Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

TCRA YATOA ELIMU YA USALAMA MTANDAONI KWA WATU WENYE ULEMAVU MKOA WA SHINYANGA

October 17, 2024 Add Comment

 

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa elimu ya matumizi sahihi na salama ya Mtandao kwa watu wenye mahitaji maalum Mkoa wa Shinyanga ili kuwajengea uelewa wa pamoja namna ya kujilinda dhidi ya uhalifu mtandaoni.

Mafunzo hayo yametolewa leo Alhamisi Oktoba 17,2024 katika ukumbi wa Empire Hotel Mjini Shinyanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum amesemaTCRA inatekeleza majukumu yake ya kuhakikisha watumiaji wote wa mitandao wakiwemo watu wenye ulemavu wanapata huduma salama na sahihi mtandaoni ikiwa ni utekelezaji wa Kampeni Kabambe ya 'Ni Rahisi Sana' yenye lengo la kuwahimiza watanzania wote wajilinde dhidi ya uhalifu mtandaoni.

Amesema Kampeni ya Ni Rahisi Sana imelenga kuwahimiza watanzania wote wajilinde dhidi ya uhalifu mtandaoni akieleza kuwa uwepo wa mazingira salama mtandaoni yatawezesha kufikia malengo ya uchumi wa Kidijiti.

“TCRA inatoa elimu kuhusu usalama wa mtandaoni kupitia kampeni za uhamasishaji kwa umma ikiwemo hii Kampeni ya Ni Rahisi Sana. Kampeni hii inahusisha jinsi ya kutambua uhalifu mtandaoni, uonevu wa mtandaoni na matapeli. Tunatoa mafunzo juu ya kutumia nywila salama, kujilinda dhidi ya utapeli wa kifedha mtandaoni na jinsi ya kuweka mipangilio ya faragha kwenye mitandao ya kijamii”,amesema Mhandisi Imelda.

Amefafanua kuwa TCRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wanaendelea kudhibiti vitendo vya uhalifu na wanaendelea kutoa elimu ili watumiaji wote wa mtandao wanakuwa salama bila kuwaacha nyuma watu wenye ulemavu ili kuhakikisha wanapata haki sawa za usalama wa taarifa binafsi.

Ameongeza kuwa, TCRA ina wajibu wa kuwalinda watumiaji wote wa mtandao na kupitia juhudi hizi, tunahakikisha watu wenye ulemavu wanaweza kutumia mtandao kwa usalama na bila wasiwasi wa kukumbana na uhalifu au ukiukwaji wa haki zao na imeendelea kutoa njia za kuripoti uhalifu na matukio ya hatari mtandaoni kama vile uonevu, udanganyifu au utapeli.


Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum (kulia) akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni.

Akielezea njia za kuwa salama mtandaoni amesema ni pamoja na kuepuka kutoa taarifa za kibinafsi kwa watu usiofahamu na kutumia njia salama za malipo mtandaoni.

“Usiruhusu kitambulisho chako cha NIDA kumsajilia mtu mwingine laini ya simu na usimpatie mtu yoyote namba ya siri (PIN) ya pesa. Kwenye masuala ya mtandao hakuna mambo ya mwili mmoja ndiyo maana kila mtu anasajili kwa kutumia namba yake ya NIDA. Hakiki namba zako kupitia *106# ”,ameeleza Mhandisi Imelda.

Aidha amewashauri watumiaji wa mtandao kulinda taarifa zao kwa kutumia nywila (neno la siri) thabiti akisisitiza kutumia neno la siri tofauti kwa kila akaunti

“Pia tuwaelimishe watoto juu ya hatari zilizomo kwenye mtandao na jinsi ya kutumia mitandao ya kijamii kwa usalama. Tunza faragha yako binafsi pamoja na ile ya familia yako, epuka kuweka kwenye mtandao wa kijamii taarifa binafsi kwa kina. Achana na mambo ya kuweka kila kitu chako mtandaoni, kuweka taarifa zako nyingi mtandaoni ni hatari”,ameongeza Mhandisi Imelda.


Wadau wakifuatilia elimu ya Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao


“Usitekeleze maelekezo yoyote kutoka kwa mtu anayejitambulisha kuwa mtoa huduma ikiwa amekupigia kwa namba ya kawaida kwani Mtoa huduma wako wa mtandao wa simu atawasiliana na wewe kwa namba 100 pekee”,ameeleza.


“Ni rahisi sana kumtambua tapeli kwani atakupigia namba ya kawaida badala ya namba 100, Ni rahisi sana kutoa taarifa kwa mtu anayetaka kukutapeli tuma namba yake kwenye namba 15040. Ni rahisi sana kuwasiliana na TCRA endapo una malalamiko yanayomhusu mtoa huduma wako au ukitaka kupata elimu au ushauri wa kutaka kuanzisha biashara ya mawasiliano piga namba ya bure 0800008272”,amesisitiza Mhandisi Imelda.


Aidha ameshauri wahakikishe program za kifaa cha mawasiliano zimeboreshwa (Updated) zimesasishwa.


“Punguza uharaka unapotuma pesa, hakiki namba unayotaka kuitumia pesa. Kabla ya kufanya malipo au kununua bidhaa mtandaoni, hakikisha taarifa za mtu unayemlipa au tumia huduma ya wakala aliyesajiliwa. Usitume pesa kabla ya kupokea mzigo au kuwa na mawasiliano ya uhakika ili kulinda usalama wa pesa zako, usiwe na haraka”,amesema.


“Epuka kufungua fungua, kubofya viunganishi (links) usivyovifahamu mtandaoni, jiepushe ili kulinda taarifa zako na ukihisi akaunti yako imeingiliwa au kudukuliwa (Hacked) toa taarifa kwa jeshi la polisi”,amesema Mhandisi Imelda.


Aidha amewataka watumiaji wa mtandao kuepuka kusambaza mtandaoni maudhui yaliyokatazwa kama vile udhalilishaji, uongo, uchochezi au upotoshaji lakini pia wahakikishe kabla ya kusambaza taarifa, wajiridhishe kama ni za kweli na zimethibitishwa kutoka chanzo rasmi kama vile chombo cha habari rasmi au ukurasa rasmi wa taasisi.


“Epuka kusambaza maudhui ya ngono mtandaoni kwa sababu inaweza kusababisha madhara kwa watoto na kuharibu mahusiano. Usikubali kutuma picha za utupu hata kama unampenda kiasi gani. Lile wazo la kupiga picha za utupu, unapiga ili iweje, unazipakua, unazitunza za kazi gani? Huu ni ushetani. Tuwe makini haya mambo ni hatari usiombe yakukute mtu kasambaza picha zako za utupu”,ameongeza.


Nao washiriki wa mafunzo hayo wameishukuru TCRA kwa kuwapatia elimu hiyo na kuomba kuendelea kutoa elimu zaidi ili watumiaji wa mitandao wawe salama zaidi.

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga leo Alhamisi Oktoba 17,2024 Mjini Shinyanga - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum (katikati) akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum (katikati) akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum (katikati) akitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Ansila Joackim Materu akizungumza wakati TCRA ikitoa elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao kwa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Shinyanga

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao



Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao




Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao

Wadau wakifuatilia elimu ya Usalama Mtandaoni : Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao


Wadau wakipiga picha ya kumbukumbu

Wadau wakipiga picha ya kumbukumbu.

MAHAFALI YA 54 UDSM : PROF. ANANGISYE AWASIHI WAHITIMU KULETA MABADILIKO NA KUTATUA CHANGAMOTO ZA JAMII

October 05, 2024 Add Comment

 MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye, amewahimiza wahitimu wa chuo hicho kutokaa wanasubiri ajira za serikalini pekee, bali pia kuangalia fursa nyingine za kiuchumi kwa kutumia maarifa na ujuzi waliyojifunza.


Akizungumza katika Mahafali ya 54 ya chuo hicho, Prof. Anangisye alisema elimu inawainua wahitimu na kuongeza thamani yao katika jamii, hivyo ni muhimu kutumia maarifa hayo kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania.

Aliwakumbusha wahitimu umuhimu wa kuwa wabunifu na kuchangia katika maendeleo ya taifa, akirejea kauli ya Mwalimu Julius Nyerere kuhusu matumizi ya rasilimali katika kuwekeza katika elimu.

Alisisitiza kuwa wazazi na wadau wanapaswa kuunga mkono juhudi za serikali katika kuwekeza katika elimu.

Prof. Anangisye alitoa wito kwa wahitimu kurejea ofisini kwa kuzingatia sheria na maadili ya utumishi wa umma, akisisitiza umuhimu wa kuwa na uadilifu katika kazi zao.

Alimshukuru Mkuu wa Chuo, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete, pamoja na Baraza la Chuo na wadau kwa mchango wao katika mafanikio ya mahafali haya.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Balozi Mwanaidi Maajar, aliwasihi wahitimu kuwa na busara na kuongeza bidii katika kutafuta fursa halali za kujiendeleza, huku akisisitiza umuhimu wa kujifunza kutoka kwa changamoto za maisha.






BENKI YA NMB YACHANGIA VIFAA VYENYE THAMANI YA MILIONI 60 SHULE TANO ZA MSINGI WILAYA YA MUHEZA

October 01, 2024 Add Comment




Na Oscar Assenga, Muheza


BENKI ya NMB nchini imetoa imechangia vifaa vyenye thamani ya Milioni 60 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya elimu kwa shule tano za Msingi katika wilaya ya Muheza mkoani Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali


Msaada huo ulikabidhiwa kwa Naibu Waziri Mkuu Dkt Doto Biteko na Afisa Mkuu wa Udhibiti wa Benki ya NMB Doreen Joseph katika Halfa iliyofanyika kwenye uwanja wa Jitegemee wilayanu humo katika wakati Juma la Elimu uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Kampeni ya Mtoto wa leo Samia wa Kesho.

Alivitaja vifaa hivyo ambavyo benki hiyo imechangia kuwa ni Madawati 200 kwa shule ya Msingi Kwemkamba ,Magusuru,Mdote,Ngomeni na Mwembeni ambapo kila shule itapata madawati 50 ,vifaa yengine ni vitanda 40 vya double deka na magodoro 80 kwa ajili ya shule ya Msingi Ngomeni .

Alisema pia wamekabidhi vitanda 32 na magodoro 64 kwa ajili ya msingi Masuguru ambayo vitakuwa chachu katika kuhakikisha wanatatua changamoto ambazo zilikuwepo awali katika shule hizo.

“Nikushukuru Naibu Waziri Mkuu Mhe Dkt Dotto Biteko pamoja na Serikali kwa kazi kubwa inayofanywa kuendelea kuleta maendeleo nchini na sisi Benki ya NMB tupo tayari kushirikiana na Serikali katika kuendeleza maendeleo”Alisema .

Aidha alisema kwamba utoaji wa vifaa hivyo ni sera ya Benki hiyo kuendelea kurudisha kwa jamii ambayo ni sehemu ya faida wanayoipata kama benki inatoka kwa wadau na jamii hivyo hiyo sehemu yao wanatakiwa kurudisha kwa jamii.

“Benki ya NMB inatambua juhudi za serikali katika kusimamia elimu kwa nguvu zote zilizowekwa ili kuboresha utoaji wa mijini na vijiji ikiwemo utoaji wa elimu bure tunaipongeza Serikali kwa hilo sisi kama wadau furaha yetu ni kuunga mkono juhudi hizo za maendeleo kuisaidia jamii yetu”Alisema

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo Naibu Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko alisema kampeni hiyo ya Mtoto wa leo ni Samia wa kesho muhimu ambayo inaonyesha walivyoamua kuwekeza kwenye msingi wa muhimu wa watoto kujiamini na hatimaye kuweza kutimiza ndoto ya kuwa viongozi bora wa baadae.

Naibu Waziri Mkuu huyo aliwataka pia wazazi na walimu kushirikiana kuwaandaa wanafunzi wao kuwa viongozi na wazazi bora kwa siku zijazo huku akieleza kwamba Serikali imewekeza katika sekta ya elimu ili kupata matokeo na maendeleo yanayoendana na uwekezaji huo.

Naye kwa upande wake Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Zainabu Katimba alisema Serikali imejipanga kuwaandaa viongozi bora wa kesho kwa kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu na miundombinu mbalimballi ikiwemo mazingira bora ya kujifunzia.


TEA & TOTALENERGIES MARKETING LTD WAKABIDHI MADWATI 130 WILAYANI KIBITI

September 25, 2024 Add Comment

 Kampuni ya TotalEnergies Marketing Ltd kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wamekabidhi madawati 130 katika shule ya Msingi Jaribuni Mpakani na Shule ya Msingi ya Kitundu za Wilayani Kibiti Mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ushirikiano baina yao katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini.


Hafla ya kukabidhi madawati hayo iliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo katika Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani tarehe 24 Septemba 2024.

Akizungumza katika hafla hiyo Kanali Kolombo ameahidi kuwa madawati hayo yatatunzwa vizuri kwa manufaa ya wanafunzi wa shule hiyo na kuongeza kuwa Wilaya ya Kibiti imekuwa ikinufaika na miradi kadhaa ya TEA ukiwemo wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Kitundu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa TotalEnergies Marketing Tanzania Ltd Bi. Getrude Mpangile amesema madawati hayo 130 ni sehemu ya madawati 200 yenye thamani ya Sh. Milioni 25.9 yaliyotolewa na kampuni hiyo kwa shule tatu za Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam.

Kufuatia msaada huyo Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani imepata madawati 65, Shule ya Msingi Kitundu madawati 65 na Shule ya Msingi Makuburi ya Jijini Dar es Salaam imepata madawati 70.

Bi. Ambangile ameeleza matumaini yake kwamba msaada huo utasaidia kuweka hamasa kwa wanafunzi kujifunza kwa bidii na hivyo kuchangia kukuza ufanisi na ufaulu wa shule zilizonufaika na madawati hayo.

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA, CPA Mwanahamisi Chambega amekumbusha shule zilizonufaika na msaada huo wa madawati kuyatunza vyema.

“Miongoni mwa majukumu ya TEA ni kutafuta raslimali fedha kutoka kwa wadau mbali mbali na kuzigawa katika taasisi za elimu ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia hivyo tunawakumbusha kutunza vifaa hivo”. Amesema CPA Chambega.


Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati katika Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani.
Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA, CPA. Mwanahamisi Chambega katika hafla ya kukabidhi madawati katika Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani.
Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa Total Energies Marketing Tanzania Ltd Bi. Getrude Mpangile (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA CPA. Mwanahamisi Chambega katika hafla ya kukabidhi madawati katika Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani wakifuatilia hafla ya kukabidhiwa madawati 


Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa TotalEnergies Marketing Tanzania Ltd Bi. Getrude Mpangile akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kitundu ambayo pia imenufaika na msaada wa madawati 
Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, Bi. Zakayo Mtenduka (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA, CPA. Mwanahamisi Chambega katika hafla ya kukabidhi madawati katika Shule ya Msingi Jaribu Mpakani
Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo katika picha ya pamoja na viongozi waliohudhuria hafla ya kukabidhi madawati katika Shule ya Msingi Jaribuni Mpakani.
 

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA, CPA. Mwanahamisi Chambega akitoa salaam katika hafla ya kukabidhi madawati katika shule ya Msingi Jaribuni Mpakani.