WACHEZAJI
waliosajili na timu ya Coastal Union ya Tanga,Uhuru Seleman na Haruna
Moshi "Boban"jana walikuwa kivutio kikubwa kwenye mazoezi
ya timu hiyo yaliyofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.
Baada
ya wachezaji hao kutua uwanjani hapo mashabiki wa soka mkoani hapa
walianza kuingia kwa wingi huku wakiwa makini kuangalia aina ya uchezaji
wao huku wengine wakiwashangilia mara kwa mara waliokuwa wakigusa
mipira.
Akizungumza
mara baada ya kumalizika mazoezi hayo,Uhuru alisema lengo la kuichezea
klabu hiyo ni kuipa ushindi timu hiyo na pamoja na kuisapoti timu hizo
ifikie malengo yake iliyojiwekea kwa siku zijazo.
Uhuru
alisema endapo wachezaji wanzie
wataunganisha nguvu ya pamoja itasaidia timu hiyo kufikia malengo yake
ya kuuutwaa ubingwa wa ligi kuu kwani hilo linawezekana iwapo mshikamano
baina ya wachezaji utakuwepo.
"Ninaamini
Coastal Union ni sehemu nzuri ya kuirudisha nafasi yangu kwenye timu ya
Taifa ya Tanzania (Taifa Stars)kwa sababu niliwahi kuchaguliwa
kuichezea timu ya Taifa nikitokea Coastal Union "Alisema Uhuru.
Kwa upande wake,Kocha Mkuu wa timu hiyo,Hemed Morroco aliwataka wachezaji ambao hawajawasili kwenye mazoezi kuwasili ili kuweza kuunganisha nguvu za pamoja kufanya maandalizi kabla ya kuanza msimu mpya wa Ligi kuu Tanzania bara.
Kwa upande wake,Kocha Mkuu wa timu hiyo,Hemed Morroco aliwataka wachezaji ambao hawajawasili kwenye mazoezi kuwasili ili kuweza kuunganisha nguvu za pamoja kufanya maandalizi kabla ya kuanza msimu mpya wa Ligi kuu Tanzania bara.
Mwisho.


EmoticonEmoticon