Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI KUENDESHA MAFUNZO MAALUM KWA MAWAKILI WA SERIKALI

May 28, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

OFISI ya Wakili Mkuu wa Serikali inatarajia kuendesha mafunzo kwa Mawakili wa Serikali kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar ambapo mafunzo hayo yatafanyika Juni 2 hadi Juni 4, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa AICC mkoani Arusha.

WAZIRI MKENDA AVALIA NJUGA SAKATA LA MADEREVA KWENDA QATAR

May 28, 2025 Add Comment
Watu wanaowapeleka madereva kufanya kazi nje ya nchi wanawajibu wa kufanya utafiti kujua mahitaji ya eneo wanaloenda ni yapi tofauti na mahitaji ya magari ya Tanzania.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Profesa Adolf Mkenda amesema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Wizara hiyo katika miaka minne ya serikali ya awamu ya sita.

Waziri Mkenda amesema wahitaji hao wa madereva wanatakiwa kujua aina ya magari yaliyopo Tanzania ni ya namna gani, yanayoenda Kongo ni ya namna gani, madereva wa Tanzania wanajifunza nini, hivyo mtu akiwachukua watu nchini na kuwapeleka Qatar ni vizuri kwanza akaangalie, asiwachukue na kuwakimbiza kule halafu wakaenda kupimwa hilo ni jambo la muhimu kulifanya.

“Lakini pia tuna haja ya kuwafundisha magari yote hata yale ambayo hayajaingia nchini lakini sisi tulishatoa maelekezo miaka miwili iliyopita kwamba Chuo cha Ufundi Arusha kiingie makubalianao na makampuni ya magari na tayari wameanza mazungumzo na wengine wanaingia mkataba lakini pia tulishawaambia VETA kufanya jambo hilo” Amekaririwa Prof Mkenda

Hata hivyo amesema hata kwenye magari wanahitaji siyo fundi Mechanical pekee bali wanahitaji fundi ambaye anajihusisha na shughuli zote za mfumo wa magari ya kisasa (Mechatronics).






SERIKALI YAITAKA COMMUNITY NETWORK KUSAMBAZA TEHAMA VIJIJINI

May 27, 2025 Add Comment
Serikali kupitia Tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeitaka Taasisi ya School of Community Network kuongeza juhudi za kuanzisha vituo vya mafunzo ya TEHAMA katika mikoa mbalimbali nchini, hususan vijijini, ili kuwajengea vijana ujuzi wa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidigitali.

LESOTHO WAVUTIWA NA REA

May 27, 2025 Add Comment
-Wampongeza Rais Samia katika suala la uhamasishaji wa nishati safi ya kupikia

TPAWU YATAKA MCHAKATO KIMA CHA CHINI SEKTA BINAFSI UHARAKISHWE

May 27, 2025 Add Comment

 

 Mwenyekiti TPAWU Taifa Daniel Bariyanka Joachim akizungumza kwenye kikao hicho

Na Godwin Myovela, Morogoro

CHAMA cha Wafanyakazi Mashambani na Kilimo nchini (TPAWU) kupitia kikao cha Baraza Kuu la chama hichoTaifa, kimeomba kuharakishwa kwa mchakato unaoendelea wa kupanga kima cha chini cha mshahara sekta binafsi, kuzingatia maoni ya wadau-sambamba na kuhakikisha kima hicho kutopungua Tsh. 350,000 kwa mwezi, ili kusaidia kumudu gharama za maisha.

Mwenyekiti TPAWU Taifa, Daniel Joachim, alitoa tamko hilo wakati wa kikao hicho kilichofanyika mkoani hapa mwishoni mwa wiki, ambapo pamoja na mambo mengine, alieleza baraza hilo limezingatia hotuba ya Rais aliyotoa wakati wa kilele cha sherehe za Mei Mosi mwaka huu, kuhusu utaratibu wa kisheria unaoendelea kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.

“Kufuatia tamko la Rais mkoani Singida, tunamuomba waziri mwenye dhamana kuharakisha mchakato wa utafiti wa kima cha chini cha mshahara sekta binafsi na kitangazwe kwenye gazeti la serikali ili kianze kutumika sambamba na kile cha watumishi wa umma kitakachoanza Julai Mosi mwaka huu,” alisema Joachim  na kuongeza;

“Wakati wa mchakato huo baraza linamuomba waziri mwenye dhamana pamoja na bodi ya kima cha chini cha mshahara sekta binafsi ifanye maandalizi hayo kwa kuzingatia maoni ya wadau ambao ni waajiri na wafanyakazi.”

Aidha, baraza hilo limewaomba waajiri wote kuzingatia takwa la sheria la majadiliano mahali pa kazi ili kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia mikataba ya hali bora za kazi kwa mujibu wa kifungu cha 68 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini sura ya 366.

Katika hatua nyingine, Tpawu imekemea na kulaani vitendo vya baadhi ya waajiri ambao hutumia kima cha chini cha sekta husika kama sababu ya wao kutoongeza mishahara, jambo ambalo halikubaliki.

“Huu ni mtazamo potofu sababu unakwamisha lengo la kutungwa kwa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, pamoja na Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani Na. 98 vinavyotoa haki ya majadiliano mahali pa kazi,” alisisitiza Joachim

Hata hivyo, alimsihi Rais Samia kusaidia wafanyakazi wa sekta binafsi hasa sekta ya kilimo kupata mshahara unaoweza kuwasaidia kumudu gharama za maisha ya kila siku-mathalani-ikiwa sekta ya umma watalipwa kima cha chini Tsh.500,000 basi sekta binafsi kima cha chini kabisa kisipungue Tsh.350,000 kwa mwezi.Katibu Mkuu TPAWU Taifa John Vahaye akizungumza kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho

Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakifuatilia ajenda mbalimbali kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho