Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

TUME KUONGEZA BVR VITUO VYENYE WATU WENGI DAR

March 19, 2025 Add Comment

 






Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele akimkabidhi kadi mpya ya Mpiga Kura Ndg. Abubakari Majuto mkazi wa Mzambarauni Kata ya Gongola Mboto Dar es Salaam ambaye ni mlemavu wa viungo alijitokeza kujiandikisha katika kituo cha Shule ya Msingi Mzambarauni leo Machi 18, 2025.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele akimkabidhi kadi mpya ya Mpiga Kura Ndg. Abubakari Majuto mkazi wa Mzambarauni Kata ya Gongola Mboto Dar es Salaam ambaye ni mlemavu wa viungo alijitokeza kujiandikisha katika kituo cha Shule ya Msingi Mzambarauni leo Machi 18, 2025.
Wananchi wakiwa katika moja ya vituo Jijini Dar es Salaam kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo Machi 18, 2025 ametembelea baadhi ya vituo vya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoani Dar es Salaam na kushuhudia mwenendo wa zoezi hilo katiuka siku ya pili.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo Machi 18, 2025 ametembelea baadhi ya vituo vya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoani Dar es Salaam na kushuhudia mwenendo wa zoezi hilo katika siku ya pili.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari, leo Machi 18, 2025, ametembelea na kukagua vituo vya kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, katika Jimbo la Temeke, lililopo Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari, leo Machi 18, 2025, ametembelea na kukagua vituo vya kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, katika Jimbo la Temeke, lililopo Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magdalena Rwebangira leo tarehe 18 Machi, 2025 ametembela vituo mbalimbali vya kuandikisha Wapiga kura Jimbo la Ilala Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuona zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linavyoendelea.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magdalena Rwebangira leo tarehe 18 Machi, 2025 ametembela vituo mbalimbali vya kuandikisha Wapiga kura Jimbo la Ilala Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuona zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linavyoendelea.

Wananchi wa Kata ya Kivule jijini Dar es Salaam wakiwa wamejitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboiresha taarifa zao katika kituo cha Ukooni Kivule.



Na. Mwandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imesema itaongeza mashine za BVR na watendaji katika vituo ambavyo vimebainika kuwa na watu wengi ili kufanikisha uandikishaji na uborteshaji wa taarifa katika Daftari la Kudumu lka Wapiga Kura mkoani Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika siku ya pili ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati akikagua vituo Mkoani Dar es Salaam.

“Leo katika siku ya pili ya zoezi nimetembelea vituo vya uboreshaji na waliojitokeza wamekua wengi mmno kiasi kwamba vifaa vinaonekana ni vichache, nimeagiza vifaa kwamba viongezwe na vituo viongezwe ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo,” alisema Mhe. Jaji wa Rufani Mwambegele.

Jaji Mwambegele akiwa katika Kituo cha Lukooni Chanika Jijini Dar es Salaam alishuhudia uwepo wa wananchi wengi waliojitokeza kwaajili ya kuboresha taarifa zao na kujiandikisha na kutoa maagizo ya kuongezwa kwa mashine za BVR katika kituo hicho.

“Hapa Lukooni eneo la Chanika katika Wilaya ya Ilala kulikua na kituo kimoja katika siku ya kwanza, lakini baada ya kubaini kwamba watu wanakua ni wengi na wanatumia muda mrefu nikaagiza vifaa viongezwe na leo nimepita bado nimeona BVR mbili hazitoshi kwahiyo nimeagiza ziongezwe ili kuweza kukabiliana na changamoto hii,” aliongeza Jaji Mwambegele.

Aidha, Jaji Mwambegele amepongeza wananchi wote waliojitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika siku za mwanzo za zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu kwani kufanya hivyo kunawezesha wao kukamilisha zoezi hilo ndani ya siku saba kama ilivyopangwa.
Nae afisa Mwandikishaji wa Jiji la Dar es Salaam, Faraja Nakua amesema katika Majimbo matatu yaliyopo katika Halmashauriu ya Jiji la Dar es Salaam yenye majimbo ya Ilala, Ukonga na Segerea zoezi linakwenda vyema na wao wamejipanga kufanikisha zoezi hilo.

“Nizidi kuwahamasisha wananchi wa Majimbo ya Ukonga, Ilala na Segerea Jijini Dar es Salaam kuendelea kujitokeza kwa wingi na sisi tumejipanga kutekeleza zoezi hili kama ambavyo Tume imeagiza na vifaa tulivyotakiwa kuongeza vipo tutavipeleka katika maeneo yote yenye changamoto,” alisema Nakua.

Nae Atness Shayo mkazi wa Ukonga Mzambarauni na Hassan Said Mmanga wa Chanika wamepongeza ujio wa zoezi hilo kwani walipoteza kadi zao za mpiga Kura na sasa wameoata kadi zao mpya zitakazoweawezesha kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu baadae mwaka huu.

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi inataraji kuandikisha Wapiga Kura wapya 643,420 mkoani Dar es Salaam ambapo jumla ya vituo 1,757 vinatumika kwenye uboreshaji kwa mwaka huu ikiwa ni ongezeko la vituo 96 katika vituo 1,661 vilivyotumika kwenye uboreshaji mwaka 2019/20.

Aidha Tume imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wote wenye sifa za kuandikishwa wanaandikishwa kwani BVR zaidi ya 5,000 na watendaji wa kutosha wapo kwaajili ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Tume imeshakamilisha uboreshaji wa Daftari katika Mikoa 29. Kwa mujibu wa ratiba, leo Tume inaanza uboreshaji katika mzunguko wa 13 ambao ni mzunguko wa mwisho wa uboreshaji wa Daftari. Mzunguko huu unahusisha Mkoa wa Dar es Salaam pekee.

Kailima amesema kwa mkoa wa Dar es Salaam Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 643,420 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 18.7 ya wapiga kura 3,427,917 waliopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Tume inatarajia baada ya uandikishaji Mkoa wa Dar es Salaam utakuwa na wapiga kura 4,071,337 idadi ambayo inaweza kuongezeka kwa kuwa inawezekana wapo watanzania ambao walikuwa na sifa za kuandikishwa kuwa wapiga kura wakati wa uboreshaji wa Daftari mwaka 2019/20, lakini kwa sababu moja au nyingine hawakuweza kujiandikisha.

Zoezi la uboreshaji wa Daftari linahusu kuandikisha wapiga kura wapya ambao ni raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na zaidi na watakaotimiza umri huo ifikapo tarehe ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, kutoa kadi mpya kwa wapiga kura waliopoteza kadi au kadi zao kuharibika na kutoa fursa kwa wapiga kura walioandikishwa kurekebisha taarifa zao yakiwemo majina na taarifa nyingine.

Uboreshaji wa Daftari pia unahusu kutoa fursa kwa wapiga kura waliopo kwenye Daftari na ambao wamehama, waweze kuhamisha taarifa zao kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuukana uraia wa Tanzania na kifo.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAHITIMISHA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA UMEME MKOANI NJOMBE

March 18, 2025 Add Comment

                                          18 Machi,2026, Njombe


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.
Akizungumza wakati wa hitimisho la ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Dkt. David Mathayo, alisema kamati yake imeridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo, lakini akasisitiza kuwa bado kuna haja ya kuongeza kasi ili kufanikisha lengo la Serikali la kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na gridi ya taifa kwa wakati.

"Tumetembelea vijiji mbalimbali, vikiwemo Mang’oto, Lwangu na Welela, tumeona maendeleo mazuri ya usambazaji wa umeme wa REA. Hata hivyo, bado tunasisitiza kuongeza kasi ya utekelezaji ili wananchi wote wanufaike na huduma hii muhimu," alisema Dkt. Mathayo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha changamoto zote za umeme vijijini zinatatuliwa kwa haraka ili kuboresha maisha ya wananchi.

"Serikali inatambua umuhimu wa umeme kwa maendeleo ya wananchi, hususan katika sekta za elimu, afya, na biashara. Tutaendelea kuweka msukumo ili kuhakikisha vitongoji vyote vinapata umeme kwa wakati, na kwa hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi wa wananchi," alisema Mhe. Kapinga.
Wananchi wa Kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, wameeleza furaha yao kwa kupatiwa umeme kupitia Miradi ya umeme Vijijini inayoendelea kutekelezwa na REA, wakisema kuwa hatua hiyo imewasaidia kuondokana na changamoto ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma muhimu, ikiwemo mashine za kusaga nafaka.

Wakizungumza mbele ya Kamati ya Bunge, wananchi hao walieleza kuwa umeme huo umeleta mabadiliko makubwa katika maisha yao ikiwa ni pamoja na kuwaongezea kipato kwakua wanautumia kwa shughuli za kiuchumi.
Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho, Oliva Kaduma, alisema kuwa uwepo wa umeme umeimarisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa urahisi, hali inayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Diwani wa Viti Maalumu wa Kata ya Mtwango, Rhoda Wanderage, aliishukuru Serikali kwa kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika, akisema kuwa hatua hiyo imesaidia kutatua changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi kwa wakazi wa eneo hilo. 
Pia, alitoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika miradi ya maendeleo inayowanufaisha wananchi wa vijijini.

"Zamani tulilazimika kutembea umbali mrefu kusaga nafaka au kupata huduma nyingine zinazotegemea umeme, lakini sasa kila kitu kipo karibu. Tunamshukuru sana Rais Samia kwa juhudi hizi," alisema Wanderage.
Naye Mkurugenzi wa umeme Vijijini kutoka wakala wa Nishati vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu, alieleza kuwa jumla ya shilingi bilioni 81.6 zinatumika kutekeleza miradi ya usambazaji wa umeme vijijini mkoani Njombe. 

Alibainisha kuwa miradi hiyo ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa kuhakikisha vijiji vyote vinaunganishwa na gridi ya taifa, huku sehemu kubwa ya miradi hiyo ikiwa imekamilika ndani ya muda uliopangwa.
"Tunahakikisha kuwa vitongoji vyote vilivyoainishwa vinapata umeme kwa wakati. Pia, tupo katika hatua za mwisho za kutangaza Zabuni mpya ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya umeme vitongojini," alisema Mhandisi Olotu.
Ziara hiyo kwa upande miradi ya REA imehitimishwa kwa Kamati ya Bunge kupokea taarifa rasmi ya utekelezaji wa miradi ya umeme mkoani Njombe ambapo miradi inayotekelezwa na REA Mkoani Njombe inagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 81.6


MAENEO YA KIJAMII YAMEPEWA KIPAUMBELE KUFIKIWA NA UMEME - KAPINGA

March 18, 2025 Add Comment





Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini umetoa kipaumbele kwenye maeneo yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo Shule, Taasisi, vituo vya afya, zahanati na maeneo ya visima vya maji kwa sababu ni maeneo yanayotoa huduma kwa jamii.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika Vijiji vya Lwangu na Welela vilivyopo katika Halmashauri ya Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kukagua miradi ya umeme vijijini pamoja na kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.


"Kipaumbele ni Taasisi kwa sababu zinatoa huduma zinazotunufaisha sisi wote, tunataka umeme ukatumike kwenye vituo vya afya, zahanati, kwenye visima vya maji lakini pia kwenye shule". Amesema Mhe. Kapinga.


Ameongeza kuwa, kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini hufanyika tathmini ili kuyabaini maeneo yanayotoa huduma za kijamii huku akibainisha hakuna maeneo yanayo rukwa.











WANANCHI NJOMBE WAIOMBA TANESCO, REA KUONGEZA KASI YA KUWAUNGANISHIA UMEME

March 18, 2025 Add Comment

Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Melela Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Mathayo Davidi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtwango mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi, 2025.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Khatib Kazungu akifafanua jambo kwa wananchi wa Kijiji cha Lwangu Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.

 

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wakala wa Nishati Vijijini(REA), Mhandisi Jones Olotu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lupende Mkoani Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakikagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.



 Hamasa ya kuunganishiwa umeme yatokana na kasi ya maendeleo katika sehemu zenye huduma ya umeme



Kapinga asema ifikapo 2030 Wananchi wote watakuwa wamefikiwa na huduma ya umeme



NJOMBE



Wananchi wa Mkoa wa Njombe ambao bado hawajafikiwa na huduma ya umeme wameiomba Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza kasi ya kuwaunganishia umeme katika kaya zao ili waweze kuutumia kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.



Hayo yameelezwa kupitia Viongozi wa Vijiji vya Melela, Mtwango, Lwangu, Lupende na Melela wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini iliyolenga kukagua maendeleo ya mradi wa usambazaji umeme vijijini katika vijiji vya Mkoa wa Njombe tarehe 18 Machi 2025.



Viongozi hao wamesema wananchi wameingia hamasa zaidi ya kuunganishiwa umeme baada ya kuona maendeleo yanazidi kuimarika katika baadhi ya Kaya ambazo tayari zimeunganishiwa umeme.



Aidha, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ambayo imetoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ukiwemo umeme katika maeneo yao ambapo kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakiona kasi kubwa ya maendeleo.



Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amewatoa hofu wananchi hao kwa kuwaeleza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inafikisha umeme kwa wananchi wote ifikapo 2030.



Ameeleza kuwa maendeleo katika maeneo yote hupelekwa kwa hatua kama ilivyo kwa miradi ya umeme lakini lengo la Serikali ni wananchi wote wafikiwe na huduma.



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mathayo David amewasisitiza wananchi kuendelea kutandaza nyaya katika nyumba zao ili miradi ya umeme uiakapowafikia waunganishwe kwa haraka.



Ameeleza kuwa, wananchi ambao hawahitaji kusuka nyaya wafike katika ofisi za TANESCO Ili wapatiwe kifaa cha umeme tayari( UMETA) kwa gharama ya Shilingi elfu 27,000 tu.

WANANCHI NJOMBE WAIOMBA TANESCO, REA KUONGEZA KASI YA KUWAUNGANISHIA UMEME

March 18, 2025 Add Comment

 

Wananchi wa Mkoa wa Njombe ambao bado hawajafikiwa na huduma ya umeme wameiomba Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza kasi ya  kuwaunganishia umeme katika kaya zao ili waweze kuutumia kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hayo yameelezwa kupitia Viongozi wa Vijiji  vya Melela, Mtwango, Lwangu, Lupende na Melela wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini iliyolenga kukagua maendeleo ya  mradi wa usambazaji umeme vijijini katika vijiji vya Mkoa wa  Njombe tarehe 18 Machi 2025.

Viongozi hao wamesema wananchi wameingia hamasa zaidi ya kuunganishiwa umeme baada ya kuona maendeleo yanazidi kuimarika katika baadhi ya Kaya ambazo tayari zimeunganishiwa umeme.

Aidha, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ambayo  imetoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ukiwemo umeme katika maeneo yao ambapo kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakiona kasi kubwa ya maendeleo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amewatoa hofu wananchi hao kwa kuwaeleza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inafikisha umeme kwa wananchi wote ifikapo 2030.

Ameeleza  kuwa maendeleo katika maeneo yote hupelekwa kwa hatua kama ilivyo kwa miradi ya umeme lakini lengo la Serikali ni wananchi wote wafikiwe na huduma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mathayo David amewasisitiza wananchi  kuendelea kutandaza nyaya katika nyumba zao ili miradi ya umeme uiakapowafikia waunganishwe kwa haraka.

Ameeleza kuwa,  wananchi ambao hawahitaji kusuka nyaya wafike katika ofisi za TANESCO Ili wapatiwe kifaa cha umeme tayari( UMETA) kwa gharama ya Shilingi elfu 27,000 tu.