MAMA SALMA KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA NHAYATI SIMON KAMILLIUS MEMBE.

October 07, 2015

Baadhi ya waombolezaji wakishiriki kwenye ibada ya mazishi ya Marehemu Simon Kamillius Membe iliyofanyika katika kijiji cha Rondo huko Lindi Vijijini tarehe 7.10.2015.
Mheshimiwa Benard Membe akitoa heshima za mwisho wakati wa kuuaga mwili wa marehemu kaka yake Ndugu Simon Camillius Membe mara baada ya kufanyika ibada ya mazishi huko Kijijini Rondo tarehe 7.10.2015.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwapa pole wana familia ya Marehemu Simon Kamillius Membe mara baada ya kuhudhuria ibada ya mazishi iliyofanyika huko Rondi, Lindi Vijijini tarehe 7.10.2015.
Baadhi ya waombolezaji wakipita mbele ya jeneza ulimolazwa  mwili wa Marehemu Simon Membe aliyefariki dunia huko India tarehe 3.10.2013,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Benard Kamillius Membe akitoa neo la shukrani kwa viongozi wa serikali, Chama Cha Mapinduzi na wananchi waliojitoa kwa hali na mali katika kufanikisha mazishi ya marehemu kaka yake Bwana Simon Kamillius Membe aliyefariki dunia huko India tarehe 3.10.2015.
Maandamano ya kwenda kuulaza mwili wa Marehemu Simon Membe kwenye nyumba yake ya milele huko kijijini Rondo katika wilaya ya Lindi.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la Marehemu Simon Membe wakati mwa mazishi katika Kijiji Rondo huko Lindi .
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Benard Membe akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu mdogo wake ndugu Simon Membe wakati wa mazishi yake huko Rondo TAREHE 7.10.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Simon Kamillius Membe aliyefariki dunia huko India tarehe 3.10.2015.
PICHA NA JOHN LUKUWI.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »