TBL Group yatekeleza kauli mbiu ya ‘Hifadhi mazingira, Muhimu kwa Tanzania ya Viwanda’kwa vitendo

June 04, 2017
MAZE1
Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group muda mfupi baada ya kumaliza zoezi la kupanda miti katika shamba la Baba Wa Taifa kijijini Butiama katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani
MAZE2
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group wakishiriki kupanda miti katika shamba la Baba wa Taifa,Mwalimu Nyerere katika Kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani
KA1
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Mbeya wakifanya usafi katika kata ya Ilomba eneo la Stendi ya Mabasi Jijini Mbeya katika  kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani
KA2
KA4
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Mbeya katika picha ya pamoja baada ya kushiriki kazi za usafi katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani
………………………………………………………
Wafanyakazi washiriki kuadhimisha Siku ya Mazingira

 Katika kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani 2017 Kampuni ya TBL Group iliyopo chini ya kampuni ya kimataifa ya vinywaji ya ABInBev imetekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya siku ya mazingira duniani nchini ya “Hifadhi mazingira, Muhimu kwa Tanzania ya Viwanda, ambapo wafanyakazi wake wameshiriki katika shughuli mbalimbali za maadhimisho.

Wafanyakazi kutoka viwanda vya TBL Group vilivyopo katika mikoa ya  Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Moshi wameshiriki katika shughuli za usafi wa mazingira na upandaji wa miti ambapo baadhi yao wameshiriki katika maadhimisho ya kitaifa kijijini Butiama na kushiriki kampeni ya kupanda miti  iliyoongozwa na Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa mgeni wa heshima.

Akiongea kuhusu mkakati wa kampuni kuhusiana na suala ya mazingira, Afisa wa Masuala Endelevu wa TBL Group, Irene Mutiganzi,alisema mazingira ni suala ambalo kampuni inalipa kipaumbele kikubwa kwa kuwa katika moja ya malengo ya kampuni mama ya TBL Group ya ABiNBEV inayojulikana kama ‘Kujenga Mazingira ya Kuishi katika Dunia iliyo safi’ suala la utunzaji mazingira linatekelezwa kwa vitendo katika maeneo yote  ya biashara za kampuni.

Alisema kwa kufuata mwongozo huu kampuni imejiwekea malengo ya kufanikisha kuhusiana na utunzaji wa mazingira katika maeneo ya matumizi mazuri ya maji katika mchakato wa uzalishaji, kutumia nishati mbadala zisizochafua hewa, kushiriki kampeni za kupanda miti na utunzaji wa vyanzo vya maji,kutumia vifungashio rafiki kwa mazingira.

 Kuhusiana na matumizi ya maji kwa umakini amesema TBL imepunguza matumizi ya maji katika mchakato wa uzalishaji wa bia  kutoka hectolita 6 za maji zilizokua zinatumika katika miaka ya karibuni hadi hectolita 3.6 kwa kila lita moja ya bia inayozalishwa kwa sasa na inaendeleza mkakati wa kupunguza matumizi zaidi ambapo pia imekuwa ikifanya utakatishaji wa maji taka  na kuharibu taka ngumu na nyepesi kwa kutumia teknolojia za kisasa ambazo ni rafiki kwa mazingira.

Mutiganzi alibainisha kuwa kampuni tayari imeanza kutekeleza hatua za kufanya uzalishaji kwa kutumia nishati mbadala zisizokuwa na athari kwa uchaguzi wa hewa ambapo katika kiwanda cha TBL Mwanza kinafanya uzalishaji kwa kutumia mashine zinazozalisha nishati zinazotokana na pumba za mpunga na katika kiwanda cha TBL Mbeya zimefungwa paneli za umeme wa jua ambayo inawezesha kupatikana umeme wa jua unaotumika katika baadhi ya shughuli za mchakato wa uzalishaji.

 Mutiganzi alisema TBL Group inaliangalia suala la utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji sio kwa kiwango cha maslahi ya viwanda vyake kupata malighafi tu bali kwa jamii nzima ambapo kampuni inafanyia biashara  kwa kuwa sera ya kujenga ‘Dunia Maridhawa’ (Better World) inashahabiana  Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa  (SDGs)  na suala la utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji ni moja ya suala ambalo limepewa umuhimu mkubwa.

“Kupitia sera ya kampuni ya ‘Kujenga Dunia Maridhawa’ tumeweza kutekeleza kwa vitendo kanuni za utunzaji wa mazingira, Kuhamasisha jamii unywaji wa kistaarabu na kuunga mkono jitihada za serikali kusaidia kufanikisha changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii hususani katika sekta ya afya,usalama barabarani na elimu na siku zote kampuni na wafanyakazi wote tutaendelea kufanikisha  uwekezaji wenye kuleta manufaa kwa jamii nzima”.Alisema Mutiganzi.

Sera ya kujenga Dunia Maridhawa ya ABInBev ambayo inatekelezwa katika maeneo yake yote ya biashara imejikita katika ufanikishaji wa malengo makuu matatu ambayo ni ‘Dunia inayokua ‘ inayolenga kukuza shughuli mbalimbali na kuwapatia watu fursa ya kujiendeleza kimaisha,’Kujenga Dunia iliyo safi inayolenga kulinda mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo na ‘Kujenga Dunia ya watu wenye Afya ambayo inahimiza  utumiaji wa vinywaji kistaarabu bila kuleta athari kwa jamii.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »