Mwili
wa Marehemu, Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa ukiwa
umebebwa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza tayari kwa zoezi la
kuagwa Kijeshi katika Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es
Salaam.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa heshima za
mwisho kwa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa
ambaye ameagwa leo Kijeshi Juni 04, 2015 katika Chuo cha Maafisa
Magereza Ukonga Jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwa mazishi
kwao Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akiwa amesimama wakati
mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa
ulipokuwa ukiwasili katika Viwanja vya Chuo Cha Maafisa Magereza
Ukonga(katikati) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias
Chikawe(kulia) ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu.
Kiongozi
Mwakilishi wa Wastaafu wa Jeshi la Magereza, Naibu Kamishna Mstaafu wa
Magereza, John Nyoka akitoa salaam za rambirambi.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akisaini katika Kitabu
cha Maombolezo kabla ya kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu wa
Magereza Mstaafu Onel Malisa.
Gadi
Maalum ya Maafisa wa Jeshi la Magereza kwa ajili ya paredi la kuuaga
mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Jeshi la Magereza, Onel
Malisa.
Baadhi
ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini
salaam mbalimbali za rambirambi zilizokuwa zikitolewa katika hafla ya
kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu, Onel Malisa.
Umati wa ndugu na Jamaa waliojitokeza kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa.