WAZIRI MKENDA AVALIA NJUGA SAKATA LA MADEREVA KWENDA QATAR
habariWaziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Profesa Adolf Mkenda amesema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Wizara hiyo katika miaka minne ya serikali ya awamu ya sita.
Waziri Mkenda amesema wahitaji hao wa madereva wanatakiwa kujua aina ya magari yaliyopo Tanzania ni ya namna gani, yanayoenda Kongo ni ya namna gani, madereva wa Tanzania wanajifunza nini, hivyo mtu akiwachukua watu nchini na kuwapeleka Qatar ni vizuri kwanza akaangalie, asiwachukue na kuwakimbiza kule halafu wakaenda kupimwa hilo ni jambo la muhimu kulifanya.
“Lakini pia tuna haja ya kuwafundisha magari yote hata yale ambayo hayajaingia nchini lakini sisi tulishatoa maelekezo miaka miwili iliyopita kwamba Chuo cha Ufundi Arusha kiingie makubalianao na makampuni ya magari na tayari wameanza mazungumzo na wengine wanaingia mkataba lakini pia tulishawaambia VETA kufanya jambo hilo” Amekaririwa Prof Mkenda
Hata hivyo amesema hata kwenye magari wanahitaji siyo fundi Mechanical pekee bali wanahitaji fundi ambaye anajihusisha na shughuli zote za mfumo wa magari ya kisasa (Mechatronics).







SERIKALI YAITAKA COMMUNITY NETWORK KUSAMBAZA TEHAMA VIJIJINI
habariTPAWU YATAKA MCHAKATO KIMA CHA CHINI SEKTA BINAFSI UHARAKISHWE
habari
Mwenyekiti TPAWU Taifa Daniel Bariyanka Joachim akizungumza kwenye kikao hicho
Na Godwin Myovela, Morogoro
CHAMA cha
Wafanyakazi Mashambani na Kilimo nchini (TPAWU) kupitia kikao cha Baraza Kuu la
chama hichoTaifa, kimeomba kuharakishwa kwa mchakato unaoendelea wa kupanga kima
cha chini cha mshahara sekta binafsi, kuzingatia maoni ya wadau-sambamba na kuhakikisha
kima hicho kutopungua Tsh. 350,000 kwa mwezi, ili kusaidia kumudu gharama za maisha.
Mwenyekiti
TPAWU Taifa, Daniel Joachim, alitoa tamko hilo wakati wa kikao hicho kilichofanyika
mkoani hapa mwishoni mwa wiki, ambapo pamoja na mambo mengine, alieleza baraza hilo
limezingatia hotuba ya Rais aliyotoa wakati wa kilele cha sherehe za Mei Mosi mwaka
huu, kuhusu utaratibu wa kisheria unaoendelea kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.
“Kufuatia tamko
la Rais mkoani Singida, tunamuomba waziri mwenye dhamana kuharakisha mchakato wa
utafiti wa kima cha chini cha mshahara sekta binafsi na kitangazwe kwenye gazeti
la serikali ili kianze kutumika sambamba na kile cha watumishi wa umma kitakachoanza
Julai Mosi mwaka huu,” alisema Joachim na
kuongeza;
“Wakati wa mchakato huo baraza linamuomba waziri mwenye dhamana pamoja na bodi ya kima cha chini cha mshahara sekta binafsi ifanye maandalizi hayo kwa kuzingatia maoni ya wadau ambao ni waajiri na wafanyakazi.”
Aidha,
baraza hilo limewaomba waajiri wote kuzingatia takwa la sheria la majadiliano mahali
pa kazi ili kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia mikataba ya hali bora za kazi
kwa mujibu wa kifungu cha 68 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini sura ya
366.
Katika hatua
nyingine, Tpawu imekemea na kulaani vitendo vya baadhi ya waajiri ambao hutumia
kima cha chini cha sekta husika kama sababu ya wao kutoongeza mishahara, jambo ambalo
halikubaliki.
“Huu ni mtazamo
potofu sababu unakwamisha lengo la kutungwa kwa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini,
pamoja na Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani Na. 98 vinavyotoa haki ya majadiliano
mahali pa kazi,” alisisitiza Joachim
Hata hivyo,
alimsihi Rais Samia kusaidia wafanyakazi wa sekta binafsi hasa sekta ya kilimo kupata
mshahara unaoweza kuwasaidia kumudu gharama za maisha ya kila siku-mathalani-ikiwa
sekta ya umma watalipwa kima cha chini Tsh.500,000 basi sekta binafsi kima cha
chini kabisa kisipungue Tsh.350,000 kwa mwezi.Katibu
Mkuu TPAWU Taifa John Vahaye akizungumza kwenye kikao hicho.
Wajumbe
Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho