MBUNGE UMMY AMSHUKURU RAIS DKT SAMIA KWA UWEKEZAJI WA BANDARI YA TANGA ULIOLETA TIJA KUBWA KWA WANANCHI

September 12, 2024


MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi wa Kata ya Ngamiani Kati wakati wa mkutano wake wa hadhara katika eneo hilo


Na Oscar Assenga,TANGA

MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa uwekezaji mkubwa katika Bandari ya Tanga ambao matunda yake yameanza kuonekana kwa kuiwezesha kupokea shehena kubwa ikiwemo za magari.

Ummy aliyasema hayo leo wakati wa mkutano wake wa hadhara uliofanyika kata ya Ngamiani Kati Jijini Tanga ambapo alisema hilo ni jambo kubwa sana ambalo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa wananchi .

Alisema kwamba uwekezaji huo wa zaidi ya Bilioni 400 uliofanywa na Serikali umekuwa ni chachu kubwa ya kufungua fursa za kiuchumi katika mkoa waTanga na sasa hata Jiji hilo limeanza kubadilika.

Alisema kwamba kutokana na uwekezaji huo utasaidia kuwezesha uchumi wa mkoa wa Tanga kukua kutokana na shehena za mizigo zinapokuwazikishushwa kwenye Bandari hiyo wananchi watanufaika.

"Uwekezaji huu kwetu sisi watu wa Tanga ni mkubwa wenye manufaa makubwa kwani utatusaidia kuweza kurudisha enzi zetu za miaka ya nyuma kukua kiuchumi na hii italeta manufaa kwetu sote hivyo niwatake wana Tanga kuchangamkia fursa hii"Alisema

Aidha alisema kwamba awali kabla ya uwekezaji huo walikuwa wakikosa fursa za kuona meli kubwa zikitia nanga gatini lakini kwa sasa imekuwa ni rahisi kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali.
 
Alisema jambo hilo limesaidia kuwarudisha wafanyabiashara ambao awali walikuwa wakitumia Bandari hiyo na hivyo kupelekea uwepo wa mzunguko wa kibiashara kwenye Jiji hilo.

"Ndugu zangu wakati natafuta kura mwaka 2020 mkoani kwetu hakukuwahi kuwa na meli kubwa tena ambazo zinashusha magari na kutia nanga gatini lakini kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa  Serikali kupitia mimi Mbunge wenu zimeleta matunda na hivyo Rais Dkt Samia Suluhu kutuletea fedha ambazo zimewezesha maboresho makubwa yaliyowezesha meli kubwa kutia nanga"Alisema
 
Hata hivyo aliwataka wakazi wa Jimbo hilo kuchangamkia fursa ya maboresho yaliyofanywa kwa kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali ya kiuchumi,ujasiriamali na kilimo kwa lengo la kuweza kujikwamua kiuchumi zinazotokana na uwekezaji huo.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »