WANAUME ZAIDI YA 1000 WAPASULIWA UGONJWA WA MABUSHA DAR

March 12, 2024

 

Na Andrew Chale,DAR.

WANAUME zaidi ya 1000 Mkoa wa Dar es Salaam, wamefanyiwa upasuaji wa ugonjwa wa mabusha (Ngilimaji) kwenye kambi maalum iliyoendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na Wadau, mwishoni mwa mwaka 2023.


Hayo yamebainishwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Dkt. Mohammed Mang’una wakati wa taarifa kwa Umma iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu  juu ya matokeo ya tathimini ya hali ya kutokomeza ugonjwa wa matende na mabusha nchini hususani mkoani Dar es Salaam.

Dkt. Mohamed Mang’una amesema mkoa wa Dar es Salaam, watu wamekuwa wakipata ugonjwa huo wa matende na mabusha kutokana na hali ya kimaisha ikiwemo kuhamahama, kutokakuwa na elimu sahihi na hali ya kimazingira.


"Takwimu za waliofanyiwa upasuaji wa ugonjwa mabusha ama ngilimaji mwishoni mwa mwaka jana katika kambi tulivuka lengo kwa kuwafanyia upasuaji wanaume zaidi ya 1000.


Upasuaji huu ni mkubwa kwani ulivuka lego lile tulilojiwekea, Lakini pia tunaendelea na zoezi la kutoa elimu ilikuweza kuwafikia watu wote  Dar es Salaam." Amesema Dkt . Mohamed Mang'una.


Awali,  Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametoa taarifa kwa umma na kueleza kuwa, watu zaidi Milioni 3.7 wameweza kuwaepusha na hatari ya kupata maambukizi ya vimelea vya ugonjwa huo wa matende na mabusha.


"Katika tathimini hizo, ni faraja kwetu kuona kuwa tumefanikiwa kuwanusuru wananchi zaidi ya Milioni 3.7 kuepuka na ugonjwa huu matende na mabusha mkoa wa Dar es Salaam.

Nipende kumshukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuunga mkono jitihada za kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, ambapo mwaka jana aliahidi kutoa kiasi cha Dola za kimarekani milioni tatu, katika kipindi cha 2024 ilikufanikisha juhudi za kutokomeza magonjwa hayo.’’ Amesema Waziri Ummy Mwalimu.


Aidha, imeelezwa na wataalamu kuwa, chanzo kikubwa  cha matende na mabusha ni vimelea vya minyoo midogomidogo jamii ya Filaria, mtu akipata minyoo hiyo inaenda kwenye damu na inaweza kusababisha madhara sehemu za haja ndogo na baadae inaweza kusababisha maji kujikusanya kwenye sehemu za korodani.


Ambapo, maji yakizidi ndio unakuta sehemu hizo za siri zinavimba na baadaye hadi ngozi inaweza kuaathiri na kuweka ugumu wakati inapitakiwa kupatiwa matibabu.


Pia sababu nyingine ya magonjwa hayo ni mbu ambao ndio wanaeneza hiyo minyoo, ni sehemu zote Nchini lakini zaidi wanapatikana sehemu za Pwani kutokana na hali ya kimazingira, Wakati tafiti zinaanza waligundua mbu aina ya Culex, hiyo ilibainishwa na wataalam wanaoangalia tabia za mbu na wadudu lakini baadaye ikabainika kuwa ni mbu wa aina zote wanaweza kusambaza vimelea vya minyoo midogomidogo vinavyosababisha matende na mabusha. Hata mbu anayeeneza Malaria anaweza kusambaza vimelea hivyo vya matende na Mabusha.


"Jamii ifanye bidii ya kuzuia mbu kama vile kusafisha mazingira yanayomzunguka, kufukia madimbwi ya maji, kutumia vyandarua, inamaanisha unapojikinga na mbu hujikingi na Malaria peke yake, bali unajikinga dhidi ya Homa ya Denge, Matende na Mabusha na vingine vingi."  Imebainisa taarifa hiyo ya kitaalamu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »