JAJA AMFUNIKA COUTINHO, AIFUNGIA YANGA IKIICHAPA THIKA UNITED 1-0

September 03, 2014
Sehemu ya mashabiki waliohudhuria mechi ya leo. (Picha na Frank Momanyi)

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MBRAZIL Geilson Santos Santana ‘Jaja’ kwa mara ya kwanza akicheza katika uwanja wa kisasa wa Taifa jijini Dar es salaam amefanikiwa kuifungia Yanga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Thika United ya Kenya.
Katika mechi hii iliyoanza saa 11:00 jioni, Jaja aliandika bao hilo katika dakika ya 60 ya mchezo.
Jaja ameweza kumfunika Mbrazil mwenzake, Andrey Coutinho aliyoonekana kuwa moto wa kuotea mbali katika mechi tatu zilizopita.
Coutinho aliifungia Yanga mabao 2 katika mechi tatu alizocheza Zanzibar wakati Jaja alifunga moja dhidi ya Chipukizi FC uwanja wa Gombani Pemba.
Cuutinho aliitungua Shangani na KMKM, Yanga ikishindi mabao 2-0 kwa kila mechi.
Lakini leo Jaja alitulia na kumzidi kete Coutinho aliyetarajia kuwavutia mashabiki wengi wa Yanga.
Maximo aliwaanzisha pamoja Jaja, Saimon Msuva na Coutinho katika safu ya ushambuliaji, wakati Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite walianza katikati.
Winga ya kulia alianza Hassan Dilunga. Safu ya ulinzi walianza Juma Abdul, kulia, Oscar Joshua, kushoto na mabeki wa kati walianza Nadir Haroub na Kelvin Yondani.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »