Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

ELIMU YANG'ARA MCHEZO WA RIADHA KATIKA MICHUANO YA SHIMIWI

October 11, 2022 Add Comment

 


Na Oscar Assenga,TANGA


TIMU ya Mchezo wa Riadhaa ya Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imeng’ara katika Mashindano ya Shimiwi yanayoendelea Jijini Tanga.

Wachezaji wa timu ya Elimu ilianza kwa kasi katika mchezo huo wa Riadhaa ambapo wakimbiaji wake walikuwa hari kubwa ya kukimbiza upepo ili kuweza kupata ushindi katika mashindano hayo.

Katika mchezo huo timu ya wanaume imefanya vizuri kwa upande wa mita 100 kupokezana vijiti huku kwenye zile za mita 200 wakiibuka washindi wa pili.

Kwa upande wa michezo mengine timu za Wizara hiyo walipambana mpaka kufikia hatua ya nane bora kwa mchezo wa kuvuta kamba ,mpira wa miguu,mpira wa pete .

Akizungumza kuhusu mashindano hayo Makamu Mwenyekiti ywa timu ya Elimu Sports Deogratius Wenga alisema kwamba mashindano hayo yamekuwa na ushindani mkubwa.

 

WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA SIMBA KWA KUENDELEZA USHINDI LIGI YA MABINGWA AFRIKA

September 18, 2022 Add Comment

 









Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameipongeza Timu ya Simba kwa kushinda kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Simba imeshinda mabao 2-0 dhidi ya timu Nyasa Big Bullet ya Malawi katika mchezo wa marudiani uliochezwa leo Septemba 18, 2022 kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.


Mhe. Mchengerwa ameambatana na Naibu Spika Mhe. Iddi Zungu, Katibu Mkuu wa Wizara yake Dkt. Hassan Abbasi na viongozi mbalimbali wa Serikali.


Amesema watanzania na wanachama wa Simba wanafurahi kuona wanafanya vizuri katika mashindano haya ambapo amefafanua kuwa Mhe. Rais pia anaipongeza timu hiyo.


Ameongeza kuwa timu hiyo imeonyesha uzalendo ambao unapaswa kuendelezwa ili kuitangaza Tanzania Kimataifa.


Ameitaka timu hiyo kutoridhika na ushindi walioupata leo na badala yake iendelee kufanya mazoezi zaidi ili kujinoa hatimaye timu hiyo iingie fainali na kuweza kurejesha kombe nyumbani.


"Ninatoa wito kwa timu yetu kutobweteka na ushindi tulioupata leo, watanzania wanakiu ya ubingwa wa kombe hili. Tunahitaji kujituma na kutanguliza uzalendo ili tuwape raha watanzania". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa


Aidha, Mhe. Mchengerwa amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kufanya uwekezaji katika michezo ili kuwasaidia wananchi kueluka na magonjwa hivyo kujenga afya zao.


Kapteni wa timu ya Simba John Boko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele kwenye michezo.

TANGA PRESS CLUB WAFANYA BONANZA LA KUHAMASISHA SENSA NA KUTAMBUA JUHUDI ZA RAIS SAMIA SULUHU KATIKA MAENDELEO

August 29, 2022 Add Comment

 

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza wakati wa bonanza hilo kushoto ni Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George akifuatiiwa na Bondia Mwakinyo na Afisa Michezo Mkoa wa Tanga Digna Tesha
MKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba akizungumza wakati wa bonanza hilo kushoto ni Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George akifuatiiwa na Bondia Mwakinyo na Afisa Michezo Mkoa wa Tanga Digna TeshaMKUU wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba kulia akiwa na Mwenyekiti wa Tanga Press Club Lulu George na Bondia Hassani Mwakinyo wakifuatilia bonanza hilo
MKUU wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandiliwa akizungyumza wakati wa bonanza hilo

 Na Mwandishi Wetu,TANGA.

Bonanza la Mama Tumeikita lenye lengo la kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi Mkoani Tanga ikiwemo kutambua jitihaza za Rais Samia Suluhu katika maendeleo ya Taifa hapa .

Bonanza hilo ambalo liliandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga *TPC*limefanyika mwishoni mwa wiki Jijini Tanga kwenye viwanja vya Disuza kwa kushirikisha viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Mkuu wa Mkoa Mgumba alisema aliupongeza uongozi wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga chini ya Mwenyekiti wake Lulu George kwa kuanza na kuratibu bonanza hilo ambalo lilikuwa la aina yake.

Alisema ubunifu ambao umefanywa na uongozi wa klabu hiyo unapaswa kuungwa mkono huku akisema bonanza hilo limefanikiwa sana  huku akiwataka viongozi hao kuhakikisha linakuwa endelevu mara kwa mara na kuwahaidi ushirikiano.

“Niwapongeze Tanga Press Club kwa ubunifu huu mkubwa mlioufanya kwa kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi na kutambua juhudi za Rais kuwaletea maendeleo wa Tanga limefanikiwa sana nimpongeza Mwenyekiti wa TPC na viongozi wengine kwa kufanikisha bonanza hilo ambalo limewakutanisha pamoja wanajamii wote wa Tanga,viongozi wa mkoa wilaya mpaka vitongoji na waandishi wa habari”Alisema

Alisema kwamba amefurahishwa kwamba na kupendwa na ujumbe uliobebwa kwenye bonanza hilo mama huku akisisitiza umuhimu wa jamii ya wana Tanga kuhakikisha wanaendelea kushiriki zoezi la Sensa ya watu na Makazi ikiwemo kuendelea kuwahabarisha wana Tanga.

Awali akizungumza wakati wa Bonanza hilo Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa aliushukuru uongozi wa Tanga Press Club kuweza kuliandaa bonanza hilo ambalo limewakutanisha wadau mbalimbali kuishiriki katika michezo ambayo ni muhimu kiafya.

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka waandishi wa habari mkoani humo waendelee kuboresha mahusiano baina yao kwa wao na taasisi mbalimbali za serikali na kupitia wao wanaweza kuwa na mabonanza mbalimbali huku akiwaomba waone umuhimu wa kufanya hivyo.

.TUTAISHANGAZA DUNIA -TIMU YA JUMUIYA YA MADOLA

July 28, 2022 Add Comment


Na John Mapepele, Birmingham - Uingereza

Kocha Mkuu Timothy Kingu wa kikosi cha ndondi kinachoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola ambayo yanaanza rasmi leo Julai 28,2022 amemhakikishia Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na watanzania wote kurejea na medali za ushindi kwenye mchezo huo kwa kuwa wamepata maandalizi ya kutosha.

Akizungumza katika kambi ya wachezaji hao jijini Birmingham, Uingereza amesema wachezaji wake wamepikwa vizuri na watapata hamasa ya kutosha tayari kwa ajili ya pambano lililopo mbele yao.

Aidha, amesema hamasa kubwa inayotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri anayesimamia Michezo nchini, Mhe Mohamed Mchengerwa na wadau mbalimbali kwa sasa zinawafanya wawe na ali na nguvu zaidi ya kushindana kufa na kupona kwenye mashindano haya.

Hadi sasa, tayari Mabondia wawili wa Tanzania Yusuf Changarawe na Kassim Mbundwike wameingia robo fainali za mchezo ya Jumuiya ya Madola inayoanza rasmi leo jijini Birmingham, Uingereza.

Bondia wa tatu wa Tanzania, Alex Isinde sio tu ataanzia mzunguko wa kwanza bali pia atakuwa ndiye Mtanzania wa kwanza kutupa kete kwenye mashindano haya ya 48 ya nchi zilizopata kutawaliwa na Uingereza kesho Julai 29, 2022. 

Isinde atapambana na bondia kutoka Antigua & Barbuda aitwaye Alston Ryan. 

Endapo Isinde atashinda ataungana na wenzie katika robo fainali ambapo mshindi anabeba medali ya shaba.

Endapo wakishinda robo fainali wataingia nusu fainali ambako watawania kunyakua angalau medali za fedha.

Michezo ya Jumuiya ya Madola 2022 inazinduliwa rasmi leo saa mbili usiku kwa saa za huku (Tanzania iko mbele kwa saa mbili).

Tanzania itatupa tena kete zingine siku ya Jumamosi Julai 30, 2022 wakati wanariadha wanne wa mbio ndefu (Marathon) wanawake na wanaume wataingia kuchuana.

Wanariadha hao wa marathon ni Alphonce Simbu, Hamisi Misai, Jakline Sakilu na Failuna Matanga.

Kwenye michezo hiyo Tanzania inawakilishwa na wanariadha tisa, mabondia watatu, wacheza judo wawili, waogeleaji wawili na mnyanyua vitu vizito kwa walemavu (Para-Powerlifting) mmoja.

WAZIRI MCHENGERWA AITEMBELEA TIMU YA JUMUIYA YA MADOLA,AIFUNDA

July 28, 2022 Add Comment

 


Na John Mapepele, Birmingham


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Mohamed Mchengerwa ameitembelea timu ya wachezaji wa Tanzania inayoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola   Birmingham nchini Uingereza na kuitaka kupambana kufa na kupona ili kurejea na medali.

Mhe. Mchengerwa ameyasema haya leo Julai 27, 2022 kwenye kambi ya timu hiyo huku akisisitiza kuwa watanzania wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu Hassan wana matumaini makubwa na timu hiyo hivyo hawana budi kulinda heshima kubwa waliyopewa na taifa kwa ujumla.

"Nawaomba tangulizeni uzalendo ili tuweze kushinda, hii ni vita  tunahitaji kupambana bila kujali idadi yetu wala kitu chochote. Tutashinda." Amesisitiza Mhe. Mchengerwa


Aidha,  amesema dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuinua  na kuendeleza michezo kwa kuwa michezo ni chanzo. Ha ajira na uchumi kwa taifa

" kwa kutambua hilo ndiyo maana kwa mara ya kwanza Serikali  imeamua kutoa fedha nyingi kwa wachezaji watakaopata medali za dhahabu dola za kimarekani 10,000, shaba 7500 na fedha 5000 bado zawadi za jumla" amesisitiza  Mhe. Mchengerwa.

Pia ametumia tukio hilo kutoa pongezi kwa timu ya wanaume na wanawake ya KABBADI kwa kufuzu kuingia kwenye mashindano ya kombe la Dunia yatakayofanyika Oktoba mwaka huu nchini India.

Mhe Mchengerwa ameongozana na Mhe. Musa Sima Mjumbe wa Kamati ya Bunge inayosimamia wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na ndugu Saidi Yakubu Naibu Katibu Mkuu.