MHE. MCHENGERWA AWAFUNDA WALIMU

June 04, 2025 Add Comment

Na John Mapepele

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa rai kwa walimu nchini kuwa wazalendo na kuzingatia weledi ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

WAZIRI MCHENGERWA AWAFUNDA WALIMU AWATAKA WAWE WAZALENDO KUZINGATIA MAADILI

June 04, 2025 Add Comment


Na John Mapepele 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa rai kwa walimu nchini kuwa wazalendo na kuzingatia weledi ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi. 


Mhe. Mchengerwa ametoa rai hiyo kwenye mkutano wa walimu na wadau wa elimu  wa Wilaya ya Rufiji uliofanyika kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Bibi Titi Mohamed, ambapo yeye mwenyewe pia alitunukiwa tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake katika sekta ya elimu wilayani Rufiji.

"Katika hali ya kawaida  Serikali imeboresha mazingira na miundombinu ya sekta ya elimu kilichobaki ni kwa sisi walimu kutanguliza uzalendo ili kuinua kiwango cha elimu katika ngazi zote" . Amesisitiza Mhe. Mchengerwa 


Aidha, amesisitiza walimu kutambua wajibu wao na kwamba Serikali haitaweza kusita kuwachukulia hatua za kinidhamu  Walimu na Maafisa Elimu ambao watakuwa wazembe katika utekelezaji wa majukumu yao.

Katika taarifa ya Wilaya ya Rufiji kwa Mhe. Waziri, iliyoandaliwa na  Mkurugenzi Mtendaji  wa Rufiji, bwana Simon Berege, inaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wanaohitimu darasa la Saba kutoka 3135 mwaka 2020 hadi wanafunzi 3715 mwaka 2024.


Idadi ya shule za Awali na Msingi zimeongezeka  kutoka 48 mwaka 2021 Hadi 63 mwaka 2025 ikiwa ni ongezeko la shule 15 sawa na asilimia 31.3.


Pia vyumba vya madarasa  vimeongezeka  kutoka vyumba 377 mwaka2921 hadi vyumba566 mwaka 2025 ikiwa ni ongezeko la vyumba vya madarasa 189 sawa na asilimia 50. 1

Aidha, katika mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa, Halmashauri ya Mji wa Rufiji imefanikiwa kushinda kwa nafasi ya kwanza katika michezo ya mpira wa miguu, pete na riadha huku ikishika nafasi ya pili kwenye mpira wa mikono hivyo kushika nafasi ya pili ya ujumla katika mashindano hayo.

Katika mkutano huo Mhe.Waziri Mchengerwa alikabidhi makombe hayo kwa shule na baadaye kupokea msaada wa madawati 50 yaliyotolewa na Benki ya CRDB.



UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 95

June 04, 2025 Add Comment



📌 *Dkt. Biteko apongeza; akumbusha Watendaji umuhimu wa tathmini katika kuboresha utendaji kazi*


📌 *Ataka TANESCO kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme; kubuni vyanzo vipya*


📌 *Aziagiza Taasisi chini ya Wizara kuungana kuitekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia*


📌 *Ofisi ya Waziri Mkuu yaipongeza Wizara kutekeleza miongozo ya ufuatiliaji na Tathmini kwa asilimia 100*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza Watendaji wa  Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuimarisha utendaji kazi na hivyo kuifanya Sekta ya Nishati kuwa na matokeo chanya katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo kufuatia tathmini ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati ambayo imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi  wa Wizara/Taasisi umeimarika kwa zaidi ya asilimia 95.


Katika kikao cha Nne cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kilichofanyika jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema kuwa, tathmini hiyo inasaidia  kujiimarisha hasa ikizingatiwa kuwa Sekta ya Nishati ina muhimu mkubwa kiuchumi na kijamii.

“Sekta hii ni muhimu sana nchini kwa kuwa ni Sekta ya huduma na sekta ya uchumi hivyo ikilegalega italeta malalamiko, ningependa kuona sekta hii inaendelea kuwa na matokeo mazuri kwa wananchi.” Amesema Dkt. Biteko

Katika kikao hicho, Dkt. Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuendelea na kasi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme pamoja na kuendelea kutafuta vyanzo vipya vya umeme.


Aidha, ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kasi iliyofanya ya kupeleka umeme vijijini na kuwezesha vijiji vyote kupata umeme pia kwa kuendelea na kasi ya kupeleka umeme vitongojini.

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, Dkt. Biteko amezitaka Taasisi zilizo chini ya Wizara hususan, REA, TPDC na TANESCO kuunganisha nguvu katika kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili ikue na kufanikiwa na hivyo kutimiza lengo la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kuwa wananchi wanahama kutoka matumizi ya Nishati isiyo safi kwenda kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Dkt. Biteko amekipongeza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati  kwa kutekeleza jukumu lao kwa ufanisi na kukumbusha Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake  kuwa, zoezi hilo la tathmini linapaswa kuwa  ni endelevu kutokana na umuhimu wake katika kuboresha utendaji kazi.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith.Kapinga kwa upande wake, amezipongeza Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Idara na Vitengo vya Wizara ya Nishati kwa utendaji kazi wenye kuleta matokeo kama ambavyo tathmini ya utendaji kazi iliyotolewa ilivyoonesha kuwa ufanisi wa kazi umeendelea kuimarika.

Aidha amezitaka Taasisi chini ya Wizara ya Nishati kuibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo la Serikali la kufikisha asilimia 80 ya Watanzania wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema kuwa kikao hicho cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara na Taasisi zake ni cha nne kutoka vikao vivyo vimeanza kufanyika.

Alieleza kuwa, kutoka zoezi la kupima utendaji kazi wa Wizara na Taasisi lianze kufanyika limeleta ufanisi hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya Wizara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini  ya Utendaji wa Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Sakina Mwinyimkuu ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutekeleza miongozo iliyowekwa na Ofisi hiyo ya ufuatiliaji na tathmini ambapo ameeleza kuwa Wizara ya Nishati imetekeleza miongozo iliyowekwa kwa asilimia 100.

Pia amempongeza Dkt. Doto Biteko kwa dhamira yake ya dhati katika kusimamia utendaji kazi wa Serikali hasa Sekta ya Nishati ambayo anaisimamia akiwa ni Waziri wa Nishati.

Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutoa motisha kwa Taasisi na Idara/Vitengo zilizofanya vizuri zaidi katika tathmini ya utendaji kazi hali ambayo inaongeza ari ya kazi.

Taasisi zilizofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) aliyeshika nafasi ya kwanza, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) aliyeshika nafasi ya pili na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) aliyeshika nafasi ya tatu.  

Aidha, Idara/Vitengo vya Wizara ya Nishati vilivyofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni  Kitengo cha Ugavi na Manunuzi (nafasi ya kwanza), Kitengo cha Sheria (nafasi ya pili), na Kitengo cha TEHAMA (nafasi ya tatu).

Mikoa ya Kitanesco iliyofanya vizuri katika tathmni ya utendaji kazi ni Manyara (nafasi ya kwanza), Arusha (nafasi ya pili) na Simiyu (nafasi ya tatu).

Hata hivyo ilielezwa kuwa kwa ujumla ufanisi wa utendaji kazi wa Idara na Vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake umeendelea kuimarika kwa zaidi ya asilimia 95.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt, James Mataragio, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Menejimenti ya Wizara ya Nishati  na Taasisi zake pamoja na   Mameneja  wa Mikoa wa TANESCO.

ZAO LA PAMBA LINAWEZA KUPUNGUZA UMASKINI KUANZIA NGAZI YA KAYA MPAKA TAIFA

June 03, 2025 Add Comment

 


Na Oscar Assenga,TANGA

WANANCHI wanaoishi kwenye maeneo yanayostahimili kilimo cha Pamba wametakiwa kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo ambalo ni la kimkakati la kibiashara kutokana na kwamba linaweza kusaidia kupunguza kiasi cha umaskini kwenye ngazi ya kaya,wilaya na Taifa kwa ujumla

Hayo yalisemwa jana na Afisa wa Bodi ya Pamba Tanzania Alphonce Ngawagala wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya 12 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga.

Alisema kwamba leng la wao kushiriki kwenye maonyesho hayo ni kutangaza fursa zinazopatikana kwenye bodi hiyo kwa kuwaelimisha wananchi maeneo gani yanafaa kulima pamba na pembejeo  zinapatikana kwa utaratibu upi ambao ni bure.

Alisem kwamba pia baada ya mkulima na kuvuna wanaanzisha soko la mkulima ili aweze kuuza mazao yake kwa wakati ili aongeze kipato chake apate awekeze kwenye mambo mengine ya kimaendeleo.

Aidha alisema kwamba bodi hiyo imepewa dhamana ya kusimamia usindikaji,uzalishaji na kusimamia masoko pamoja na kuelimisha wananchi maeneo yanayotakiwa kulimwa pamba na pembejeo zinapatikana kwa utararibu upi ambao ni bure na baadae ya kulima hizo wao wanasimamia soko ili wakulima wauze.

“Lakini uchakataji wa Pamba inapokwenda kiwandani napo bodi ipo  kwa ajili ya kusimamia inasimamia kuhakikisha shughuli zote zinafuata utaratibu, sheria na kanuni zilizowekwa ikiwemo kuangalia ubora na usafi unapatikani”Alisema

Alisema wanafanya hivyo ili kumuwezesha yule mchambuaji baada ya kumaliza taratibu zake aweze kupata kibali kama maborota yake yanapelekwa nje ya nchi apeleke kwa wakati kwa kukamailisha tararibu zote.

Mwisho.

VITONGOJI 284 ARUMERU MASHARIKI VYAFIKIWA NA UMEME

June 03, 2025 Add Comment

*📌  Ni kati ya Vitongoji 330 vya Jimbo la Arumeru Mashariki.*


*📌Kapinga asema upelekaji umeme unafanyika kwa  awamu kulingana na upatikanaji wa fedha*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imevifikishia huduma ya umeme Vitongoji 284 katika Jimbo la Arumeru Mashariki kati ya Vitongoji 330.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Juni 03, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mhe. Dkt. John Danielson Pallangyo aliyeuliza ni  lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA katika Vitongoji 37 ambavyo vipo gizani katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

 


"Mheshimiwa Mwenyekiti, Vitongoji 17 vipo katika hatua ya utekelezaji kupitia Mradi wa Ujazilizi (Densification IIB) na mradi wa kupeleka umeme katika Vitongoji Awamu ya Pili  A (HEP IIA), aidha, katika Vitongoji 29 zabuni imetangazwa ili kupata Wakandarasi wa kutekeleza miradi kupitia mradi wa kupeleka umeme Vitongojini Awamu ya Pili B (HEP IIB). 


Amesema kukamilika kwa miradi hiyo, kutawezesha vitongoji vyote vya Jimbo la Arumeru Mashariki kufikiwa na umeme.


Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mhe. Dkt.John Danielson Pallangyo aliyeuliza kuhusu  Kata za Arumeru Mashariki zinazo pata maji kutoka msitu wa mlima Arumeru na kuwa na  flouride ambapo Kampuni ya Kweka imejitolea kuweka mtambo wa kusafisha lakini kinachohitajika ni umeme,   Mhe. Kapinga amesema tayari Serikali imetenga fedha katika mwaka ujao wa fedha kukipelekea umeme wa uhakika Kitongoji cha Seneto Kata ya Legeruki kwa ajili ya kutibu flouride katika maji.

Akijibu swali la Mbunge wa Moshi Vijijini, Mhe. Profesa Patrick Alois Ndakidemi aliyeuliza Serikali itakiunganishia lini umeme Kitongoji cha Orera kilichopo Kijiji cha Mweka, Mhe. Kapinga amesema katika Jimbo la Moshi Vijijini yupo Mkandarasi anayetekeleza miradi ya kupeleka umeme kwenye Vitongoji 15 vya kila Mbunge na kuongeza kuwa kitongoji hicho kipo katika orodha hiyo ya Mkandarasi.


Akijibu swali la Mbunge wa Kondoa Mjini, Mhe. Ally Makoa aliyeuliza Serikali itapeleka lini umeme kwenye mitaa ya Mongoroma, Chandimo na Hachi,  Mhe. Kapinga amesema Serikali imeipelekea umeme mitaa ya Kondoa Mjini ambapo imebaki mitaa hiyo mitatu na kuongeza kuwa itatengwa fedha katika bajeti ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuifikishia mitaa hiyo umeme.


Mhe. Kapinga ameongeza kuwa upelekaji wa umeme unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha na bajeti ambayo imetengwa.


Akijibu swali la Mbunge wa Mwibara, Mhe. Charles Kajage aliyeuliza kuhusu lini Serikali itavipelekea umeme Vitongoji vya Jimbo la Mwibara ambavyo havina umeme, Mhe. Kapinga amesema Jimbo la Mwibara lina miradi ya Vitongoji ambayo inaendelea kutekelezwa. 


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Rita Kabati aliyeuliza kauli ya Serikali kuhusu uwepo wa nguzo Kata ya Ilula Wilaya ya Kilolo toka mwezi wa 11 mwaka jana na hadi leo umeme haujawaka, Mhe. Kapinga amesema hadi kufikia mwezi wa saba eneo hilo litakuwa limefikiwa na huduma ya umeme.