TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LEO

April 24, 2018
NGORONGORO HEROES YAREJEA,WAPEWA MAPUMZIKO SIKU TATU

Timu ya Taifa ya Vijana U20 (Ngorongoro Heroes) imerejea nchini Leo ikitokea nchini DR Congo kwenye mchezo wake wa marudiano wa kufuzu fainali za Africa za Vijana U20 dhidi ya DR Congo.

Wachezaji wa Ngorongoro ambao wamefanikiwa kuivusha timu hiyo kwenda raundi ya pili wamepewa mapumziko ya siku tatu kwa mujibu wa program ya Kocha Mkuu Ammy Ninje.

Katika raundi ya pili Ngorongoro Heroes watacheza dhidi ya Mali mwezi ujao mchezo wa kwanza wakianzia nyumbani.

SERENGETI BOYS KUPIGA NUSU FAINALI KESHO

TIMU YA Taifa ya Vijana U17 (Serengeti Boys) kesho inatupa karata yake muhimu kwenye mchezo wa nusu fainali dhidi ya Kenya.

Mchezo huo utachezwa saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Muyinga nchini Burundi.

Kufuzu hatua ya nusu fainali Serengeti Boys walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Uganda kwenye mchezo wa kwanza kabla ya kuifunga Sudan kwa magoli 6-0 kwenye mchezo wa mwisho wa kundi B.

Tunaitakia kila la kheri Serengeti Boys iweze kufanya vizuri kwenye mchezo huo wa nusu fainali.

Mungu Ibariki Tanzania,Mungu Ibariki Serengeti Boys.



MECHI YA SIMBA NA YANGA MAGETI KUFUNGULIWA MAPEMA,JESHI LA POLISI LAWEKA ULINZI MKALI

Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaowakutanisha Simba na Yanga Jumapili Aprili 29,2018 uliopangwa kuchezwa saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Taifa Tiketi zinaendelea kuuzwa kupitia Selcom.

Yeyote anayetaka kununua tiketi hizo kupitia Selcom anachotakiwa kufanya ni kujaza pesa kwenye kadi yake ya Selcom ambayo inamuwezesha kuweza kununua tiketi hizo kupitia simu ya mkononi.

Mageti yanatarajia kufunguliwa mapema kuanzia saa 2 asubuhi ambapo vyakula na vinywaji vitapatikana ndani.

Jeshi la Polisi limehakikisha ulinzi utakua wa hali ya juu na kuwatahadharisha wale wote wenye nia ya kufanya vitendo vya uovu.

Mamlaka ya Uwanja imethibitisha kuongezeka kwa camera za Uwanjani ambapo sasa zimefikia 109 ambazo zitakuwa zinafuatilia matukio yote

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »