Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

MNYETI AWATAKA WAFUGAJI KUFUNGA KISASA KUONGEZA TIJA

June 14, 2025 Add Comment


Na. Stanley Brayton, WMUV 

PWANI


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kufuga kisasa ili kuongeza tija katika sekta ya mifugo nchini itakayoendana na mahitaji ya Soko ya sasa.

Akizungumza katika Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo yanayoshirikisha nchi tatu za Tanzania, Kenya na Namibia, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo iliyopo Chalinze  Mkoa wa Pwani, Mhe. Mnyeti, amesema Serikali awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa inaendelea kuhamasisha wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kuingia kwenye Ufugaji wa kisasa wenye tija.



“Ni matumaini yangu kuwa wafugaji mtachangamkia fursa hii kwa kutafuta na kununua mbegu bora za mifugo zitakazowaletea tija zaidi kwenye ufugaji wenu kuliko kuendelea na Ufugaji wa kizamani usio na tija.” ameseama Mhe. Mnyeti 


Aidha, Mhe. Mnyeti amesema maonesho hayo ya mifugo yamelenga  kuhamasisha matumizi ya mbegu bora za mifugo ili kumwezesha mfugaji kuzalisha mazao mengi ya mifugo na kupata faida zaidi ili kuifanya Sekta ya Mifugo iweze  kuchangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi wa Taifa  na kuwawezesha pato la mtu mmoja mmoja.


Vilevile, Mhe. Mnyeti amesema swala la Malisho ya Mifugo imekuwa changamoto na wafugaji wengi wanatembea na rundo kubwa la mifugo kwa ajili ya kutafuta malisho, lakini Ufugaji wa kisasa utasaidia kuwa na Mifugo michache yenye tija ambayo italeta faida kubwa kutokana na uzito na ubora wa mifugo kuliko kuwa na Mifugo mingi yenye uzito mdogo ambayo haina faida yeyote wala tija.

Katika hatua nyingine  Mhe. Mnyeti amewataka wafugaji kutafuta mbegu Bora za Malisho na kuzipanda kwa wingi kwa ajili ya Mifugo yao ili Mifugo iweze kupata chakula Cha kutosha kitakachowafanya kuwa Bora zaidi.

Mhe. Mnyeti amehitimisha hotuba yake kwa kukishukuru Chama cha Wafugaji Ng’ombe Kibiashara, Ranchi ya Mbogo pamoja na wadau wengine kwa kuandaa na kufanikisha maonesho hayo ambayo yameambatana na mnada wa mbegu bora za mifugo zenye tija zaidi kwenye uzalishaji wa Mifugo Bora mana wameungana na Serikali katika kuhamasisha Ufugaji wa kisasa.



LATRA YATOA MWEZI MMOJA WATOA HUDUMA WA TIKETI MTANDAO KUUNGANISHA MIFUMO NA SERIKALI

June 14, 2025 Add Comment
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) imewataka watoa huduma wa tiketi mtandao kuunganisha mifumo yao na mfumo wa serikali inayosimamiwa na LATRA pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kabla ya Julai 1, 2025.

DKT.BITEKO AWAASA CCM BUKOMBE KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

June 14, 2025 Add Comment


📌 Azindua maduka ya kisasa 31 Ushirombo


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,  Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewaasa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bukombe wasikubali kuvutana na kugombana bali wadumishe amani, kuendelea kuheshimiana na kulinda utu wao hususan katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani.

Dkt. Biteko amesema hayo Juni 14, 2025 wilayani Bukombe, mkoani Geita mara baada ya kuzindua maduka 31 ya kisasa yaliyopo katika eneo la Ofisi za CCM wilayani humo.

“Naomba niwakumbushe tena kwa sasa tunaukaribia mwezi wa Oktoba, 2025. Tunakaribia kuingia katika zoezi la Uchanguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, niwaombe tu kwamba, zoezi la uchaguzi ni zoezi la mara moja, lakini maisha yetu sisi yanadumu na yataendelea kudumu na kuna maisha baada ya kampeni na baada ya Uchanguzi. Hivyo, kwa heshima, nawaomba tuendelee kudumisha umoja, upendo na undugu uliopo baina yetu,” amesema Dkt. Biteko.


Katika hatua nyingine, amezungumzia ujenzi wa maduka hayo ya kisasa kuwa ni hatua kubwa kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo la Ushirombo na maeneo mengine ya jirani kwa kuwa ni chanzo cha maendeleo na mzunguko wa fedha katika eneo hilo.

Amesisitiza “ Maduka haya yataongeza mvuto na hivyo kuongeza thamani ya eneo hili la ardhi pamoja na thamani ya jengo. Ukuaji wa eneo letu hili huchangiwa zaidi na shughuli za madini na shughuli nyingine za kiuchumi. Taarifa zinaonesha kuwa, Mkoa wa Geita umeonesha kasi kubwa zaidi ya ukuaji kutokana na shughuli za madini, na watu wanaochimba watapata huduma kwenye hili,”

Aidha, amewapongeza na kuwashukuru Mwenyekiti na Katibu wa CCM Wilaya ya Bukombe na Madiwani 23 kwa ushirikiano wao na kusema kuwa wamefanya kazi kubwa ya kuchangia ujenzi wa maduka hayo na kusema kuwa anafurahishwa kufanya kazi nao akiongeza kuwa wajumbe wa kata wanazotoka wanaweza kuwapima kwa kazi walizofanya. 

Dkt. Biteko amesema kuwa CCM katika wilaya hiyo itaendelea kuunga mkono mawazo mapya yatakayotolewa kwa ajili ya kusaidia maendeleo ambapo ametaja baadhi ya miradi ya ujenzi wa soko, stendi na barabara inayoendelea kujengwa wilayani humo inalenga kukuza uchumi wa wilaya na mkoa kwa ujumla.

Vilevile, Dkt. Biteko awaomba wanachama wa CCM kumuunga mkono kwa kumchagua Rais Samia na mgombea mwenza Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Geita, Nicholous Kasendamila  amewapongeza CCM Wilaya ya Bukombe kwa ujenzi wa maduka hayo na kusema kuwa hilo ni darasa na siasa ni uchumi na ni wajibu wa CCM kukiimarisha chama chao. 


Naye, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Mkoa wa Geita, Evarist Gervas amepongeza Dkt. Biteko kwa kuimarisha Chama katika wilaya  hiyo na kushirikiana vizuri na viongozi wa Chama kwa kuimarisha wilaya hiyo kiuchumi.


Awali akitoa taarifa ya ujenzi wa maduka hayo ya kisasa, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe, Leonard Mwakalukwa amesema kuwa Wilaya hiyo  inatimiza sera ya CCM ya miradi ya uwekezaji na kwa kutambua kauli mbiu ya siasa na uchumi, ilitekeleza wazo la ujenzi wa maboresho ya vibanda hivyo 21 vilivyokuwepo awali liliasisiwa na Mbunge wa jimbo la Bukombe Dkt. Biteko.


Amesema Dkt. Biteko alitoa wito wa kuwa na vitega uchumi zaidi vya Chama cha Mapinduzi na kutunza na kuboresha mandhari ya eneo la CCM la Wilaya ya Bukombe. Ndipo Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe ikapitisha pendekezo hilo.


Ametaja faida za mradi kuwa ni pamoja na CCM wilayani humo kukusanya mapato kwa wingi.


MWISHO

TFS YABORESHA MIUNDOMBINU YA UTALII MSITU WA PUGU KAZIMZUMBWI KUPITIA MRADI WA BIONUWAI

TFS YABORESHA MIUNDOMBINU YA UTALII MSITU WA PUGU KAZIMZUMBWI KUPITIA MRADI WA BIONUWAI

June 14, 2025 Add Comment





Kisarawe, Pwani – Juni 2025

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kupitia Mradi wa Kuimarisha Ustahimilivu wa Bioanuwai ya Misitu ya Mazingira Asilia dhidi ya Matishio ya Mabadiliko ya Tabianchi, unaendelea kutekeleza hatua madhubuti za kuboresha miundombinu rafiki kwa utalii katika maeneo ya hifadhi ya misitu nchini.

Katika Hifadhi ya Msitu wa Pugu Kazimzumbwi, moja ya misitu ya asili ya pekee inayopatikana karibu kabisa na Jiji la Dar es Salaam, mradi huu unajenga jengo la kisasa la mbao kwa ajili ya mapumziko ya watalii. Jengo hilo, lenye ukubwa wa mita za mraba 72, litakuwa na sehemu tatu za kupumzikia wageni na lina uwezo wa kuhudumia hadi watu 50 kwa wakati mmoja.

Kazi ya ujenzi imefikia asilimia 55 na inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 26 Juni 2025 kwa gharama ya shilingi milioni 120. Kukamilika kwa jengo hili kutakuwa hatua muhimu ya kuboresha huduma kwa wageni na kuongeza mvuto wa utalii wa misitu katika Ukanda wa Pwani.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya kazi, Msimamizi wa Ujenzi, Bw. Fredrick Chakyi alisema kuwa mradi sasa unasonga mbele kwa kasi baada ya changamoto za mvua zilizokuwepo awali kupungua.

“Awali mvua zilikuwa changamoto kubwa, lakini hali sasa ni shwari. Tunatarajia kukamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa,” alisema Chakyi.

Kwa upande wake, Mhifadhi wa Misitu wa Wilaya ya Kisarawe, Bw. Baraka Mtewa, alieleza kuwa uwekezaji huo ni sehemu ya mkakati mpana wa TFS wa kuimarisha utalii wa misitu na kuhifadhi bioanuwai kwa njia endelevu.

“Mradi huu utasaidia kuvutia watalii wa ndani na nje ya nchi, kuongeza mapato ya hifadhi, na kuchochea maendeleo ya kijamii kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka Msitu wa Pugu Kazimzumbwi,” alisema Mtewa.

Kwa msaada wa UNDP na ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa Mazingira (GEF), mradi huu unalenga kulinda mazingira ya asili, kuimarisha uthibiti wa mabadiliko ya tabianchi, na kukuza ushirikiano kati ya Serikali, jamii, na wadau wa maendeleo.

TFS inaendelea kushirikiana na sekta mbalimbali ili kuhakikisha kuwa rasilimali za misitu si tu zinahifadhiwa, bali pia zinatumika kwa njia endelevu katika kuleta tija kwa taifa – kijamii, kiuchumi, na kimazingira.






MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

June 14, 2025 Add Comment

Na John Mapepele

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini kuwaongeza wananchi katika maeneo yao kufanya "jogging" na mazoezi ili kuimarisha afya.