Tanzania na Umoja wa Ulaya kuendeleza Ushirikiano wa Kimkakati

May 22, 2025 Add Comment
Brussels, 21 Mei,2025

Tanzania na Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuendeleza ushirikiano wa kimkakati baina yao.

NCAA YASHIRIKIANA NA JAMII INAYOZUNGUKA HIFADHI KUKABILIANA NA GUGU KAROTI

May 22, 2025 Add Comment


Na Mustapha Seifdine, Karatu.


Katika kuhakikisha mazingira ya hifadhi na shoroba za Wanyamapori yanabaki salama kwa uhifadhi endelevu, Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) imeendelea kushirikiana kwa karibu na wananchi wa vijiji vinavyopakakana na hifadhi ya Ngorongoro kupambana na mmea vamizi hatari uitwao Gugu Karoti (Parthenium hysterophorus) ambao umeota baadhi ya maeneo.

Hatua ya ushirikishaji wa jamii ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa kudhibiti mimea vamizi nchini, hususan katika maeneo ya yaliyohifadhiwa na kuzilinda shoroba muhimu zinazounganisha mifumo ya ikolojia kama vile shoroba ya Upper Kitete inayounganisha hifadhi za Ngorongoro, ziwa Manyara na Tarangire.


Afisa Uhifadhi darala la Kwanza Gregory Mtega kutoka NCAA  akiongoza wananchi wa Kijiji cha Upper Kitete na baadhi ya wataalam ameeleza kuwa  operesheni ya kung’o gugu karoti imefanyika kwa mafanikio makubwa kupitia ushirikiano kati ya NCAA, Halmashauri ya Wilaya ya Karatu na shirika la PAMS na kuongeza kuwa juhudi hizo zinaendelea katika vijiji vingine vinavyopakana na hifadhi kwa ajili ya kuhifadhi uoto wa asili, malisho ya mifugo, na maisha ya wanyamapori.


“Tumekuwa na utaratibu wa kutoa elimu ya uhifadhi shirikishi kwa wananchi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi, NCAA kila mwaka tunatoa miche ya miti bure wananchi wapande kwenye maeneo yao, tunagawa mizinga ya Nyuki kuwainua kiuchumi na kupambana na Wanyama wanaoingia kwenye maeneo hayo, pamoja na programu hizo tumeamua pia kuwahusisha kwenye kung’oa mimea vamizi ili kulinda mfumo wa ikolojia kuwa imaraa, kuimarisha nyanda za malisho na kuwa na uhifadhi endelevu”

Mtega ameongeza kuwa Gugu Karoti ni mmea unaosababisha uharibifu mkubwa wa mazingira kwa kuwa unazaliana kwa kasi (mbegu zaidi ya 40,000 kutoka mmea mmoja!), na ni tishio kwa wanyamapori, mifugo, na hata kilimo cha wananchi hivyo mamlaka imewekeza juhudi za kutosha kukabiliana nalo kw akutumia njia mbalimbali.


Afisa Wanyamapori wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Kornelio Lengai, amepongeza ushirikiano wa NCAA na kueleza kuwa mmea huo umekuwa kikwazo kwa uzalishaji wa chakula na maisha ya wakazi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi hivyo Jitihada za NCAA kushirikiana na wadau mbalimbali ni ishara nzuri katika uhifadhi endelevu kwa vizazi vijavyo.

Kwa upande wake, Emanuel Siriri, mkazi wa kijiji cha Upper Kitete, ameishukuru NCAA kwa kuendelea kutoa elimu na kuwashirikisha wananchi wa kijiji hicho ambapo jitihada hizo si tu zinaleta matumaini bali zimefungua fursa za kiuchumi kwa vijana kupitia kazi za udhibiti wa mmea huo ambao unapodhibitiwa unaboresha shughuli za kilimo na kupata mazao ya kutosha.

DKT. KILABUKO AZINDUA MWONGOZO WA KITAIFA KWA WATOA HUDUMA ZA MAENDELEO YA BIASHARA

May 21, 2025 Add Comment
NA. MWANDISHI WETU - DAR ES SALAAM

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. James Kilabuko amezindua rasmi Mwongozo wa Kitaifa kwa Watoa Huduma za Maendeleo ya Biashara katika hafla iliyofanyika kwenye Hoteli ya Four Points by Sheraton, Jijini Dar es Salaam.

KUPITIA MRADI WA FEMA AILEADERS WABUNGE WABUNIFU NA MAKUNDI MENGINE WAPIGWA MSASA AKILI MNEMBA

May 21, 2025 Add Comment





Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam


Kupitia Mradi wa FemAILeaders, Shirika la Women Political Leaders (WPL), GIZ Makao Makuu, GIZ Tanzania na Omuka imeandaa Mafunzo ya Akili Mnemba “Artificial Intelligence - AI” yaliyoanza Mei  19 hadi 20 mwaka 2025, Dar es Salaam yaliyolenga mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa mtandao,ubunifu na matumizi ya AI.

 

Mafunzo haya yaliwaleta pamoja Wabunge, Wabunifu na Makundi mengine kwa lengo la kuangazia ubunifu na matumizi ya AI, ulinzi wa kimtandao, utatuzi wa changamoto za AI na uhitaji wa kisera.

Delegation ya Bunge iliongozwa na Mhe Salome Makamba na kujumisha Mhe Prof Joyce Ndalichako, Mhe Esther Matiko, Mhe Ng’wasi Kamani na Makatibu wa Kamati za Bunge, Adv Ganjatuni Kilemile na Pius Katabazi.

 

Tanzania imeendelea kuongoza barani Afrika kwa Kuimarisha Uelewa na Ushawishi wa Wabunge Wanawake ili wawe Vinara wa AI hivyo kuchangia kwa Tanzania kunufaika na fursa zinazotokana na Akili Mnemba - AI. Tanzania imechaguliwa kuwa Mfano wa Kuigwa barani Afrika katika eneo hili. 

 

Aidha, Mradi wa FemAILeaders umeweza kufanyika Tanzania kufuatia jitihada za Mhe Neema Lugangira (Mb) ambae pja ni Mwakilishi wa Afrika/Mjumbe Maalum wa Afrika wa Shirika la Women Political Leaders (WPL) hivyo ametumia nafasi hiyo kuileta fursa hii Tanzania.
 

PANGANI WAPONGEZWA KWA KUSHIRIKI VYEMA UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI

May 21, 2025 Add Comment

 

 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Mei 21, 2025 ametembelea na kukagua mwenendo wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali unaoendelea katika mikoa 16 ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar Katika Halmashauri ya Wilaya ya Pangani katika Jimbo la Uchaguzi la Pangani Mkoani Tanga. 

Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni.
Jaji Mwambegele aliwapongeza wananchi wa Pangani kwa namna walivyojitokeza kuboresha taarifa zao na kutazama daftari la awali lililobandikwa katika vituop mbalimbali walivyovitumia wakati wa uboreshaji wa daftari hapo awali. 



Mkazi wa Mtaa wa Kimanga uliyopo Kata ya Kimanga, Wilayani Pangani, Mtwana Juma akionesha kadi yake baada ya Kuboresha 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akimkabidhi Kadi ya Mpiga Kura Mkazi wa Mtaa wa Kimanga uliyopo Kata ya Kimanga, Wilayani Pangani, Mtwana Juma  leo Mei 21, 2025  wakati alipotembelea na kukagua mwenendo wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali unaoendelea katika mikoa 16 ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar Katika Halmashauri ya Wilaya ya Pangani katika Jimbo la Uchaguzi la Pangani Mkoani Tanga. 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Pangani, Ndg. Charles Edward Fussi. 

Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akisalimiana na wananchi wa Pangani waliojitokeza kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye kituo cha Soko la Samaki Pangadeco
Jaji Mwambegele akimsikiliza Mwandikishaji Msaidizi wa Kituo cha Soko la Samaki Pangadeco Wilayani Pangani.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegelakiwa kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata ya Pangani