WIZARA YA NISHATI ENDELEENI KUWEZESHA UWEKEZAJI WA VITUO VYA MAFUTA VIJIJINI-WAZIRI SIMBACHAWENE

June 17, 2025 Add Comment


📌 *Atembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma*


DODOMA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene ameiasa Wizara ya Nishati kuendelea kuweka mazingira wezeshi yatakayowezesha uwekezaji zaidi wa vituo vya mafuta vijijini.


 Simbachaene amesema hayo tarehe 17 Juni, 2025, jijini Dodoma wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali ambayo leo yamefunguliwa rasmi

" Wafanyabiashara wengi wanataka kuwekeza kwenye vituo vya Mafuta vijijini kwakuwa bado  kuna uhaba wa vituo, hivyo angalieni masharti yanayowekwa kwenye uwekezaji yasiwe kikwazo kwenye huduma hii muhimu." Amesema Simbachawene

Pia, Simbachawene  ameishauri Wizara kuongeza kasi ya upatikanaji  wa Nishati Safi ya Kupikia Vijijini pamoja na kuhamasisha uwekezaji kwenye Nishati Safi ya Kupikia.


Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati na  Taasisi zake kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuendelea kutoa huduma za Nishati kwa wananchi.

TANAPA KUNADI MAENEO YAKE YA UWEKEZAJI KATIKA MKUTANO WA UWEKEZAJI ZANZIBAR

June 17, 2025 Add Comment



Na. Mwandishi wetu Zanzibar.

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limekuwa miongoni mwa wadau wakuu wanaoshiriki kunadi fursa za uwekezaji zinazopatikana katika Hifadhi za Taifa 21 kwenye Mkutano wa Uwekezaji Zanzibar (Zanzibar Investment Summit 2025), uliofanyika kwa mara ya kwanza Kisiwani Pemba huku ukifunguliwa rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Mhe. Dkt. Mwinyi alisisitiza umuhimu wa kutumia mkutano huo kama jukwaa la kutangaza fursa za kiuchumi zilizopo Zanzibar hususan kisiwani Pemba na maeneo mengine ya Tanganyika hasa maeneo ya Hifadhi za Taifa. 


Aidha, alitilia mkazo zaidi kwa wawekezaji wa ndani na nje kuchangamkia mazingira bora ya uwekezaji yaliyowekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya kuvutia wawekezaji wengi zaidi.

Katika Mkutano huo ulioanza June 15, 2025 TANAPA ilijikita kutangaza fursa za uwekezeji katika mazao ya utalii pamoja na miundombinu ya malazi kwa watalii wanaotembelea vivutio hivyo vilivyosheheni aina mbalimbali ya wanyama, mimea na mandhali za kuvutia zenye uoto wa asili ikijumuisha mabonde, milima na mito.


Mbali na kunadi fursa za uwekezaji pia, Wahifadhi hao walihamasisha watanzania na wawekezaji mbalimbali waliohudhulia mkutano huo kutembelea Hifadha za Taifa mbalimbali kutokana na upekee wa kila hifadhi ili wawe mabalozi wazuri wa kuzinadi hifadhi hizo warudipo nchini kwao na kuongeza kasi ya ujio wa watalii ili kukuza pato la Taifa.

Mkutano huo unaotarajiwa kutamatika leo June 17, 2025 ukibeba kauli mbinu isemayo; *“Ni Wakati wa Pemba”* pia unawajumuisha wadau kutoka sekta za utalii, kilimo, uchumi wa buluu, miundombinu, na biashara kutoka mataifa mbalimbali.

OCTOBA KURA ZOTE KWA RAIS DKT SAMIA- UMMY MWALIMU

June 17, 2025 Add Comment


Na Mwandishi Wetu, TANGA


Kazi nzuri na miradi tele ya maendeleo iliyotekelezwa katika Jimbo la Tanga Mjini imetengeneza deni kwa wananchi wa Tanga Mjini dhidi ya Rais Dk. Samia Suluhu ambaye pia ni Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba, 2025.


Hayo yameelezwa na Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM), Ummy Mwalimu, Juni 16, 2025, alipokuwa akitoa hotuba fupi kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Tanga Mjini katika Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Tanga. Katika hotuba yake, Ummy Mwalimu amesema Jimbo la Tanga Mjini limepata miradi mingi na mikubwa ya maendeleo ambayo imetatua kero za wananchi. 


Kwa msingi huo, Ummy Mwalimu amemuhakikishia Rais Dk. Samia kuwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu, asiwe na wasiwasi wa kura kwani wananchi wa Tanga Mjini watampa asante yao kwa njia ya kumpigia kura nyingi za kishindo ili aendelee kukaa Ikulu awatumikie Watanzania.


"Kwa kazi nzuri zilizofanyika, sisi watu wa Tanga kwakweli hatuna deni na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, na Oktoba 2025, watu wa Tanga tutamlipa Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kumrejesha Ikulu," amesema Ummy Mwalimu.


Mwenge wa Uhuru wilayani Tanga umezindua miradi mbalimbali ya maendeleo ikijumuisha miradi ya afya, maji, elimu, viwanda na utawala ambapo wananchi wamepongeza miradi hiyo iliyozinduliwa kwani imegusa ustawi na maendeleo yao.

WIZARA YA NISHATI KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA

June 17, 2025 Add Comment

Matukio mbalimbali wakati Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Wizara ya Nishati, Ziana Mlawa alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma

#NishatiTupoKazini

SERIKALI MKOA WA KILIMANJARO KUENDELEA KUPIGA UKATILI DHIDI YA WATOTO

June 17, 2025 Add Comment

 



Na Ashrack Miraji 

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw.Kiseo Nzowa  ametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto.

Bw. Nzowa alitoa kauli hiyo leo Juni 16,2025 wakati wa maadhimisho ya kilele cha Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Manispaa ya Moshi, ambapo aliwataka wazazi na walezi kutoa taarifa za matukio ya ukatili dhidi ya watoto mara yanapotokea ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa wakati.

Kwa upande wake, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa, Bi. Pili Bayo, alisema kuwa Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali imekuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki za watoto na kutoa elimu ya kupambana na ukatili katika jamii.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Mkoa wa Kilimanjaro, Ndg. Baraka Mduma, alishukuru Serikali na wadau wa maendeleo kwa kuanzisha mikakati madhubuti ya ulinzi wa mtoto, ikiwemo uundwaji wa mabaraza ya watoto katika ngazi ya mkoa na halmashauri.

Aidha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika hufanyika kila mwaka tarehe 16 Juni, kwa lengo la kuhamasisha jamii kulinda na kutetea haki za watoto barani Afrika.