WAZIRI UMMY MWALIMU AFANYA ZIARA YA KIKAZI IFAKARA, MOROGORO

April 06, 2016

8560f637-78b3-467f-95ea-e2f591c0189a
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akiongea na wananchi katika hospitali ya Rufaa ya St. Francis pamoja na wajawazito wanaosubiri kujifungua na ambao wapo chini ya uangalizi wa madaktari.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu amefanya ziara ya siku 1 mjini Ifakara kufuatilia utendaji wa shughuli mbalimbali za Afya Wilayani Kilombero, Morogoro.
Katika ziara hiyo, Mhe Ummy ambae alieambatana na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Mhe Florence Tonguely-Mattli alifungua kozi ya miezi mitatu ya kutoa huduma ya dharura ya afya kwa kina mama wajawazito hususani katika eneo la upasuaji na utoaji wa dawa za usingizi.
Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Taasisi ya Mafunzo ya Kimataifa ya Afya (TTCIH) chini ya Mradi wa “Upatikanaji wa Uzazi Salama Tanzania” yanawahusisha Washiriki 70 kutoka mikoa ya Morogoro, Njombe na Mbeya.
Mhe Ummy pia alikagua shughuli mbalimbali za taasisi za afya ikiwemo kutembelea Taasisi ya Utafiti ya Ifakara (Ifakara Health Institute), Hospitali Teule ya Rufaa ya St. Francis, Chuo cha Uunguzi cha Edgar Malanta na Chuo Kikuu cha Tiba cha St. Francis.
0f1f0d9a-ef44-4d26-bb82-c85e3a577fd9
2da305bb-0c4e-49f9-953c-105cabb0c669
69adfba7-e3c5-42fd-a407-ff0981d8fccd
449c9d9c-134c-4d45-b132-66e5ecab2fb1
Mhe Ummy Mwalimu akibadilishana mawazo na Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Kimataifa ya Afya (TTCIH) Prof. Pemba, Balozi wa Uswisi nchini Mhe Florence Tonguely-Mattli.
3527b65c-f43a-4359-bc0b-9a25fefda589
Picha ya pamoja.
b85fa399-431e-4ade-84c1-c55a1076097e
d7d05480-8495-4f65-ae56-423c9a313630
eea390ef-f89d-458f-92b7-145abb5e19c8
Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na washiriki wakati wa kufungua mafunzo ya miezi mitatu ya kutoa huduma ya dharura ya afya kwa kinamama wajawazito mjini katika taasisi ya TTCIF, Ifakara.
f92df671-ceb3-45a5-8093-a889995f1267

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »