HOSPITALI ZATAKIWA KUSIMAMIA, KULINDA MIUNDOMBINU ILIYOPO
Na WAF - Bariadi, Simiyu
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amezitaka Hospitali zote nchini kuwa na utamaduni wa kusimamia na kulinda miundombinu iliyopo kwa wivu mkubwa kwakuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya kwa kuboresha miundombinu na vifaa tiba.
Waziri Mhagama amesema hayo leo Juni 15, 2025 alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simuyu kwa lengo la kukagua ubora na huduma zinazotolewa, kuwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika wodi ya mama na mtoto, kukagua ujenzi unaoendelea katika jengo hilo pamoja na kuzungumza na watumishi katika hospitali hiyo.
![]() |
Aidha, Waziri Mhagma amesema Serikali imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 29 kwenye huduma za afya ambapo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Serikali imewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 19.8 hivyo miundombinu iliyopo inapaswa kulindwa kwa wivu mkubwa.
"Ombi langu jingine kwenu ninyi watumishi mzingatie maadili katika utoaji wa huduma zenu, wakataeni wale wanaokwepa kiapo chao cha maadili na kujiingiza kwenye makosa ya jinai, tuzingatie viapo vyetu na kutoa huduma kwa utu na usiri mkubwa," amesisitiza Waziri Mhagama.
![]() |
Katika hatua nyingine, Waziri Mhagama ameitaka Idara ya TEHAMA kusimamia mwenendo mzima wa usimamizi wa shughuli zote za hospitali na kuacha mara moja mapungufu yote yaliyopo katika Idara hiyo.
Jambo jingine, Waziri Mhagama amesema kumekuwa na tatizo la lishe katika mkoa wa Simiyu, ameielekeza hospitali kushirikiana na mkoa kutengeneza mazingira mazuri ya kutoa elimu kwa kina mama badala ya kusubiri hadi watoto wakiwa wagonjwa ili kuhakikisha vifo vyao vinapungua nchini.
DKT. ADESINA AMALIZA ZIARA YA SIKU NNE NCHINI TANZANIA
habariDkt. Adesina aliondoka nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kusindikizwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Mhe. Denis Londo.
Ziara ya Dkt. Adesina nchini imetokana na mwaliko kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa madhumuni ya kutembelea miradi ambayo benki hiyo imetoa fedha ya kuigharamia.
Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato na barabara ya mzunguko ya Dodoma ambayo kwa pamoja Rais Samia na Dkt. Adesina waliitembelea jijini Dodoma Juni 14, 2025.
Dkt. Adesina ni Rais wa 8 wa AfDB na katika uongozi wake amefanya mageuzi makubwa katika benki hiyo na kuifanya kuwa chombo imara, chenye mtaji wa kutosha na utaalamu wa kuchagiza mageuzi ya kiuchumi barani Afrika hususan katika sekta za miundombinu, kilimo, afya, nishati, mabadiliko ya tabianchi na mifumo ya kifedha.
Kutokana na mchango mkubwa alioutoa barani Afrika, Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kilimtunikia Shahada ya Heshima ya Falsafa katika Sayansi katika mahafali ya 55, duru ya kwanza yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam Juni 13, 2025.















MNYETI AWATAKA WAFUGAJI KUFUNGA KISASA KUONGEZA TIJA
habariNa. Stanley Brayton, WMUV
PWANI
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kufuga kisasa ili kuongeza tija katika sekta ya mifugo nchini itakayoendana na mahitaji ya Soko ya sasa.
Akizungumza katika Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo yanayoshirikisha nchi tatu za Tanzania, Kenya na Namibia, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo iliyopo Chalinze Mkoa wa Pwani, Mhe. Mnyeti, amesema Serikali awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa inaendelea kuhamasisha wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kuingia kwenye Ufugaji wa kisasa wenye tija.
“Ni matumaini yangu kuwa wafugaji mtachangamkia fursa hii kwa kutafuta na kununua mbegu bora za mifugo zitakazowaletea tija zaidi kwenye ufugaji wenu kuliko kuendelea na Ufugaji wa kizamani usio na tija.” ameseama Mhe. Mnyeti
Aidha, Mhe. Mnyeti amesema maonesho hayo ya mifugo yamelenga kuhamasisha matumizi ya mbegu bora za mifugo ili kumwezesha mfugaji kuzalisha mazao mengi ya mifugo na kupata faida zaidi ili kuifanya Sekta ya Mifugo iweze kuchangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi wa Taifa na kuwawezesha pato la mtu mmoja mmoja.
Vilevile, Mhe. Mnyeti amesema swala la Malisho ya Mifugo imekuwa changamoto na wafugaji wengi wanatembea na rundo kubwa la mifugo kwa ajili ya kutafuta malisho, lakini Ufugaji wa kisasa utasaidia kuwa na Mifugo michache yenye tija ambayo italeta faida kubwa kutokana na uzito na ubora wa mifugo kuliko kuwa na Mifugo mingi yenye uzito mdogo ambayo haina faida yeyote wala tija.
Katika hatua nyingine Mhe. Mnyeti amewataka wafugaji kutafuta mbegu Bora za Malisho na kuzipanda kwa wingi kwa ajili ya Mifugo yao ili Mifugo iweze kupata chakula Cha kutosha kitakachowafanya kuwa Bora zaidi.
Mhe. Mnyeti amehitimisha hotuba yake kwa kukishukuru Chama cha Wafugaji Ng’ombe Kibiashara, Ranchi ya Mbogo pamoja na wadau wengine kwa kuandaa na kufanikisha maonesho hayo ambayo yameambatana na mnada wa mbegu bora za mifugo zenye tija zaidi kwenye uzalishaji wa Mifugo Bora mana wameungana na Serikali katika kuhamasisha Ufugaji wa kisasa.