Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

KAMATI YA USTAWI WA JAMII BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR YATEMBELEA CHUO CHA DMI

April 18, 2025 Add Comment


Na Mwandishi Wetu.


WAJUMBE wa Kamati ya Ustawi wa jamii ya Baraza la wawakilishi Zanzibar wametembelea Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kwa lengo la kujifunza ili waweze kuishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayolenga kujenga Chuo cha mabaharia kwa upande wa Zanzibar.


Akizungumza mara baada ya kutembelea mitambo na vifaa vya kujifunzia na kujifundishia Mwenyekti wa Kamati hiyo Mhe. Sabiha FilFil Thani amesema anaushukuru uongozi wa Chuo kwa ushirikiano waliotoa.

"Tumefanikiwa kujifunza kuhusu namna ya kuendesha Chuo cha Bahari lakini pia kujipanga kuwa na vifaa vya mafunzo vitakavyowezesha kutoa elimu bora pamoja na taaluma kwa wakufunzi watakaotarajiwa kuwa wakufunzi wa chuo hicho" amesema.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar Mhe. Ali Abdul-Gulam Hussein amesema ziara hiyo imekua ya umuhimu mkubwa kwa kutembelea Chuo cha DMI ambacho kimetangulia katika taaluma za ubaharia.


"Hii itawasaidia kuepuka makosa wakati wa ujenzi wa chuo kipya lakini pia kuishauri Serikali ipasavyo hususani katika eneo la vifaa vya kujifunzia ambavyo vina gharama kubwa itakayolazima Serikali kuwekeza fedha nyingi" amesema.

Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam Prof. Tumaini Gurumo amesema kuwa chuo kimefanikiwa kuwaeleza shughuli zinazofanyika hasa eneo la kozi za ubaharia zinazosimamiwa na mikataba ya Kimataifa unaojulikana kama STCW 1978.

Amesema kozi hiyo inalazimu Chuo kuwa na Wakufunzi wabobezi Mabaharia, vifaa vya kujifundishi vinavyojulikana kama Simulators ambazo ni nusu ya uhalisia wa baharini na wanafunzi wa ubaharia kufanya mazoezi ya uhalisia baharini.


Ameongeza kuwa Chuo cha bahari DMI kinasimamiwa na taasisi za Kimataifa na Kitaifa, ambapo Kimataifa DMI inasimamiwa na taasisi iliyothibitishwa na shirika la Kimataifa la Bahari IMO inayojulikana kama DNV inayotazama viwango vya ubora vya elimu vinavyotolewa chuoni na Kitaifa Chuo kinasimamiwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kwa kupande wa mitaala inayotolewa kwa mabaharia.

“Katika kukidhi matakwa ya kitaifa na kimaifa chuo tumefanikiwa kuongeza mitambo ya kisasa ya kujifunzia na kufundishia inayolenga kuhakikisha viwango vya ubora vya elimu vinavyoendana na teknolojia ambapo itawalazimu chuo tarajiwa cha Zanzibar kufuata matakwa hayo. Alisema Prof Tumaini.


Chuo cha DMI ni chuo pekee kinachotoa mafunzo ya ubaharia hapa nchini na chuo kinachotambulika Kitaifa na Kimataifa pia serikali imeweza kukiwezesha chuo hicho kupata mitambo ya kisasa kama vile Full mission engine room and bridge simulator, GMDSS Simulator, High Voltage simulator, leth Mashine na Drilling mashine.

DC SAME MGAMBO NI SILAHA MUHIMU KULINDA TAIFA

April 17, 2025 Add Comment



Na Ashrack Miraji Tanga Raha App 

Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Kasilda Mgeni amewasisitiza vijana waliojitokeza kwa ajili ya kuanza mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba (Mgambo) kutanguliza Uzalendo, kuzingatia matumizi sahihi ya silaha, Uadilifu na kutumia vyema mafunzo watakayoyapata katika kupambana na uhalifu kwenye maeneo yao ikiwemo kupambana na Rushwa.

Mhe. Kasilda amesema hayo Aprili 16, 2025 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya awali ya jeshi la Akiba (Mgambo) kundi la 29/2025 kata ya Mwembe Wilayani Same, ambapo amewasisitiza kuyatendea haki mafunzo hayo.

“Mafunzo haya ni muhimu sana hakikisheni mnayatendea haki na mnayatumia vizuri kwa kutanguliza Uzalendo, Uadilifu, zingatieni matumizi sahihi ya silaha hakikisheni hazitumiki kinyume, pia mafunzo mtakayoyapata msiende kutatumia kwenye uhalifu ninyi muwe sehemu ya kupambana na uhalifu kwenye maeneo yenu” amesema Mhe. Kasilda.

Sambamba na hayo Mhe. Kasilda amesema kuwa vijana wa Jeshi la Akiba (Mgambo) ni muhimu sana katika kulinda usalama wa maeneo mbalimbali hususani maeneo ya Viijijini huku akiwaonya wale watakaotumia vibaya mafunzo hayo kwa kufanya uhalifu kuwa watachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kuwafutia sifa za kuwa Askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo).

Kwa upande wake Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Same Afisa Mteule daraja la pili Emmanuel Shija amesema kuwa masomo yatakayotolewa katika mafunzo hayo ni pamoja na Uraia, utimamu wa Mwili, kuzuia rushwa, mbinu za kivita, huduma ya kwanza, Usomaji ramani, Uhandisi pamoja na mambo mengine yanayolihusu Jeshi la Akiba.

Pia mafunzo hayo kwa vijana yatawasaidia katika kupambana na matumizi ya dawa za kulevya, majanga mbalimbali ikiwemo moto, mabadiliko ya Tabianchi, uhalifu pamoja na kuwasaidia katika kujipatia kipato na ajira.

Katika mafunzo hayo ya Awali ya Jeshi la Akiba (Mgambo) kundi la  29/2025 katika wilaya ya Same hadi sasa idadi ya washiriki imefikia 87 wakiwemo wanaume 72 na wanawake 13, Aidha mafunzo hayo yanatarajia kumalizika mwezi Agosti mwaka huu.




 

DKT. BITEKO ASHIRIKI MKUTANO WA NISHATI WA MAWAZIRI EAPP

April 17, 2025 Add Comment

 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo 17 Aprili, 2025 ameshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Nishati wa kikanda kwa nchi za  Afrika Mashariki ambao ni wanachama wa Umoja wa Soko la pamoja la Kuuziana Umeme na Kuimarisha Mifumo ya Gridi ya EAPP (Eastern Africa Power Pool).

Mkutano huo wa siku 2  umeanza tarehe 16, Aprili 2025 na unatarajiwa kumalizika leo Aprili 17, 2025 jijini Kampala nchini Uganda


TASAC YATOA ELIMU KWA MAWAKALA WA MELI NA FORODHA MKOANI TANGA ILI KUONGEZA UFANISI KATIKA SEKTA YA USAFISHAJI MAJINI

April 17, 2025 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA

SHIRIKA la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) wamekutana na Mawakala wa Meli na Forodha Mkoani Tanga kwa lengo la kutoa uelewa na kukumbushana majukumu yao katika kuchangia kufanikisha ufanisi wa sekta ya usafirishaji kwa njia ya maji.



Akizungumza wakati akifungua kikao hicho Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa njia ya Maji kutoka Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Nelson Mlali alisema wamekutana nao ili kuwaeleza mabadiliko ambayo yanaendelea kutokea na wanachotarajia kutoka kwao na kutoa fursa ya kuweza kutoa maoni yao.

Alisema katika kikao hicho wamejikita kwenye masuala na masharti ya leseni nani anapaswa kupata leseni na anatakiwa afanye nini na asipoifuata jambo gani linaweza kumtokea wakati akiendelea kutoa huduma


Aidha alisema lengo ni kukumbusha kwenye maeneo ambayo wanadhani hawafanyi vizuri ili waweze kufanya vizuri kwa ajili ya faida ya tasnia ya usafiri kwa njia ya maji katika maeneo mbalimbali nchini

“Tunapenda kupunguza malalamiko, migogoro na ucheleweshaji wa huduma za usafiri kwa njia ya maji maana tunapochelewesha huduma labda kwa uzembe au kutokujua “Alisema

“Kwani kufanya hivyo tunazifanya bandari zetu kuwa za gharama kuliko Bandari shindani zilizopo nchi jirani tunajikuta kama nchi na kama wafanyabiashara binafasi wanapoteza na kazi nyingi zinakuwa haziji upande wetu zinaenda kwenye mataifa shindani”Alisema


Hata hivyo alitoa wito kwa wadau kuendelea kushirikiana kwa sababu wote wapo kwenye tasnia hiyo kutokana na kwamba wote wanafanya kazi moja ili baadae waweze kujikita kutoa huduma za usafiri kwa njia ya maji kwa ufanisi mkubwa zaidi bila kuwa na migogoro na bila kucheleweshana na kusababisha gharama kwenye mnyororo wa usafirishaji wa bidhaa na watu kwa njia ya maji .

Awali akizungumza AfisaMwandamizi wa Udhibiti Usafiri wa Njia ya Maji kutoka Shirika la Wakala wa Meli nchini Tasac Mbwana Ng’anzialisema kikubwa walichokifanya na wadau hao ni kutoa elimu na masharti ya leseni na changamoto wanazokumbana nazo katika kutekeleza majuku yao ya kila siku.


Alisema kwamba miongoni mwa changamoto ambazo wanakumbana nazo kuchelewa kurudisha vifaa kwa wenzao jambo ambalo ni kinyume cha sheria .

Alisema wamekubaliana kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na uadilifu bila kugushi nyaraka za wakala huo na kuwaeleza kuhakikisha hawafanyi hivyo ikiwemo matumizi mabaya wa fedha wanazopewa kwa ajili ya kufanya jambo Fulani.

WAZIRI KOMBO AFANYA MAZUNGUMZO NA BANDARI YA KIMATAIFA YA ANTWERP

April 17, 2025 Add Comment



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo ametembelea na kufanya mazungumzo na timu ya uongozi wa Bandari ya Kimataifa ya Antwerp iliyopo nchini Ubelgiji ukiongozwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Bandari hiyo Bw. Stefan Cassimon. 



Mazungumzo hayo yalilenga kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania na Bandari ya Kimataifa ya Antwerp, hususan katika maeneo ya usimamizi wa bandari, fursa za uwekezaji, na programu za kujenga uwezo.

 


Akizungumza katika mkutano huo Waziri Kombo ameeleza kuhusu umuhimu wa Mamlaka hizo mbili za Bandari kushirikiana, akitaja kuwa pamoja na masuala mengine itasaidia kuongeza wigo wa soko na ufanisi kwa manufaa ya pande zote mbili. 

 


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Bandari hiyo Bw. Stefan Cassimon ameeleza kuhusu utayari wa Bandari hiyo wa kushirikiana na Tanzani katika masuala ya uendeshaji na usumamizi wa bandari, akisisitiza kuwa hatua hiyo itakuwa ni kichocheo cha maendeleo ya uendeshaji wa bandari kwa mfumo kisasa na tija zaidi. 

 



Waziri Kombo amehitimisha ziara yake ya kikazi katika Umoja wa Ulaya (EU) ambayo aliianza Aprili 14, 2025.