|
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Meru,Dastan Malya akiwa na watendaji wengine wa serikali katika ofisi
ya mtendaji wa kata ya Siela Sing’isi
wakati mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassar alipofika
kwa ajili ya kwenda kutembelea Shamba la
Madiira. |
|
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua
Nassar akitia saini katika kitabu cha wageni katika ofisi ya kata ya
Siela Sing'isi alipotembelea katika kijiji hicho cha
Sing'isi. |
|
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua
Nassar akiongozana na Diwani wa kata ya Mbunguni Paul Laizer maarufu
kama Askofu (shoto) wakati alipowaongoza wakazi wa vijiji vya Sing'isi
na Malala kwenda kuangalia shamba la Madiira ambalo hekari 92
zimetolewa kwa vijiji hivyo. |
|
Wananchi wa vijiji vya Sing'isi na Malala
wakitizama sehemu ya eneo la Shamba la Madiira lililotolewa kwa
wananchi wa vijiji hivyo. |
|
Mpima wa Halmashauri ya wilaya ya Meru
,Seveline Luambano akiwaonesha wananchi wa vijiji vya Sing'isi na
Malala,mipaka pamoja na michoro ya ramani ya eneo la hekari 92
zilizotolewa kwa vijiji hivyo .zoezi hilo limeshuhudiwa na Mbunge wa
jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassar. |
|
Wananchi wakiwa katika Shamba la Madiira
kutizama mipaka ya eneo ambalo limetolewa kwao. |
|
Sehemu ya Shamba la
Madiira. |
|
Mbunge Nassari akiwaongoza wananchi wa
vijiji vya Sing'isi na Madiira wakitembelea shamaba la Madiira
kutizama mipaka ya eneo la Hekari 92 lililotolewa
kwao. |
|
Mbunge Nassari akimsikiliza Mwenyekiti wa
kijiji cha Sing'isi Elishiria Kimoto akitoa maelezo ya
kusitishwa kwa zoezi la kuoneshwa eneo hilo hadi pale Maofisa Ardhi wa
Halamashauri hiyo watakapo weka mionundo mbuni ya barabara katika eneo
hilo. |
|
Mbunge Nasari akizungumza na wananchi wa
vijiji hivyo mara baada ya kutembelea maeneo kadhaa ya eneo la Shamba
la Madiira ambao aliwataka kusitisha kilimo ili kuruhusu maofisa Ardhi
kupitishwa greda kwa ajili ya kuchonga barabara pamoja na mitaa katika
eneo hilo. |
|
Wananchi wakiwa katika kikao cha
pamoja. |
Na Dixon Busagaga wa Globu
ya Jamii
Kanda ya Kaskazini.
Share this