.heic)
Kijani Bond ilizinduliwa kwa mafanikio nchini Tanzania ikivutia wawekezaji wengi na kukusanya zaidi kwa thamani ya Shilingi Bilioni 171.8 (sawa na Dola za Marekani Milioni 65.7). Kuorodheshwa kwake katika orodha rasmi ya Dhamana za Soko la Hisa la Luxembourg (LuxSE SOL) ni ushuhuda wa kuongezeka kwa mahitaji na uwezo wa Afrika kuwekeza katika miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi huku ikivutia masoko ya mitaji ya kimataifa.
Hafala ya kuorodheshwa kwa hatifungani hiyo imefanyika katika kwenye makao makuu ya LuxSE, ikihudhuriwa na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji na Luxembourg, Bw. Juma Ali Salum, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela, Afisa Mkuu wa Biashara na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya LuxSE, Arnaud Delestienne, pamoja na viongozi wengine waandamizi kutoka Benki ya CRDB, LuxSE na Orbit Securities Tanzania mawakala wa uuzaji wa dhamana hiyo ambayo pia imeorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema: “Kuorodheshwa kwa Kijani Bond si tu hitimisho la mchakato wa kifedha, bali ni mwanzo wa ushirikiano mpya kati ya Afrika na Ulaya katika kufadhili uchumi wa kijani. Tuna fahari kuwa waanzilishi katika nyanja hii kwa kufanikisha ukusanyaji wa zaidi ya Dola Milioni 65.7 kupitia dhamana yetu ya kwanza ya kijani, ambayo ilispata mafanikio ya zaidi ya asilimia 429. Leo, tunaipeleka safari yetu ya uendelevu katika jukwaa la kimataifa, si kwa ajili ya kupata fedha pekee, bali pia kuinua viwango vyetu vya ufadhili endelevu. Huu ni ujumbe kwa dunia: Afrika ipo tayari kuongoza katika ufadhili endelevu kwa ubunifu, uadilifu, na dhamira ya kweli.”
Kijani Bond ni hatifungani ya kwanza ya aina yake nchini Tanzania na miongoni mwa kubwa zaidi Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa wakati wa kutolewa. Fedha zilizopatikana kupitia dhamana hii tayari zinaelekezwa katika sekta mbalimbali zenye mchango mkubwa kwa maendeleo endelevu ikiwemo: Nishati mbadala, Kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, Nishati safi ya kupikia, Majengo rafiki kwa mazingira, Usafiri wa kijani, Maji safi na huduma bora za usafi wa mazingira, pamoja na miradi mingine inayozingatia mabadiliko ya tabia nchi.

Akitoa salamu kutoka kwa Serikali ya Tanzania, Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji na Luxembourg, Juma Ali Salum, alieleza:

Benki ya CRDB ikiwa ni taasisi iliyoidhinishwa na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (UN-GCF), inaendelea kujijengea nafasi thabiti kama kiongozi wa ufadhili endelevu katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Kuorodheshwa kwa Kijani Bond katika Soko la Hisa la Luxembourg kunaiwezesha benki kupanua wigo wake wa kupata mitaji ya kimataifa huku ikiimarisha mchango wake katika kusaidia jitihada za serikali kukuza uchumi wa kijani.


EmoticonEmoticon