Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts
RAIS DKT. SAMIA ATOA BILIONI 42.34 KULIPA FIDIA KWA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA

RAIS DKT. SAMIA ATOA BILIONI 42.34 KULIPA FIDIA KWA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA

May 24, 2025 Add Comment








Na Prisca Libaga RAS Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa kiasi cha shilingi bilioni 42.34 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha ili kumaliza migogoro ya ardhi na uendelezaji wa maeneo mbalimbali katika mkoa huo.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Moshono, Jijini Arusha, Mhe. Makonda amesema fidia hiyo imetolewa kwa maeneo kadhaa yaliyoguswa na miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa barabara, uwanja wa ndege, maeneo ya jeshi, na uchimbaji wa madini.

Katika Jiji la Arusha, eneo la Losirwa lililokuwa chini ya matumizi ya Jeshi limepewa fidia ya shilingi Bilioni 2.27, ambapo fidia hiyo imekwishalipwa, eneo la Oloresho kwaajili ya maandalizi ya mashindano ya AFCON, limetengewa fidia ya shilingi bilioni 7.27, barabara ya Mianzini – Ngaramtoni nayo imelipwa fidia ya shilingi bilioni 3.49 ambapo fedha hizo zimelipwa tayari pamoja na eneo la barabara ya Mirongoine – Olmot limepokea fidia ya shilingi milioni 591.64 ambayo nayo imelipwa.

Aidha, Wilaya ya Arumeru, fidia kwa eneo la Jeshi lililopo Duluti imetolewa kwa kiasi cha shilingi bilioni 7.9 na tayari imelipwa yote kwa walengwa.

Wilaya ya Karatu imepata fidia ya shilingi bilioni 5.9 kwa ajili ya uwanja wa ndege wa Manyara uliopo katika eneo hilo, hatua inayolenga kufanikisha uboreshaji wa miundombinu ya usafiri wa anga.

Kwa upande wa Wilaya ya Monduli, eneo la Engaruka, ambalo linahusishwa na shughuli za uchimbaji wa madini ya magadi soda, limetengewa fidia ya shilingi bilioni 14.9, ikiwa ni sehemu ya uwekezaji wa kimkakati katika sekta ya madini.

Katika hatua nyingine, Mhe. Makonda amewataka viongozi wote wa Mkoa huo kuacha mara moja tabia ya kuwaondoa wananchi kwenye maeneo yao bila kuwapa fidia stahiki, akisisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita inalenga haki, usawa na maendeleo ya watu na ndiyo dhamira ya Rais Dkt. Samia katika kulinda haki za wananchi na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya Taifa.

RAIS DKT.SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI IKULU JIJINI DAR LEO

May 24, 2025 Add Comment

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Prof. Tumaini Joseph Nagu kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia masuala ya Afya kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Blandina Bugazi Kilama kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango anayeshughulikia biashara na ubunifu kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.


Viongozi wateule wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Jaji Mstaafu John Samweli Mgetta kuwa Mjumbe wa Baraza la Maadili kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.

RC BALOZI BATILDA :TAKWIMU NI NGUZO MUHIMU KATIKA MAENDELEO YA NCHI

May 24, 2025 Add Comment

 



Na Oscar Assenga,TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amesema kwamba takwimu ni nguzo na nyenzo muhimu katika kupanda utekelezaji wa mipango mbalimbali maendeleo duniani.

Dkt Batilda aliyasema hayo leo Jijini Tanga wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini (NBS) ambapo alisema kwamba mabazara hayo yana maada mkubwa kwa wafanyakazi.

Ambapo alisema kwamba Serikali inatambua jukumu hilo kubwa la (NBS) kuzalisha na kusambaza pamoja na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa takwimu rasmi kwa ajili ya kupanda utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo katika nchi.

Alisema kutokana na hilo wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa utashi wake mkubwa wa kisiasa alionao katika kuendeleza Tasnia ya Takwimu nchini na wote wameona mafanikio yake .

“Wote tunaona kwa namna ya kipekee  Serikali ya awamu ya sita  imekuwa mstari wa mbele kuwezesha uzalishaji wa takwimu rasmi pamoja na matumizi ya takwimu katika mipango mbalimbali ya maendeleo na Dira bila takwimu hakuna kinachoendelea”Alisema

Hata hivyo aliipongeza timu ya  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa  umoja na mshikamano kutokana na takwimu huanzia katika uzalishaji,uchakataji wake,uhakiki wake mpaka usambazaji wake kutokana na kwamba  mtu moja hawezi kufanya pekee yake hivyo lazima wafanye kazi kwa ushirikiano.

Alisema kwamba wanaendelea kuhamasisha wenzao wajiunge kwebye vyama vya wafan yakazi hasa tughe ili waweze na kauli kubwa ambavyo itakuwa na maslahi mapana kwa nchi na sisi wenyewe.

Aidha aliwataka kuhakikisha wanafanya kazi kwa tija na uzalendo na kuongea nao waelewe dira na dhima ya taasisi zao na mambo ambayo hawataji kuyaona kwenye taasisi zao ikiwemo uvujaji wa siri.

“Katika mambo ambayo tunawapongeza sana NBS ni usiri mkubwa mlionao kwa kweli mnafanya kazi kubwa na sasa wanakwenda kwenye teknolojia ya habari tunaweza kuwa na usiri lakini mkaingiliwa kuna viti ya kimtandao inabidi tuendelee kujiimarisha sana kwa maana nyie ndio wamebeba roho ya nchi”Alisema

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kwa sababu taarifa zote zipo kwao kwa hiyo wajipange na moja ya maeneo ambayo watapaleka watu wengi kusoma ni masuala ya ulinzi wa kimtandao ili kuungana na kikosi kazi cha Serikali  ili kuhakikisha kwamba taarifa zinakuwa salama na hakuna jambo ambalo litaingizwa.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi (NBS) na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt Amina Msengwa alimshukru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kumteua kuwa Mtakwimu Mkuu wa Serikali anatambua heshima kubwa aliyopewa na kuhaidi kuendelea kusimamia ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa maelekezo na waledi mkubwa ili kuhakikisha majukumu ya NBS yanakwenda sambamba na kasi ya maendeleo ya Rais.

“Nimshukuru Kamisaa Anna Makinda kwa kuendelea kutusaidia katika ushauri lakini kusimamia mkakati wetu wa usambazaji wa matokeo ya Sensa na tunaendelea kujivunia kutoka kwake”Alisema

Aidha alisema kwamba kupitia ofisi ya Taifa ya Takwimu wanataka kuijenga Tanzania yenye maendeleo ya juu kabisa huku akieleza kwamba wamekuwa wakitekeleza sheria na kanuni za zinazoongoza uundaaji na uendeshaji  na u vikao vya mabaraza la wafanyakazi .

Naye kwa upande wake Kamisa wa Sensa na Spika wa Bunge Mstaafu Anna Makinda alisema  baraza la wafanyakazi ndio roho muhimu ambayo inaunganisha wafanyakazi na menejimenti ambapo alitumia wasaa huo kuwataka watumishi kujiunga kwenye mabaraza hayo kutokana na uwepo wa manufaa mbalimbali.

Mwisho

TBS YAWAKUMBUSHA WANANCHI UMUHIMU WA KUJIRIDHISHA NA TAARIFA ZA BIDHAA

May 22, 2025 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutoa msisitizo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiridhisha na taarifa zilizo kwenye vifungashio vya bidhaa kabla ya kununua, likisema taarifa hizo ni sehemu muhimu ya uthibitisho wa ubora na usalama wa bidhaa husika.

TANESCO MUHEZA: KATIKATIKA YA UMEME ILITOKANA NA WIZI WA NYAYA ZA KOPA KWENYE TRANSFOMA

May 22, 2025 Add Comment


Na Paskal Mbunga, MUHEZA.

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) katika wilaya ya Muheza Mkoani Tanga limetolea ufafanuzi katikakatika ya Umeme katika wiki mbili zilizopita ilitokana na kuibiwaa kwa wizi wa nyaya za kopa kwenye Transfoma 18 katika maeneo tofauti tofauti wilayani humo na hivyo kupelekea kuungua na kusababisha umeme kuzima.

Hayo yalisemwa na Meneja wa TANESCO wilaya ya Muheza African Chuwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kutolea ufafanuzi suala hilo lililosababisha baadhi ya wananchi kulalamika, ambapo alisema jitahada zilifanywa ili kuurejesha umeme kwa haraka.

Alisema wakati wa zoezi la kurejesha umeme, walilazimika kufanya majaribio ili kutambua eneo lenye matatizo kwani wilaya hiyo pia inapeleka huduma ya umeme kwenye wilaya za Mkinga na Pangani.

Alibainisha kwamba kwa vile baadhi ya maeneo yanachukua umeme kutoka Muheza, na kwamba ili kubaini tatizo lipo upande upi, ilikuwa lazima kwanza kuurejesha umeme ili endapo itazima, watabaini changamoto ipo wapi. Alieleza kwamba wanaendelea kufuatilia vitendo vya wizi wa waya unaofanywa na baadhi ya watu uliosababisha b umeme kukatika mara kwa mara.

“Lakini niwaambie kwamba tatizo jingine linalosababisha umeme kukatikakatika ni matengenezo makubwa yanayofanyika pale kituo cha kuzalisha umeme Hale yanayopelekea kuzimwa kwa line inayokwenda Muheza na kusisitiza kwamba wanalazimika kuzima umeme wakati wa matengenezo wa line inayotoka Hale kwenda Songa na kwenda Muheza na line inayotoka Kituo cha Hale Songa kwenda Korogwe.

Hata hivyo alibainisha kwamba Ofisi ya TANESCO wilayani Muheza inatoa taarifa kwa wananchi ya uwepo wa matengenezo na kwamba wakati wa matengenezo hayo, umeme huzimwa. Meneja huyo wa TANESCO wilayani hapa alifahamisha kwamba kutakuwa na katikakatika kwa umeme wakati wa matengenezo yanayoendelea kwa kipindi cha miezi minne hadi mwezi Agosti, 2025 ambapo yatakuwa yamekamilika.



(Mwisho)