambo ya Fedha ya kimataifa yanapaswa kuwa na
kukubaliana kuhusu maazimio yao.
Mikutano ya mwaka inakuwa na
mwenyekiti ambaye ni Gavana wa Benki na wa Mfuko, na uenyekiti huo
unakuwa ni wa kupokezana kati ya wanachama kila mwaka. Kila baada ya
miaka miwili inachagua Mkurugenzi mtendaji. Kila mwaka wanachama wapya
wowote wanakaribishwa katika Benki na mfuko.
Kwa sababu Mikutano hii ya mwaka inakusanya idadi kubwa ya wanachama kutoka
nchi mbalimbali, Shirika la fedha la kimataifa na kundi la Benki
ya Dunia inatoa nafasi ya kuwapatia ushauri mkubwa na mdogo, kwa
mpangilio wa kuwa na utaratibu maalumu au kutokuwa na utaratibu maalumu
alimradi hawavurugi mpangilio uliopo.
Semina mbali mbali zinafanyika na
zinaendeshwa na wafanyakazi wanachama kwa waandishi wa habari. Aidha
programu za Mikutano ya mwaka zimetengenezwa kwa kuzingatia matakwa ya
sekta binafsi, wajumbe kutoka Serikalini na maafisa wakuu wa Mabenki na
watumishi wa Mfuko.
Mikutano ya mwaka iliyofanyika nje ya Amerika kuanzia mwaka 1947 hadi 2015.
Mwaka Mahali
1947 London
1950 Paris
1952 Mexico City
1955 Istanbul
1958 New Delhi
1961 Vienna
1964 Tokyo
1967 Rio de Janeiro
1970 Copenhagen
1973 Nairobi
1976 Manila
1979 Belgrade
1982 Toronto
1985 Seoul
1988 Berlin
1991 Bangkok
1994 Madrid
1997 Hong Kong
2000 Prague
2003 Dubai
2006 Singapore
2009 Istanbul
2012 Tokyo
2015 Lima
Magavana wa mikutano hiyo ni
Mawaziri wa fedha kutoka nchi mbalimbali, Magavana wa Benki kuu na
Makatibu wakuu wa Wizara za fedha.
Mpaka sasa karibu nchi zote zimeshawasili katika mikutano hiyo na hali ya hewa ni mawingu na baridi kiasi.
Imetolewa na: Ingiahedi Mduma
Msemaji Mkuu
Wizara ya Fedha
Lima – Peru