TANZANIA,MOROCCO KUCHOCHEA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI

May 14, 2025 Add Comment

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morroco

Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini
Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini


Sehemu ya wajumbe mbalimbali alioambatana nao Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko wakati wa mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Morocco, Mei 14, 2025.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali mara baada ya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.

katika mazungumzo hayo, Dkt. Biteko aliongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na mwakilishi katika eneo la Morocco, Mhe. Ali Jabir Mwadini pamoja na Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  nishati vijijini (REA), Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Mei 14, 2025.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morocco.



📌 Matumizi ya teknolojia kupewa kipaumbele Sekta ya Nishati


📌 Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Tanzania na Ufalme wa Morocco zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa matumizi ya teknolojia katika Sekta ya Nishati ili kuiwezesha sekta hiyo kuwa na mchango endelevu nchini.


Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa  Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko alipokutana na Mwenyeji wake Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.


"Mwaka 2016 Tanzania na Morocco zilisaini hati ya makubaliano (MoU) ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya umeme, mafuta na matumizi ya nishati mbadala ili yapewe kipaumbele katika nchi hizo, ". Amesema Dkt. Biteko


Mhe. Dkt. Biteko amesema pamoja na maendeleo ya nishati yaliyofikiwa, bado nchi inahitaji uwekezaji zaidi katika sekta ya nishati mbadala ikiwa na matarajio ya kukuza shughuli za kiuchumi hususan katika sekta za viwanda na madini jambo ambalo linahitaji uwekezaji wa kimkakati zaidi katika sekta ya nishati.


Ametaja mambo mengine ni pamoja na kubadilishana uzoefu miongoni mwa wataalam katika sekta ya nishati ikilenga kuifanya kuwa na tija kwa taifa na uchumi kwa ujumla.


Kwa upande wake, Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali amesema kuwa Tanzania inaweza kubadilisha sura yake kwa kuwa na juhudi za pamoja za kuunganisha rasilimali zilizopo kuhakikisha nishati ya umeme inawafikia wananchi wengi zaidi. 


Amesema hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana gizani hivyo, njia ya kuleta maendeleo na ustawi wa watu ni kuwaangaza maisha yao kwa kupitia sekta ya Nishati.


Aidha, Mhe. Benali amepongeza kwa dhati juhudi za Rais Samia kuwa kinara wa maendeleo ya nishati safi ya kupikia, Tanzania na Afrika kwa ujumla. 


Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi katika eneno la Morocco, Mhe. Ally Mwadini, Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).


Mwisho.

SERIKALI INAENDELEA KUTEKEKEZA MIRADI YA UMEME KWENYE MAENEO YA KIMKAKATI-KAPINGA

May 14, 2025 Add Comment


*📌 Maeneo 300 tayari yamefikkwa*


*📌 Asisitiza gharama ya kuunganisha umeme Vijijini ni shilingi 27,000/-*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye  maeneo ya kimkakati nchini ikiwemo maeneo ya migodi midogo,  maeneo ya uvuvi, Viwanda na  yanayochagiza shughuli za kiuchumi.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 14, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Mwibara, Mhe. Charles Kaijage aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali kuyapelekea umeme maeneo ya uvuvi ili kukuza uchumi wa wananchi wa maeneo hayo.

 

"Mheshimiwa Naibu Spika Mradi huu wa kupeleka umeme maeneo ya kimkakati umefikia zaidi ya maeneo 300 ikiwemo vituo vya afya na visima vya maji kwa maeneo ambayo yanatoa huduma za kijamii."  Amesema  Kapinga

Akijibu swali la Mbunge wa Igunga, Mhe. Nicholas Ngassa aliyeuliza lini Serikali itaanza usambazaji umeme kwenye Vitongoji vya Jimbo la Igunga. Mhe. Kapinga amesema  Jimbo la Igunga lina jumla ya Vitongoji 337 ambapo kati ya hivyo, Vitongoji 95 vimepatiwa umeme.


Ameongeza kuwa, katika Vitongoji 15 Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili A (HEP IIA) na Vitongoji 69 zabuni imetangazwa kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili B (HEP IIB).


Amesema kuwa, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itaendelea kutenga fedha za kuvipelekea umeme vitongoji 158 vilivyosalia.


Amesisitiza kuwa, gharama ya kuunganisha umeme kwa maeneo ya Vijijini ni shilingi 27,000/- na kuongeza kuwa, kuna mradi utakaoanza hivi karibuni unaohusisha Vitongoji ambavyo havina laini kubwa ya umeme na vilivyo na kwenye laini kubwa ya umeme.

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

May 14, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni. 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni. 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Hidaya Gwandu akizungumza 
Mapema kabla ya kuanza kikao hicho Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Mei 14, 2025 amemtembelea na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge ofisini kwake. Mwenyekiti wa Tume na ujumbe wake wapo mkoa wa Pwani kwaajili ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambalo linaingia awamu ya pili katika mikoa 16 ya Tanzania Bara na Zanzibar ukiwepo mkoa wa Pwani pamoja na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga kura.
 ************************
Na Mwandishi wetu, Pwani
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka wananchi kutoka mikoa 16 ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar wanaokwenda kuanza Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu yapili kujitokeza kuboresha taarifa zao pamoja na kutazama daftari la awali la Wapiga Kura lililobandikwa katika vituo walivyotumia kujiandikisha au kuboresha taarifa zao hap[o awali.
 
Hayo yamesemwa leo Mei 14, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku moja ya watendaji wa Uboreshaji kutroka Halmashauri ya Mji wa Kibaha Mkoani Pwani.
 
“Niwasisitize watanzania wote katika mikoa hii 16, wajitokeze kuja kuboresha taarifa zao au kuja kujiandikisha kwasababu baada ya hapa Tume haita boresha tena Daftari…litaboreshwa kuanzia tarehe 16 hadi 22 Mei kwa muda wa siku saba,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 22, 2025.
 
Katika hatua nyingine Jaji Mwambegele amewakumbusha watendaji hao wa uboreshaji ambao ni Waandikishaji Wasaidizi na waendesha vifaa vya Biometriki kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za Uchaguzi wakati wa utekelezaji wa awamu ya pili ya zoezi hilo litakalofanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura.
 
“Nawakumbusha tena kama nilivyowakumbusha katika zoezi lililopita, kwamba katika utekelezaji wa zoezi hili mzingatie sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi, muwe wanyenyekevu kwa wateja mtakao kuwa mnawahudumia,”alisema Jaji Mwambegele.
 
“Zoezi hilo linafanyika kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 16(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024 kinachoipa Tume jukumu la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya uteuzi wa wagombea kwa uchaguzi mkuu unaofuata.
 
Nae Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa amewataka wananchi wa Kibaha na viunga vyake kujitokeza kutazama daftari la awali lililowekwa wazi na kama kuna changamoto waweze kuziboresha wakati huu.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili ulianza kufanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari unafanyika kwa mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza ulihusisha mikoa 15, mzunguko wa pili mikoa 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya mafunzo.
 
Mikoa iliyohusika kwenye mzunguko wa kwanza wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.
 
Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo 7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.
 
Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.
 
Aidha, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 11(1) na (2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume pia ina jukumu la kuandaa Daftari la Awali la Wapiga Kura na kuliweka wazi kwa umma.
 
Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.
 
Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25 Machi, 2025.
Baadhi ya viongozi wa Halmashauri wanaoshughulika na Uboreshaji huo wakiwa katika mafunzo. 
Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.


Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.

Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza. 

Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.

ZAIDI YA BILIONI 17 KUSAMBAZA UMEME VITONGOJINI SINGIDA

May 14, 2025 Add Comment
-Kunufaisha Kaya 3,960 kutoka katika Vitongoji 120 ndani ya Wilaya Tano

KATIBU TAWALA MKOA WA KATAVI, AHITIMISHA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU KITAIFA (GAWE) 2025

May 14, 2025 Add Comment

 

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akizungumza na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akisisitiza jambo kwenye kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Mgeni Rasmi, katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela (wa pili kulia) kikabidhi zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika ufundishaji kwenye shule zao, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yanafanyika kitaifa mkoani Katavi, Halmashauri ya Mpimbwe. Wa kwanza kulia  ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro.

Na Mwandishi Wetu, Katavi

MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET) kwa kushirikiana na wanachama wake, imekusanya nguvu ya pamoja na kujitolea kiasi cha shilingi milioni 35,000,000 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika Halmashauri ya Mpimbwe, mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliofanyika mkoani hapa.

Akizungumza katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, yaliyofanyika kitaifa mkoani Katavi, halmashauri ya Mpimbwe, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania, Bw. Simon Nanyaro alisema wametoa fedha hiyo ili iweze kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu katika Mkoa wa Katavi.

Akifafanua zaidi Bw. Nanyaro alisema wameguswa na muitikio mkubwa wa wazazi/walezi, viongozi wa mila na dini katika shule walizozitembelea wakiwa katika ziara za maadhimisho kwani walijumuika pamoja kujadili mambo mbali mbali muhimu yanayohusu elimu, ikiwemo jitihada kubwa za walimu katika kuendelea kuwafundisha wanafunzi wengi licha ya changamoto zinazowakumba katika mazingira ya ufudishaji hali inayoonyesha kufanya kazi kwa bidii, kujitolea na dhamira ya kuinua kiwango cha Elimu nchini.

"Tumeshuhudia changamoto kadha wa kadha zinazozikabili shule zetu zinazohitaji kushughulikiwa ili kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji: ikiwemo upungufu na uchakavu wa miundombinu ya madarasa kwa baadhi ya shule, upungufu wa walimu, hasa wa kike, ukosefu nyumba za walimu, hasa katika baadhi ya shule, ukosefu wa mabweni kwa wanafunzi, hasa wanaotoka vijiji vya mbali, unaolazimu watoto kutembea hadi kilometa 12 kila siku Kwenda na kurudi shuleni jambo linalochangia utoro na wengine kuacha shule kabisa." Alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro.

Aidha wadau hao wa elimu walipendekeza msaada walioutoa kusaidia kutatua changamoto ya jumla ya madawati 407 meza 10 na viti 10 kwa mchanganuo ufuatao; Madawati 250 yaende shule ya Msingi Migunga, Madawati 47 yasaidie Shule ya Msingi Ikulwe, Madawati 110 yapelekwe katika Shule ya Msingi Minyoso na meza 10 na Viti 10 ziende kwa ajili ya walimu wa shule ya sekondari Mirumba.

Pamoja na hayo walipendekeza viongozi wa Serikali kuandaa mpango na kutenga bajeti ya ujenzi wa hostel za wanafunzi wa kike na wakiume, kujenga matundu ya vyoo, vyumba vya kujisitiri wanafuzi wa kike wakati wa hedhi na upatikanaji wa maji safi na salama; utakaoendana sambasamba na ujenzi wa madarasa ili kukidhi uhitaji uliopo kwa sasa ili kulinda afya na usalama wa Watoto.

Wada wa elimu tunashauri viongozi katika sekta ya elimu ngazi ya wilaya na mkoa kuandaa ziara za mara kwa mara kutembelea shuleni kukutana na wanafunzi, walimu, kamati za shule na wazazi/walezi kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wanafunzi na walimu shuleni.  

"...Tunawahimiza wazazi na walezi kuendelea kuchangia utoaji wa chakula na lishe shuleni ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni na kusoma bila njaa ili kuongeza ufaulu wao na kupunguza utoro shuleni. Kuzingatia sheria na Kanuni za utoaji wa adhabu kwa Wanfunzi kama ilivoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu No. 24 wa mwaka 2002, unaotoa mwongozo namna ya utolewaji wa adhabu ya viboko shuleni. ili kuepuka kutoa adhabu kali za viboko kwa wanafunzi shuleni," alisema Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Nanyaro akiwasilisha taarifa ya wadau wa elimu baada ya kilele cha maadhimisho.

Baadhi ya viongozi na wananchi wakiwa katika hafla ya  Maadhimisho ya kilele cha Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakijisomea vitabu mbalimbali ndani ya Banda la Room to Read Tanzania kwenye kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, katika Halmashauri ya Mpimbwe.